Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 113
Bible en Swahili de l’est


Bonté de Dieu pour les faibles

1 Haleluya. Enyi watumishi wa Bwana, sifuni, Lisifuni jina la Bwana.
Psaumes 135.1-135.3 Psaumes 33.1-33.2 Psaumes 135.20 Psaumes 34.22 Apocalypse 19.5
2 Jina la Bwana lihimidiwe Tangu leo na hata milele.
Daniel 2.20 Ephésiens 3.21 Apocalypse 5.13 1 Chroniques 29.10-29.13 Psaumes 41.13
3 Toka maawio ya jua hata machweo yake Jina la Bwana husifiwa.
Malachie 1.11 Esaïe 59.19 Habakuk 2.14 Esaïe 42.10-42.12 Psaumes 72.11
4 Bwana ni mkuu juu ya mataifa yote, Na utukufu wake ni juu ya mbingu.
Psaumes 99.2 Psaumes 8.1 Psaumes 97.9 Esaïe 40.22 1 Rois 8.27
5 Ni nani aliye mfano wa Bwana, Mungu wetu aketiye juu;
Exode 15.11 Psaumes 89.6 Deutéronome 33.26 Esaïe 40.25 Jérémie 10.6
6 Anyenyekeaye kutazama, Mbinguni na duniani?
Psaumes 138.6 Psaumes 11.4 Esaïe 57.15 Esaïe 6.2 Job 15.15
7 Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, Na kumpandisha maskini kutoka jaani.
Psaumes 107.41 1 Samuel 2.7-2.8 2 Samuel 7.8-7.9 Job 2.8 Jacques 2.5
8 Amketishe pamoja na wakuu, Pamoja na wakuu wa watu wake.
Job 36.7 Psaumes 68.13 Philippiens 2.8-2.11 Psaumes 45.16 Apocalypse 5.9-5.10
9 Huweka nyumbani mwanamke aliye tasa, Awe mama ya watoto mwenye furaha.
Psaumes 68.6 Esaïe 54.1 1 Samuel 2.5 Luc 1.13-1.15 Genèse 21.5-21.7

Cette Bible est dans le domaine public.