Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 19.15
Bible en Swahili de l’est


Fuite d’Élie

1 Basi, Ahabu akamwambia Yezebeli habari ya mambo yote aliyoyafanya Eliya, na jinsi alivyowaua manabii wote kwa upanga.
1 Rois 18.40 1 Rois 21.25 1 Rois 21.5-21.7 1 Rois 16.31
2 Ndipo Yezebeli akampelekea Eliya mjumbe, kusema, Miungu wanifanyie hivyo na kuzidi, nisipokufanya roho yako kesho, panapo wakati huu, kama roho ya mmojawapo wa hao.
1 Rois 20.10 Ruth 1.17 2 Rois 6.31 2 Rois 19.27-19.28 2 Rois 19.22
3 Naye alipoona hayo, aliondoka, akaenda aihifadhi roho yake, akafika Beer-sheba, mji wa Yuda, akamwacha mtumishi wake huko.
Genèse 21.31 2 Corinthiens 12.7 Matthieu 26.70-26.74 Genèse 12.12-12.13 Exode 2.15
4 Lakini yeye mwenyewe akaendelea katika jangwa mwendo wa siku moja, akaenda akaketi chini ya mretemu. Akajiombea roho yake afe, akasema, Yatosha; sasa, Ee Bwana, uiondoe roho yangu; kwa kuwa mimi si mwema kuliko baba zangu.
Nombres 11.15 Jonas 4.8 Jonas 4.3 1 Rois 19.3 Jérémie 20.14-20.18
5 Naye akajinyosha akalala chini ya mretemu; na tazama, malaika akamgusa, akamwambia, Inuka, ule.
Hébreux 1.14 Daniel 9.21 Hébreux 13.5 Actes 12.7 Daniel 10.9-10.10
6 Akatazama, kumbe! Pana mkate umeokwa juu ya makaa, na gudulia la maji, kichwani pake. Akala, akanywa, akajinyosha tena.
1 Rois 17.6 Matthieu 4.11 Esaïe 33.16 Jean 21.5 1 Rois 17.9-17.15
7 Malaika wa Bwana akamwendea mara ya pili, akamgusa, akasema, Inuka, ule; maana safari hii ni kubwa mno kwako.
Deutéronome 33.25 Psaumes 103.13-103.14
8 Akainuka, akala, akanywa, akaenda katika nguvu za chakula hicho siku arobaini mchana na usiku hata akafika Horebu, mlima wa Mungu.
Exode 34.28 Exode 3.1 Deutéronome 9.18 Matthieu 4.2 Exode 24.18
9 Akafika kunako pango, akalala ndani yake. Na tazama, neno la Bwana likamjia, naye akamwambia, Unafanya nini hapa, Eliya?
Exode 33.21-33.22 1 Rois 19.13 Jérémie 9.2 Jérémie 2.18 Jonas 1.3-1.4
10 Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu, waiondoe.
1 Rois 18.4 1 Rois 18.22 Nombres 25.13 Exode 34.14 Exode 20.5
11 Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za Bwana. Na tazama, Bwana akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunja-vunja miamba mbele za Bwana; lakini Bwana hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo, tetemeko la nchi; lakini Bwana hakuwamo katika lile tetemeko la nchi;
Ezéchiel 1.4 Exode 24.12 Ezéchiel 37.7 Exode 19.20 Exode 34.2
12 na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini Bwana hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu.
Job 4.16 Zacharie 4.6 Deutéronome 4.33 2 Rois 1.10 Actes 2.36-2.37
13 Ikawa, Eliya alipoisikia, alijifunika uso wake katika mavazi yake, akatoka, akasimama mlangoni mwa pango. Na tazama, sauti ikamjia, kusema, Unafanya nini hapa, Eliya?
1 Rois 19.9 Jean 21.15-21.17 Esaïe 6.2 Exode 33.23 1 Rois 18.42
14 Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana, Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu waiondoe.
Jérémie 22.9 Deutéronome 31.20 Deutéronome 29.25 Osée 6.7 Esaïe 62.6-62.7
15 Bwana akamwambia, Enenda, urudi njia ya jangwa la Dameski; ukifika, mtie mafuta Hazaeli awe mfalme wa Shamu.
2 Rois 8.7-8.15 2 Rois 9.14 Esaïe 45.1 Genèse 14.15 Actes 9.2-9.3
16 Na Yehu mwana wa Nimshi mtie mafuta awe mfalme wa Israeli; na Elisha mwana wa Shafati wa Abel-Mehola mtie mafuta awe nabii mahali pako.
1 Rois 19.19-19.21 2 Rois 2.15 2 Rois 2.9 Luc 4.27 2 Rois 9.1-9.14
17 Na itakuwa atakayeokoka na upanga wa Hazaeli, Yehu atamwua; na atakayeokoka na upanga wa Yehu, Elisha atamwua.
2 Rois 13.22 2 Rois 8.12 2 Rois 13.3 2 Rois 10.32 Osée 6.5
18 Pamoja na hayo nitajisazia katika Israeli watu elfu saba, kila goti lisilomwinamia Baali, na kila kinywa kisichombusu.
Osée 13.2 Romains 11.4-11.5 Esaïe 1.9 Esaïe 10.20-10.22 Psaumes 2.12

Appel d’Élisée

19 Basi, akaondoka huko, akamkuta Elisha mwana wa Shafati, aliyekuwa akilima, mwenye jozi za ng’ombe kumi na mbili mbele yake, na yeye mwenyewe alikuwa pamoja na lile la kumi na mbili. Eliya akapita karibu naye, akatupa vazi lake juu yake.
2 Rois 2.8 1 Samuel 28.14 2 Rois 2.13-2.14 Psaumes 78.70-78.72 Matthieu 4.18-4.19
20 Naye akawaacha ng’ombe, akamfuata Eliya mbio, akasema, Nipe ruhusa, nakuomba, nimbusu baba yangu na mama yangu, kisha mimi nitakufuata. Akamwambia, Enenda, urudi; ni nini niliyokutendea?
Matthieu 8.21-8.22 Luc 9.61-9.62 Actes 20.37 Matthieu 9.9 Matthieu 19.27
21 Akarudi akiacha kumfuata, akatwaa lile jozi la ng’ombe, akawachinja, akatokosa nyama zao kwa ile miti ya ng’ombe, akawapa watu, wakala. Kisha akainuka, akamfuata Eliya, akamhudumia.
2 Samuel 24.22 2 Timothée 4.11 2 Rois 2.3 Philémon 1.13 Actes 13.5

Cette Bible est dans le domaine public.