Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Néhémie 12.18
Bible en Swahili de l’est


Recensement des prêtres et des Lévites

1 Basi, hawa ndio makuhani na Walawi waliopanda na Zerubabeli, mwana wa Shealueli, na Yoshua; Seraya, Yeremia, Ezra;
Néhémie 10.2-10.8 Esdras 2.1-2.2 Néhémie 12.12-12.21 Aggée 1.1 Esdras 5.2
2 Amaria, Maluki, Hatushi;
3 Shekania, Harimu, Meremothi;
4 Ido, Ginethoni, Abia;
Luc 1.5
5 Miyamini, Maazia, Bilgai;
6 Shemaya, Yoyaribu, Yedaya;
1 Chroniques 9.10 Néhémie 11.10
7 Salu, Amoki, Hilkia, Yedaya. Hawa walikuwa wakuu wa makuhani na ndugu zao siku za Yoshua.
Néhémie 12.1 Zacharie 3.1 Aggée 1.1 1 Chroniques 24.18 Esdras 3.2
8 Tena Walawi; Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na Matania, aliyekuwa juu ya shukrani, yeye na ndugu zake.
Néhémie 11.17 Néhémie 12.24 Néhémie 11.22 Néhémie 9.4 Néhémie 10.9-10.13
9 Tena Bakbukia na Uno, ndugu zao, kuwaelekea kwa zamu.
Néhémie 12.24 Psaumes 134.1-134.3
10 Naye Yoshua akamzaa Yoyakimu, Yoyakimu akamzaa Eliashibu, Eliashibu akamzaa Yoyada,
Néhémie 13.28 Néhémie 13.4 Néhémie 3.1 Néhémie 13.7 1 Chroniques 6.3-6.15
11 Yoyada akamzaa Yohana, Yohana akamzaa Yadua.
12 Na siku za Yoyakimu wakawako makuhani, wakuu wa mbari za mababa; wa Seraya, Meraya; wa Yeremia, Hanania;
1 Chroniques 24.6-24.31 1 Chroniques 15.12 1 Chroniques 9.33-9.34 Néhémie 12.22
13 wa Ezra, Meshulamu; wa Amaria, Yehohanani;
14 wa Maluki, Yonathani; wa Shekania, Yusufu;
15 wa Harimu, Adna; wa Meremothi, Helkai;
16 wa Ido, Zekaria; wa Ginethoni, Meshulamu;
17 wa Abia, Zikri; wa Miyamini; wa Maazia, Piltai;
18 wa Bilgai, Shamua; wa Shemaya, Yehonathani;
19 wa Yoyaribu, Matenai; wa Yedaya, Uzi;
20 wa Salu, Kalai; wa Amoki, Eberi;
21 wa Hilkia, Hashabia; wa Yedaya, Nethaneli.
22 Walawi siku za Eliashibu, na Yoyada, na Yohana, na Yadua, wameandikwa wakuu wa mbari za mababa; tena na makuhani; hata siku za kumiliki kwake Dario, Mwajemi.
Néhémie 12.10-12.13
23 Wana wa Lawi, wakuu wa mbari za mababa, wameandikwa katika kitabu cha tarehe, hata siku za Yohana mwana wa Eliashibu.
1 Chroniques 9.14-9.44
24 Nao wakuu wa Walawi; Hashabia, Sherebia, Yeshua, Binui, Kadmieli, na ndugu zao kuwaelekea, ili kusifu na kushukuru, kama amri ya Daudi, mtu wa Mungu, zamu kwa zamu.
1 Chroniques 25.1-25.26 Esdras 2.40 Josué 14.6 Néhémie 8.7 Néhémie 12.8-12.9
25 Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni, na Akubu, walikuwa mabawabu, wa kulinda nyumba za hazina penye malango.
Néhémie 12.8-12.9 Esaïe 21.8 1 Chroniques 23.32 1 Chroniques 26.15 1 Chroniques 26.12
26 Hao walikuwapo siku za Yoyakimu, mwana ya Yoshua, mwana wa Yosadaki, na siku za Nehemia, liwali, na Ezra, kuhani, mwandishi.
Néhémie 8.9 Esdras 7.6 Esdras 7.11

Dédicace de la muraille de Jérusalem

27 Basi, walipouweka wakfu ukuta wa Yerusalemu wakawatafuta Walawi katika mahali pao pote, ili kuwaleta Yerusalemu, wapate kufanya wakfu pamoja na furaha, na kwa shukrani, na kwa kuimba, kwa matoazi, vinanda na vinubi.
1 Chroniques 15.16 2 Chroniques 5.13 2 Chroniques 29.30 1 Chroniques 15.28 Deutéronome 20.5
28 Waimbaji wakakusanyika kutoka uwanda na viunga vya Yerusalemu, na kutoka vijiji vya Wanetofathi;
1 Chroniques 9.16 1 Chroniques 2.54 Néhémie 6.2
29 tena toka Beth-gilgali, na toka mashamba ya Geba na Azmawethi; kwa maana waimbaji hao walikuwa wamejijengea vijiji katika viunga vya Yerusalemu.
Josué 5.9 Josué 10.43 Deutéronome 11.30 Josué 21.17 Esdras 2.24
30 Makuhani na Walawi wakajitakasa, nao wakawatakasa watu, na malango, na ukuta.
Job 1.5 Exode 19.10 Esdras 6.21 Exode 19.15 2 Chroniques 29.5
31 Ndipo nikawapandisha wakuu wa Yuda juu ya ukuta, nikawaagiza mikutano mikubwa miwili ya hao walioshukuru, na kuandamana; mmoja uende kwa kuume ukutani kuliendea lango la jaa;
Néhémie 2.13 Néhémie 12.38 2 Chroniques 5.2 1 Chroniques 28.1 1 Chroniques 13.1
32 na baada yao wakaenda Hoshaya, na nusu ya wakuu wa Yuda,
33 na Azaria, na Ezra, na Meshulamu,
Néhémie 10.2-10.7
34 na Yuda, na Benyamini, na Shemaya, na Yeremia,
35 na baadhi ya makuhani wenye baragumu; Zekaria, mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu;
2 Chroniques 13.12 Nombres 10.2-10.10 1 Chroniques 26.10-26.11 Néhémie 11.17 1 Chroniques 25.2
36 na ndugu zake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda, na Hanani, wenye vinanda vya Daudi mtu wa Mungu; Ezra, mwandishi, akawatangulia;
Néhémie 12.24 1 Chroniques 23.5 2 Chroniques 8.14 Amos 6.5 Esdras 7.1
37 na kwa lango la chemchemi, wakienda moja kwa moja mbele yao, wakapanda madaraja ya mji wa Daudi, uinukapo ukuta, juu ya nyumba ya Daudi, mpaka lango la maji upande wa mashariki.
Néhémie 2.14 Néhémie 3.26 Néhémie 8.16 Néhémie 8.1 Néhémie 8.3
38 Na mkutano wa pili wao wenye kushukuru wakaenda kuwalaki, na mimi nikafuata nyuma yao, pamoja na nusu ya watu, ukutani juu ya mnara wa tanuu, mpaka ule ukuta mpana;
Néhémie 3.8 Néhémie 3.11 Néhémie 12.31
39 na juu ya lango la Efraimu, na kupita lango la kale, na lango la samaki, na mnara wa Hananeli, na mnara wa Hamea, mpaka lango la kondoo; nao wakasimama hapo langoni pa gereza.
Néhémie 3.1 Néhémie 3.6 Néhémie 3.3 Néhémie 8.16 Néhémie 3.25
40 Ndivyo walivyosimama mikutano miwili yao walioshukuru nyumbani mwa Mungu, na mimi, na nusu ya mashehe pamoja nami;
Psaumes 42.4 Psaumes 134.1-134.3 Psaumes 47.6-47.9 Néhémie 12.31-12.32
41 na makuhani, Eliakimu, Maaseya, Miyamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania, wenye baragumu;
42 na Maaseya, na Shemaya, na Eleazari, na Uzi, na Yehohanani, na Malkiya, na Elamu, na Ezeri. Waimbaji wakaimba kwa sauti kuu, wenye Yezrahia kuwa msimamizi wao.
Psaumes 98.4-98.9 Psaumes 81.1 Néhémie 11.14 Psaumes 100.1-100.2 Psaumes 95.1
43 Wakatoa dhabihu nyingi siku ile, wakafurahi; kwa kuwa Mungu amewafurahisha furaha kuu; na wanawake pia na watoto wakafurahi; hata ikasikiwa mbali sana furaha hiyo ya Yerusalemu.
Psaumes 92.4 2 Chroniques 29.35-29.36 Psaumes 30.11-30.12 Ephésiens 5.19 Exode 15.20-15.21

Revenus des serviteurs du temple

44 Na siku hiyo watu wakaagizwa juu ya vyumba vya hazina, kwa sadaka za kuinuliwa, na kwa malimbuko, na kwa zaka, ili kuzikusanya, kwa kadiri ya mashamba ya miji, sehemu zilizoamriwa katika torati za makuhani, na Walawi; kwa maana Yuda waliwafurahia makuhani na Walawi waliotumika.
Néhémie 13.12-13.13 1 Chroniques 23.28 2 Chroniques 31.11-31.13 Néhémie 10.37-10.39 Nombres 3.10
45 Wakauangalia ulinzi wa Mungu wao, na ulinzi wa kutakasika, na hao waimbaji na mabawabu vile vile, sawasawa na amri ya Daudi, na ya Sulemani mwanawe.
1 Chroniques 25.1-25.26 2 Chroniques 23.6 1 Chroniques 23.28
46 Kwa kuwa siku za Daudi zamani, Asafu alikuwa mkuu wa waimbaji, na juu ya nyimbo za sifa na shukrani kwa Mungu.
2 Chroniques 29.30 Psaumes 73.1 1 Chroniques 25.1-25.31 Psaumes 83.1
47 Na Israeli wote, siku za Zerubabeli, na siku za Nehemia, walitoa sehemu za waimbaji na mabawabu, kama ilivyohusika kila siku; nao wakawatakasia Walawi; na Walawi wakawatakasia wana wa Haruni.
Malachie 3.8-3.10 Néhémie 12.26 Néhémie 12.12 Galates 6.6 Néhémie 13.10-13.12

Cette Bible est dans le domaine public.