Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 18.18
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 2 de Bildad

1 Ndipo Bildadi, Mshuhi, akajibu, na kusema,
Job 8.1 Job 2.11 Job 25.1 Job 42.7-42.9
2 Je! Hata lini utayategea maneno mitambo? Fikiri, kisha baadaye tutanena.
Job 16.2-16.3 Job 3.17 Job 3.5-3.6 Jacques 1.19 Job 33.1
3 Twahesabiwa kuwa wanyama kwa sababu gani, Tena kuwa wanajisi machoni pako?
Psaumes 73.22 Job 17.10 Job 17.4 Job 12.7-12.8 Ecclésiaste 3.18
4 Wewe ujiraruaye mwenyewe katika hasira yako, Je! Dunia itaachwa kwa ajili yako wewe? Au jabali litaondolewa mahali pake?
Job 16.9 Job 14.18 Job 13.14 Jonas 4.9 Job 40.8
5 Naam, mwanga wa waovu utazimika, Wala mwali wa moto wake hautang’aa.
Proverbes 13.9 Proverbes 20.20 Proverbes 24.20 Job 21.17 Proverbes 4.19
6 Mwanga hemani mwake utakuwa giza, Nayo taa iliyo juu yake itazimishwa.
Apocalypse 18.23 Psaumes 18.28 Job 21.17
7 Hatua zake za nguvu zitasongwa, Na shauri lake mwenyewe litamwangusha chini.
Proverbes 4.12 Psaumes 18.36 Job 20.22 Job 36.16 Psaumes 33.10
8 Kwani ametupwa katika wavu na miguu yake mwenyewe, Naye huenda juu ya matanzi.
Psaumes 9.15 Job 22.10 Psaumes 35.8 2 Timothée 2.26 Proverbes 29.6
9 Tanzi litamshika kisigino chake, Na mtambo utamgwia.
Esaïe 8.14-8.15 Job 5.5 Job 1.15 Job 1.17
10 Amefichiwa tanzi chini, Na mtego amewekewa njiani.
Psaumes 11.6 Ezéchiel 12.13 Romains 11.9
11 Matisho yatamtia hofu pande zote, Na kumfukuza karibu na visigino vyake.
Job 15.21 Jérémie 6.25 Jérémie 46.5 Job 20.25 Lévitique 26.36
12 Nguvu zake zitaliwa na njaa, Na msiba utakuwa tayari kwa kusita kwake.
Psaumes 7.12-7.14 1 Samuel 2.36 Job 15.23-15.24 2 Pierre 2.3 Psaumes 109.10
13 Utakula via vya mwili wake, Naam, mzaliwa wa kwanza wa mauti atavila via vyake.
Esaïe 14.30 Jonas 2.6 Job 17.16 Genèse 49.3 Apocalypse 6.8
14 Atang’olewa katika hema yake aliyokuwa akiitumaini; Naye atapelekwa kwake mfalme wa utisho.
Psaumes 112.10 Job 24.17 Job 41.34 Job 8.22 Hébreux 2.15
15 Ambacho si chake kitakaa katika hema yake; Kiberiti kitamwagwa juu ya makazi yake.
Psaumes 11.6 Esaïe 34.9-34.10 Deutéronome 29.23 Genèse 19.24 Apocalypse 19.20
16 Chini, mizizi yake itakaushwa; Na juu, tawi lake litasinyaa.
Osée 9.16 Malachie 4.1 Amos 2.9 Esaïe 5.24 Job 15.30
17 Kumbukumbu lake litakoma katika nchi, Wala hatakuwa na jina mashambani.
Psaumes 34.16 Proverbes 10.7 Psaumes 109.13 Proverbes 2.22 Job 13.12
18 Atakimbizwa kutoka mwangani hata gizani, Na kufukuzwa atoke duniani.
Job 10.22 Job 20.8 Esaïe 17.13-17.14 Daniel 4.33 Proverbes 14.32
19 Hatakuwa na mwana wala mjukuu kati ya watu wake, Wala hatasalia mtu hapo alipokaa.
Jérémie 22.30 Esaïe 14.21-14.22 Job 1.19 Job 27.14-27.15 Job 42.13-42.16
20 Hao wanaokaa magharibi watastaajabia siku yake, Kama vile wanaokaa mashariki walivyotiwa hofu.
Psaumes 37.13 Jérémie 50.27 Ezéchiel 21.25 Job 2.12-2.13 Deutéronome 29.23-29.24
21 Hakika ndivyo yalivyo makazi ya wapotovu, Na hapa ni mahali pake asiyemjua Mungu.
Jérémie 9.3 2 Thessaloniciens 1.8 Juges 2.10 Tite 1.16 Jérémie 10.25

Cette Bible est dans le domaine public.