Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 14.2
Bible en Swahili de l’est


1 Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke Siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu.
Job 5.7 Job 25.4 Ecclésiaste 2.23 Job 15.14 Genèse 47.9
2 Yeye huchanua kama vile ua, kisha hukatwa; Hukimbia kama kivuli, wala hakai kamwe.
Job 8.9 1 Pierre 1.24 Esaïe 40.6-40.8 Psaumes 103.15-103.16 1 Chroniques 29.15
3 Nawe, je! Wafumbua macho yako kumwangalia mtu kama yeye, Na kunitia katika hukumu pamoja nawe?
Psaumes 144.3 Psaumes 143.2 Psaumes 8.4 Job 7.17-7.18 Job 9.19-9.20
4 Ni nani awezaye kutoa kitu kilicho safi kitoke katika kitu kichafu? Hapana awezaye.
Jean 3.6 Psaumes 51.5 Job 15.14 Ephésiens 2.3 Romains 5.12
5 Kwa kuwa siku zake zimeamriwa, hesabu ya miezi yake unayo wewe, Nawe umemwekea mipaka yake asiyoweza kuipita;
Psaumes 39.4 Job 21.21 Actes 17.26 Job 14.14 Apocalypse 1.18
6 Acha kumwangalia yeye, apate kupumzika, Hata atakapoitimiza siku yake, kama aliyeajiriwa.
Job 7.19 Job 7.1-7.2 Psaumes 39.13 Job 7.16 Job 10.20
7 Kwani yako matumaini ya mti, ya kuwa ukikatwa utachipuka tena, Wala machipukizi yake hayatakoma.
Esaïe 27.6 Job 19.10 Esaïe 11.1 Daniel 4.15 Job 14.14
8 Ijapokuwa mizizi yake huchakaa mchangani, Na shina lake kufa katika udongo;
Esaïe 26.19 1 Corinthiens 15.36 Jean 12.24
9 Lakini kwa harufu ya maji utachipuka, Na kutoa matawi kama mche.
Ezéchiel 19.10 Ezéchiel 17.3-17.10 Romains 11.17-11.24 Ezéchiel 17.22-17.24
10 Lakini mwanadamu hufa, huifariki dunia; Naam, mwanadamu hutoa roho, naye yupo wapi?
Job 7.7-7.10 Job 14.12 Actes 5.10 Matthieu 27.50 Genèse 49.33
11 Kama vile maji kupwa katika bahari, Na mto kupunguka na kukatika;
Esaïe 19.5 Job 6.15-6.18 Jérémie 15.18
12 Ni vivyo mwanadamu hulala chini, asiinuke; Hata wakati wa mbingu kutokuwako tena, hawataamka, Wala kuamshwa usingizini.
Apocalypse 20.11 Job 10.21-10.22 Apocalypse 21.1 Actes 3.21 Job 3.13
13 Laiti ungenificha kuzimuni, Ukanilinda kwa siri, hata ghadhabu zako zitakapopita, Na kuniandikia muda ulioamriwa, na kunikumbuka!
Esaïe 26.20-26.21 Esaïe 57.1-57.2 Psaumes 106.4 Job 3.17-3.19 Genèse 8.1
14 Mtu akifa, je! Atakuwa hai tena? Mimi ningengoja siku zote za vita vyangu, Hata kufunguliwa kwangu kunifikilie.
Job 7.1 Job 13.15 Psaumes 27.14 Ezéchiel 37.1-37.14 1 Corinthiens 15.42-15.44
15 Wewe ungeita, nami ningekujibu; Ungekuwa na tamaa ya kazi ya mikono yako.
Job 10.3 Job 13.22 1 Pierre 4.19 1 Jean 2.28 Job 7.21
16 Lakini sasa wazihesabu hatua zangu; Je! Huchungulii dhambi yangu?
Job 10.6 Job 31.4 Job 34.21 Proverbes 5.21 Jérémie 32.19
17 Kosa langu limetiwa muhuri mfukoni, Nawe waufunga uovu wangu.
Deutéronome 32.34 Osée 13.12 Job 21.19
18 Lakini, tazama, mlima ukianguka hutoweka, Nalo jabali huondolewa mahali pake;
Job 18.4 Jérémie 4.24 Esaïe 41.15-41.16 Apocalypse 6.14 Esaïe 54.10
19 Maji mengi huyapunguza mawe; Mafuriko yake huuchukua mchanga wa nchi; Nawe matumaini ya wanadamu wayaangamiza.
Job 27.8 Genèse 7.21-7.23 Ezéchiel 37.11 Psaumes 30.6-30.7 Luc 12.19-12.20
20 Wewe wamshinda nguvu sikuzote, naye hupita aende zake Wabadili sura zake, na kumpeleka aondoke.
Job 2.12 Job 14.14 Ecclésiaste 8.8 Lamentations 4.8
21 Wanawe hufikilia heshima, wala yeye hajui; Kisha wao huaibishwa, lakini yeye hana habari zao.
Ecclésiaste 9.5 Esaïe 63.16 1 Samuel 4.20 Psaumes 39.6 Esaïe 39.7-39.8
22 Lakini mwili ulio juu yake una maumivu, Na nafsi yake ndani huomboleza.
Job 19.22 Job 19.26 Job 19.20 Luc 16.23-16.24 Proverbes 14.32

Cette Bible est dans le domaine public.