Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 138
Bible en Swahili de l’est


Louange pour l’accomplissement des promesses

1 Nitakushukuru kwa moyo wangu wote, Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.
Psaumes 111.1 Psaumes 95.3 Jean 10.34-10.36 Psaumes 119.46 Psaumes 82.1
2 Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu, Nitalishukuru jina lako, Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako, Kwa maana umeikuza ahadi yako, Kuliko jina lako lote.
Psaumes 5.7 Matthieu 5.18 Matthieu 24.35 Esaïe 42.21 Psaumes 56.10
3 Siku ile niliyokuita uliniitikia, Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu.
Psaumes 18.6 Philippiens 4.13 Ephésiens 3.16 Colossiens 1.11 2 Corinthiens 12.8-12.10
4 Ee Bwana, wafalme wote wa dunia watakushukuru, Watakapoyasikia maneno ya kinywa chako.
Psaumes 102.15 Psaumes 22.22 Psaumes 22.27 Psaumes 72.11 Esaïe 60.3-60.5
5 Naam, wataziimba njia za Bwana, Kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
Psaumes 21.5 Apocalypse 4.11 Malachie 1.11 Apocalypse 19.1 Sophonie 3.14-3.15
6 Ingawa Bwana yuko juu, amwona mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.
Proverbes 3.34 Jacques 4.6 Esaïe 57.15 Psaumes 113.5-113.6 Esaïe 66.2
7 Nijapokwenda kati ya shida utanihuisha, Utanyosha mkono juu ya hasira ya adui zangu, Na mkono wako wa kuume utaniokoa.
Psaumes 71.20-71.21 Psaumes 23.3-23.4 Esaïe 5.25 Psaumes 85.6 Esaïe 41.10
8 Bwana atanitimilizia mambo yangu; Ee Bwana, fadhili zako ni za milele; Usiziache kazi za mikono yako.
Philippiens 1.6 Psaumes 57.2 1 Thessaloniciens 5.24 Esaïe 26.12 Psaumes 136.1

Cette Bible est dans le domaine public.