Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 14.5
Bible en Swahili de l’est


Règne d’Asa

1 Basi Abiya akalala na baba zake, wakamzika mjini mwa Daudi, akatawala Asa mwanawe mahali pake; katika siku zake nchi ikastarehe miaka kumi.
1 Rois 14.31 1 Chroniques 3.10 1 Rois 2.10 2 Chroniques 9.31 1 Rois 15.8-15.24
2 Basi, Asa akafanya yaliyo mema, yaliyo ya adili, machoni pa Bwana, Mungu wake;
1 Rois 15.11 2 Chroniques 31.20 Luc 1.75 1 Rois 15.14
3 maana aliziondoa madhabahu za kigeni, na mahali pa juu, akazivunja nguzo, akayakata-kata maashera;
Deutéronome 7.5 Exode 34.13 1 Rois 15.12-15.14 2 Rois 23.14 2 Chroniques 15.17
4 akawaamuru Yuda wamtafute Bwana, Mungu wa baba zao, na kuzitenda torati na amri.
Genèse 18.19 2 Chroniques 11.16 1 Samuel 3.13 2 Chroniques 34.32-34.33 Amos 5.4
5 Tena akaondoa kutoka miji yote ya Yuda mahali pa juu na sanamu za jua; ufalme ukastarehe mbele yake.
2 Chroniques 34.4 2 Chroniques 34.7
6 Akajenga miji yenye maboma katika Yuda; kwa kuwa nchi ilikuwa imestarehe, wala hakuwa na vita miaka ile; kwa sababu Bwana amemstarehesha.
2 Chroniques 15.15 Job 34.29 1 Chroniques 22.9 Josué 23.1 1 Rois 5.4
7 Naye akawaambia Yuda, Na tuijenge miji hii, na kuizungushia maboma, na minara, na malango, na makomeo; nchi bado ikalipo mbele yetu, kwa kuwa tumemtafuta Bwana, Mungu wetu; naam, tumemtafuta, naye amemstarehesha pande zote. Basi wakajenga, wakafanikiwa.
2 Chroniques 14.6 Actes 9.31 Jérémie 29.12-29.14 2 Chroniques 14.4 2 Chroniques 8.5
8 Naye Asa alikuwa na jeshi waliochukua ngao na mikuki, katika Yuda mia tatu elfu; na katika Benyamini wenye kuchukua vigao na kupinda upinde, mia mbili na themanini elfu; hao wote walikuwa mashujaa.
2 Chroniques 13.3 2 Chroniques 11.1 2 Chroniques 25.5 2 Chroniques 17.14-17.19
9 Kisha, akatoka juu yao Zera Mkushi, mwenye jeshi elfu elfu, na magari mia tatu; akaja Maresha.
2 Chroniques 16.8 2 Chroniques 12.2-12.3 Josué 15.44 2 Chroniques 11.8 Apocalypse 16.14
10 Akatoka Asa amlaki, wakapanga vita Maresha bondeni mwa Sefatha.
Josué 19.4 Juges 1.17
11 Naye Asa akamlilia Bwana, Mungu wake, akasema, Bwana, hapana kuliko wewe aliye wa kusaidia, kati yake yeye aliye hodari, na yeye asiye na nguvu; utusaidie, Ee Bwana, Mungu wetu; kwa kuwa sisi twakutegemea wewe, na kwa jina lako tumekuja juu ya jamii kubwa hii. Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, asikushinde mwanadamu.
2 Corinthiens 12.9-12.10 2 Chroniques 13.18 2 Chroniques 13.14 Romains 8.31 1 Chroniques 5.20
12 Basi, Bwana akawapiga Wakushi mbele ya Asa, na mbele ya Yuda; na Wakushi wakakimbia.
2 Chroniques 13.15 Psaumes 60.12 Deutéronome 32.39 1 Corinthiens 9.26 Josué 10.10
13 Asa na watu waliokuwa pamoja naye wakawafuata mpaka Gerari; nao wengi wakaanguka wa Wakushi hata wasiweze kupona; kwa sababu waliangamizwa mbele za Bwana, na mbele ya jeshi lake; na hao wakachukua mateka mengi sana.
Genèse 10.19 Genèse 20.1 Genèse 26.1 2 Chroniques 14.14 Job 9.4
14 Wakaipiga miji yote kando-kando ya Gerari; maana hofu ya Bwana ikawajia; nao wakaiteka nyara miji yote, kwa maana zilikuwamo ndani yake nyara nyingi mno.
2 Chroniques 17.10 Genèse 35.5 2 Chroniques 20.29 Job 15.21 Psaumes 48.5-48.6
15 Wakazipiga pia hema za ng’ombe, wakachukua kondoo wengi na ngamia, wakarudi Yerusalemu.
Nombres 31.9 1 Chroniques 4.41 1 Samuel 30.20 1 Chroniques 5.21 Nombres 31.30-31.47

Cette Bible est dans le domaine public.