Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 14.5
Bible en Swahili de l’est


1 Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke Siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu.
Job 5.7 Ecclésiaste 2.23 Job 25.4 Psaumes 51.5 Matthieu 11.11
2 Yeye huchanua kama vile ua, kisha hukatwa; Hukimbia kama kivuli, wala hakai kamwe.
Job 8.9 1 Pierre 1.24 Esaïe 40.6-40.8 Psaumes 103.15-103.16 1 Chroniques 29.15
3 Nawe, je! Wafumbua macho yako kumwangalia mtu kama yeye, Na kunitia katika hukumu pamoja nawe?
Psaumes 143.2 Psaumes 144.3 Psaumes 8.4 Romains 3.19 Job 13.27
4 Ni nani awezaye kutoa kitu kilicho safi kitoke katika kitu kichafu? Hapana awezaye.
Jean 3.6 Job 15.14 Psaumes 51.5 Ephésiens 2.3 Romains 5.12
5 Kwa kuwa siku zake zimeamriwa, hesabu ya miezi yake unayo wewe, Nawe umemwekea mipaka yake asiyoweza kuipita;
Psaumes 39.4 Job 21.21 Actes 17.26 Job 12.10 Daniel 5.30
6 Acha kumwangalia yeye, apate kupumzika, Hata atakapoitimiza siku yake, kama aliyeajiriwa.
Job 7.19 Job 7.1-7.2 Psaumes 39.13 Job 7.16 Job 10.20
7 Kwani yako matumaini ya mti, ya kuwa ukikatwa utachipuka tena, Wala machipukizi yake hayatakoma.
Job 19.10 Esaïe 27.6 Esaïe 11.1 Daniel 4.15 Job 14.14
8 Ijapokuwa mizizi yake huchakaa mchangani, Na shina lake kufa katika udongo;
1 Corinthiens 15.36 Jean 12.24 Esaïe 26.19
9 Lakini kwa harufu ya maji utachipuka, Na kutoa matawi kama mche.
Ezéchiel 17.3-17.10 Romains 11.17-11.24 Ezéchiel 17.22-17.24 Ezéchiel 19.10
10 Lakini mwanadamu hufa, huifariki dunia; Naam, mwanadamu hutoa roho, naye yupo wapi?
Job 14.12 Job 7.7-7.10 Job 3.11 Job 17.13-17.16 Proverbes 14.32
11 Kama vile maji kupwa katika bahari, Na mto kupunguka na kukatika;
Esaïe 19.5 Job 6.15-6.18 Jérémie 15.18
12 Ni vivyo mwanadamu hulala chini, asiinuke; Hata wakati wa mbingu kutokuwako tena, hawataamka, Wala kuamshwa usingizini.
Job 10.21-10.22 Apocalypse 21.1 Actes 3.21 Job 3.13 Apocalypse 20.11
13 Laiti ungenificha kuzimuni, Ukanilinda kwa siri, hata ghadhabu zako zitakapopita, Na kuniandikia muda ulioamriwa, na kunikumbuka!
Esaïe 26.20-26.21 Genèse 8.1 Marc 13.32 Actes 17.31 Esaïe 12.1
14 Mtu akifa, je! Atakuwa hai tena? Mimi ningengoja siku zote za vita vyangu, Hata kufunguliwa kwangu kunifikilie.
Job 7.1 Job 13.15 Job 14.5 Apocalypse 20.13 Matthieu 22.29-22.32
15 Wewe ungeita, nami ningekujibu; Ungekuwa na tamaa ya kazi ya mikono yako.
Job 10.3 Job 13.22 1 Jean 2.28 Job 7.21 Psaumes 138.8
16 Lakini sasa wazihesabu hatua zangu; Je! Huchungulii dhambi yangu?
Job 10.6 Job 31.4 Proverbes 5.21 Job 34.21 Jérémie 32.19
17 Kosa langu limetiwa muhuri mfukoni, Nawe waufunga uovu wangu.
Deutéronome 32.34 Osée 13.12 Job 21.19
18 Lakini, tazama, mlima ukianguka hutoweka, Nalo jabali huondolewa mahali pake;
Job 18.4 Jérémie 4.24 Esaïe 64.1 Matthieu 27.51 Apocalypse 8.8
19 Maji mengi huyapunguza mawe; Mafuriko yake huuchukua mchanga wa nchi; Nawe matumaini ya wanadamu wayaangamiza.
Ezéchiel 37.11 Psaumes 30.6-30.7 Luc 12.19-12.20 Genèse 6.17 Job 19.10
20 Wewe wamshinda nguvu sikuzote, naye hupita aende zake Wabadili sura zake, na kumpeleka aondoke.
Job 14.14 Ecclésiaste 8.8 Lamentations 4.8 Job 2.12
21 Wanawe hufikilia heshima, wala yeye hajui; Kisha wao huaibishwa, lakini yeye hana habari zao.
Ecclésiaste 9.5 Esaïe 63.16 Psaumes 39.6 Esaïe 39.7-39.8 Ecclésiaste 2.18-2.19
22 Lakini mwili ulio juu yake una maumivu, Na nafsi yake ndani huomboleza.
Job 19.26 Job 19.20 Luc 16.23-16.24 Proverbes 14.32 Job 33.19-33.21

Cette Bible est dans le domaine public.