Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 11.20
Bible en Swahili de l’est


Règne de Roboam

1 Hata Rehoboamu alipofika Yerusalemu, akakusanya nyumba ya Yuda na Benyamini, watu wateule mia na themanini elfu waliokuwa hodari, watu wa vita, ili wapigane juu ya Israeli, ili wamrudishie Rehoboamu huo ufalme.
Psaumes 33.16 Proverbes 21.30-21.31 1 Rois 12.21-12.24 Psaumes 33.10
2 Lakini neno la Bwana likamjia Shemaya mtu wa Mungu, kusema,
2 Chroniques 12.15 1 Rois 12.22-12.24 Deutéronome 33.1 1 Timothée 6.11 2 Chroniques 8.14
3 Mwambie Rehoboamu mwana wa Sulemani, mfalme wa Yuda, uwaambie na Israeli wote waliomo Yuda na Benyamini, ukisema,
2 Rois 17.34 Genèse 49.28 Exode 24.4 Apocalypse 7.4-7.8 Philippiens 3.5
4 Bwana asema hivi, Hamtapanda wala kupigana na ndugu zenu; rudini kila mtu nyumbani kwake; kwa kuwa jambo hili limetoka kwangu. Basi, wakayasikiliza maneno ya Bwana, wakarudi katika kumwendea Yeroboamu.
1 Rois 11.29-11.38 Genèse 50.20 2 Chroniques 25.7-25.10 2 Chroniques 10.15-10.16 2 Chroniques 28.8-28.15
5 Naye Rehoboamu akakaa Yerusalemu, akajenga miji yenye ngome katika Yuda.
2 Chroniques 8.2-8.6 2 Chroniques 26.6 2 Chroniques 14.6-14.7 2 Chroniques 16.6 2 Chroniques 17.12
6 Akajenga na Bethlehemu, na Etamu, na Tekoa,
Amos 1.1 Néhémie 3.5 2 Chroniques 20.20 Juges 15.8 Matthieu 2.5-2.6
7 na Bethsuri, na Soko, na Adulamu,
Josué 15.35 Josué 12.15 1 Samuel 22.1 Michée 1.15 2 Samuel 23.13
8 na Gathi, na Maresha, na Zifu,
Psaumes 54.1 1 Samuel 23.19 Josué 15.44 Josué 15.24 1 Samuel 23.14
9 na Adoraimu, na Lakishi, na Azeka,
Josué 15.39 Josué 10.11 Josué 15.35 2 Chroniques 32.9 Josué 10.5
10 na Sora, na Aiyaloni, na Hebroni, iliyoko katika Yuda na Benyamini, miji yenye maboma.
Nombres 13.22 Josué 15.33 Josué 19.41-19.42 2 Samuel 2.11 Josué 14.14
11 Akazifanya imara hizo ngome, akaweka majemadari humo, na akiba ya vyakula, na mafuta, na mvinyo.
2 Chroniques 11.23 2 Chroniques 17.19 Esaïe 22.10-22.11
12 Na ndani ya miji yote mmoja mmoja aliweka ngao na mikuki, akaifanya kuwa na nguvu nyingi mno. Yuda na Benyamini ikawa milki yake.
2 Chroniques 26.14-26.15 2 Samuel 13.19 2 Chroniques 32.5 2 Samuel 13.22
13 Wakamwendea makuhani na Walawi waliokuwa katika Israeli yote, kutoka mpaka wao wote.
14 Kwani Walawi wakaacha malisho yao, na milki yao, wakaja Yuda na Yerusalemu; kwa sababu Yeroboamu na wanawe waliwatupa, ili wasimfanyie Bwana ukuhani;
2 Chroniques 13.9 Nombres 35.2-35.5 1 Rois 12.28-12.33 1 Rois 13.33 Lévitique 27.30-27.34
15 naye akajiwekea makuhani wa mahali pa juu, na wa wale majini, na wa zile ndama alizozifanya.
1 Rois 12.28 1 Rois 12.31 1 Rois 13.33 Psaumes 106.19-106.20 1 Rois 14.9
16 Na kutoka katika kabila zote za Israeli, wakaandamwa na hao waliojikaza nia kumtafuta Bwana, Mungu wa Israeli, wakaja Yerusalemu, ili wamtolee dhabihu Bwana, Mungu wa baba zao.
2 Chroniques 15.9 Deutéronome 12.5-12.6 Deutéronome 12.11 Job 34.14 Actes 11.23
17 Hivyo wakaufanya imara kwa miaka mitatu ufalme wa Yuda, na kumtia nguvu Rehoboamu mwana wa Sulemani; kwa maana muda wa miaka mitatu wakaiendea njia ya Daudi na Sulemani.
2 Chroniques 12.1 Osée 6.4 2 Chroniques 7.17-7.19 2 Chroniques 1.1-1.12 2 Chroniques 8.13-8.16
18 Rehoboamu akaoa mke, Mahalathi binti Yerimothi mwana wa Daudi, na wa Abihaili binti Eliabu, mwana wa Yese;
1 Samuel 16.6 1 Samuel 17.13 1 Samuel 17.28 1 Chroniques 27.18 1 Chroniques 2.13
19 akamzalia wana, Yeushi, na Shemaria, na Zahamu.
20 Kisha baada yake akamwoa Maaka, binti Absalomu; na yeye akamzalia Abiya, na Atai, na Ziza, na Shelomithi.
2 Chroniques 13.2 Matthieu 1.7 2 Chroniques 12.16 2 Chroniques 11.21 1 Rois 15.1-15.2
21 Rehoboamu akampenda Maaka binti Absalomu kuliko wakeze wote na masuria yake; (maana alioa wake kumi na wanane, na masuria sitini, akazaa wana ishirini na wanane na binti sitini).
Deutéronome 17.17 2 Samuel 3.2-3.5 1 Chroniques 3.1-3.9 1 Rois 11.3 Cantique 6.8-6.9
22 Rehoboamu akamsimamisha Abiya, mwana wa Maaka, kuwa mkuu, mtawala kati ya nduguze, kwa kuwa aliazimia kumtawaza awe mfalme.
Deutéronome 21.15-21.17 1 Chroniques 5.1-5.2 1 Chroniques 29.1
23 Akafanya kwa akili, akawatawanya wanawe wote kati ya nchi zote za Yuda na Benyamini, katika kila mji wenye boma; akawapa vyakula tele. Akawatafutia wake wengi.
Luc 16.8 Genèse 25.6 1 Rois 1.5-1.6 2 Chroniques 21.3 2 Chroniques 10.8-10.15

Cette Bible est dans le domaine public.