Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 1.4
Bible en Swahili de l’est


Jusqu’à la chute du royaume d’Israël

Maladie et mort d’Achazia, le roi d’Israël

1 Ikawa, baada ya kufa kwake Ahabu, Moabu wakawaasi Israeli.
2 Samuel 8.2 2 Rois 8.20 1 Chroniques 18.2 Psaumes 60.8 2 Rois 8.22
2 Na Ahazia akaanguka katika dirisha la chumba chake orofani, katika Samaria, akaugua; akatuma wajumbe, akawaambia, Enendeni mkaulize kwa Baal-zebubu, mungu wa Ekroni, kwamba nitapona ugonjwa huu.
2 Rois 1.16 Marc 3.22 2 Rois 8.7-8.10 Matthieu 10.25 Esaïe 37.12
3 Lakini malaika wa Bwana akamwambia Eliya Mtishbi, Ondoka, uende ukaonane na wale wajumbe wa mfalme wa Samaria, ukawaambie, Je! Ni kwa sababu hapana Mungu katika Israeli, hata mnakwenda kuuliza kwa Baal-zebubu, mungu wa Ekroni?
1 Rois 17.1 2 Rois 1.8 2 Rois 1.2 Jonas 2.8 Actes 8.26
4 Basi sasa, Bwana asema hivi, Hutashuka katika kile kitanda ulichokipanda, bali hakika utakufa. Eliya akaondoka.
2 Rois 1.6 2 Rois 1.16 Nombres 26.65 Proverbes 14.32 1 Samuel 28.19
5 Wale wajumbe wakarudi, na mfalme akawaambia, Mbona mmerudi?
6 Wakamwambia, Mtu alitokea, akaonana nasi, akatuambia, Enendeni, rudini kwa mfalme yule aliyewatuma, mkamwambie, Bwana asema hivi Je! Ni kwa sababu hapana Mungu katika Israeli, hata mnakwenda kuuliza kwa Baal-zebubu, mungu wa Ekroni? Basi kwa ajili ya hayo hutashuka katika kile kitanda ulichokipanda, bali hakika utakufa.
Esaïe 41.22-41.23 Psaumes 16.4 2 Rois 1.2-1.4 1 Chroniques 10.13-10.14
7 Akawaambia, Je! Mtu yule aliyetokea, akaonana nanyi, akawaambia maneno hayo, alikuwa mtu wa namna gani?
Juges 8.18 1 Samuel 28.14
8 Wakamwambia, Alikuwa amevaa vazi la manyoya, tena amejifunga shuka ya ngozi kiunoni mwake. Naye akasema, Ndiye yule Eliya Mtishbi.
Matthieu 3.4 Zacharie 13.4 Marc 1.6 Luc 1.17 Esaïe 20.2
9 Ndipo mfalme akatuma akida wa askari hamsini pamoja na hamsini wake, wamwendee Eliya. Akamwendea, na tazama, ameketi juu ya kilima. Akamwambia, Ewe mtu wa Mungu, mfalme asema, Shuka.
2 Rois 6.13-6.14 Luc 6.11-6.12 Matthieu 27.41-27.43 Amos 7.12 Marc 15.32
10 Eliya akajibu, akamwambia yule akida wa hamsini, Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, na ushuke moto kutoka mbinguni, ukuteketeze wewe na hamsini wako. Moto ukashuka, ukamteketeza, yeye na hamsini wake.
Luc 9.54 Job 1.16 Apocalypse 11.5 1 Rois 18.36-18.38 Hébreux 12.29
11 Akatuma tena akida wa hamsini mwingine pamoja na hamsini wake, wamwendee. Akajibu, akamwambia, Ewe mtu wa Mungu, mfalme asema, Shuka upesi.
Jérémie 5.3 1 Samuel 6.9 Luc 22.63-22.64 1 Samuel 22.17-22.19 Proverbes 29.12
12 Eliya akajibu, akamwambia, Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, na ushuke moto kutoka mbinguni, ukuteketeze wewe na hamsini wako. Moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza, yeye na hamsini wake.
2 Rois 1.9-1.10
13 Tena akatuma akida wa hamsini wa tatu, pamoja na hamsini wake. Yule akida wa hamsini wa tatu akapanda, akaenda akapiga magoti mbele ya Eliya, akamsihi sana, akamwambia, Ee mtu wa Mungu, nakusihi, roho yangu, na roho za watumishi wako hawa hamsini, ziwe na thamani machoni pako.
Esaïe 1.5 Psaumes 102.17 Jacques 4.7 Exode 11.8 1 Samuel 26.21
14 Tazama, moto ulishuka kutoka mbinguni, ukawateketeza wale akida wa hamsini wawili wa kwanza pamoja na hamsini wao; laiti sasa roho yangu na iwe na thamani machoni pako.
Proverbes 6.26 Psaumes 116.15 Actes 20.24 2 Rois 1.10-1.11 Psaumes 72.14
15 Malaika wa Bwana akamwambia Eliya, Shuka pamoja naye; usimwogope. Akaondoka, akashuka pamoja naye hata kwa mfalme.
Esaïe 51.12 Jérémie 1.17 Ezéchiel 2.6 2 Rois 1.3 Jérémie 15.20
16 Akamwambia, Bwana asema hivi, Kwa kuwa umetuma wajumbe waulize kwa Baal-zebubu, mungu wa Ekroni, je! Ni kwa sababu hapana Mungu katika Israeli, uulize neno lake? Kwa hiyo hutashuka katika kile kitanda ulichokipanda, bali hakika utakufa.
Exode 4.22-4.23 1 Rois 21.18-21.24 Psaumes 132.3 2 Rois 5.21 2 Rois 1.2-1.4
17 Basi akafa, sawasawa na neno la Bwana alilolinena Eliya. Na Yoramu alianza kutawala mahali pake katika mwaka wa pili wa Yehoramu mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda; kwa kuwa yeye hakuwa na mwana.
2 Rois 3.1 2 Rois 8.16-8.17 1 Rois 22.51
18 Na mambo yote yaliyosalia aliyoyafanya Ahazia, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli?
1 Rois 14.19 1 Rois 22.39

Cette Bible est dans le domaine public.