Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 14.29
Bible en Swahili de l’est


1 Siku zile akaugua Abiya, mwana wa Yeroboamu.
1 Samuel 31.2 1 Rois 14.12-14.13 1 Rois 13.33-13.34 1 Samuel 4.19-4.20 Exode 20.5
2 Yeroboamu akamwambia mkewe, Ondoka, tafadhali, ujibadilishe, wasikujue kuwa mkewe Yeroboamu; ukaende Shilo; tazama, yuko huko Ahiya nabii, aliyeninena mimi ya kwamba nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.
2 Samuel 14.2 1 Samuel 28.8 2 Chroniques 18.29 1 Rois 22.30 1 Rois 11.29-11.38
3 Twaa mkononi mikate kumi, na kaki, na mtungi wa asali, ukamwendee; naye atakuambia kijana atakuwaje.
1 Samuel 9.7-9.8 1 Rois 13.7 2 Rois 4.42 Luc 7.2-7.3 2 Rois 5.15
4 Akafanya hivi mkewe Yeroboamu, akaondoka, akaenda Shilo, akaja nyumbani kwa Ahiya. Basi Ahiya hakuweza kuona; kwa kuwa macho yake yamepofuka kwa sababu ya uzee wake.
1 Rois 11.29 1 Samuel 3.2 1 Samuel 4.15 Jérémie 7.12-7.14 1 Samuel 4.3-4.4
5 Bwana akamwambia Ahiya, Angalia, mkewe Yeroboamu anakuja akuulize mambo ya mwanawe; kwa maana hawezi; hivi na hivi umwambie; kwani itakuwa akiingia atajifanya kuwa mwanamke mwingine.
Amos 3.7 2 Rois 4.27 Psaumes 139.1-139.4 Proverbes 21.30 Actes 10.19-10.20
6 Ikawa, Ahiya alipoisikia sauti ya miguu yake, akiingia mlangoni, alisema, Karibu, mkewe Yeroboamu; mbona wajifanya kuwa mwingine maana nimetumwa kwako wewe, mwenye maneno mazito.
Ezéchiel 2.4-2.5 1 Rois 22.8 Luc 20.20-20.23 1 Rois 13.20-13.22 Jérémie 21.2-21.7
7 Nenda, umwambie Yeroboamu, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kwa kuwa nilikutukuza miongoni mwa watu, nikakufanya uwe mkuu juu ya watu wangu Israeli,
1 Rois 16.2 2 Samuel 12.7-12.8 1 Rois 12.24 1 Samuel 2.27-2.30 1 Samuel 15.16
8 nikaurarulia mbali ufalme utoke nyumba yake Daudi, na kukupa wewe; walakini wewe hukuwa kama mtumishi wangu Daudi, aliyezishika amri zangu, na kunifuata kwa moyo wake wote, asifanye lo lote ila yaliyo mema machoni pangu;
1 Rois 15.5 Actes 13.22 1 Rois 11.30-11.31 1 Rois 11.33-11.38 Actes 13.36
9 lakini umekosa kuliko wote waliokutangulia, umekwenda kujifanyia miungu mingine, na sanamu zilizoyeyuka, unikasirishe, na kunitupa nyuma yako;
Psaumes 50.17 1 Rois 12.28 Ezéchiel 23.35 2 Chroniques 11.15 Néhémie 9.26
10 tazama, kwa hiyo mimi nitaleta mabaya juu ya nyumba yake Yeroboamu, nami nitamkatia Yeroboamu kila mwanamume, aliyefungwa na aliyeachwa katika Israeli, nami kuondoa nitawaondoa waliobaki wa nyumba yake Yeroboamu, kama mtu aondoavyo mavi, hata itakapokwisha pia.
Deutéronome 32.36 1 Rois 21.21 2 Rois 14.26 2 Rois 9.8-9.9 Psaumes 83.10
11 Yeye afaye wa Yeroboamu mjini mbwa watamla; afaye mashambani ndege wa angani watamla; kwa kuwa Bwana amelinena hilo.
1 Rois 16.4 1 Rois 21.23-21.24 Apocalypse 19.17-19.18 Ezéchiel 39.17-39.19 Esaïe 66.24
12 Basi ondoka, urudi nyumbani kwako; na miguu yako itakapoingia mjini huyo kijana atakufa.
2 Rois 1.6 1 Rois 14.16-14.17 2 Rois 1.16 1 Rois 14.3 Jean 4.50-4.52
13 Na Israeli wote watamlilia, na kumzika, kwa maana ndiye peke yake wa Yeroboamu atakayeingia kaburini; kwa sababu limeonekana ndani yake jambo lililo jema kwa Bwana, Mungu wa Israeli, nyumbani mwa Yeroboamu.
2 Chroniques 19.3 2 Chroniques 12.12 Jérémie 22.10 Job 19.28 Philémon 1.6
14 Tena Bwana atajiinulia mfalme wa Israeli atakayeiharibu nyumba ya Yeroboamu siku ile; na nini tena hata sasa?
1 Rois 15.27-15.29 Ecclésiaste 8.11 Ezéchiel 7.2-7.7 Jacques 5.9 2 Pierre 2.3
15 Kwa kuwa Bwana atawapiga Israeli kama manyasi yatikiswavyo majini; naye atawang’oa Israeli katika nchi hii njema, aliyowapa baba zao, naye atawatawanya ng’ambo ya Mto; kwa sababu wamejifanyia maashera yao, wakimkasirisha Bwana.
Psaumes 52.5 Josué 23.15-23.16 2 Rois 15.29 Proverbes 2.22 Deutéronome 12.3-12.4
16 Naye atawatoa Israeli kwa ajili ya makosa ya Yeroboamu, aliyoyakosa, ambayo kwa hayo amewakosesha Israeli.
1 Rois 15.30 1 Rois 13.34 1 Rois 12.30 1 Rois 15.34 1 Rois 16.2
17 Basi mkewe Yeroboamu akaondoka, akaenda zake, akafika Tirza; naye alipofika kizingitini kwa nyumba, huyo kijana akafa.
1 Rois 15.33 1 Rois 16.23 1 Rois 15.21 1 Rois 16.15 Cantique 6.4
18 Israeli wote wakamzika, wakamlilia; sawasawa na neno la Bwana, alilolinena kwa mkono wa mtumishi wake Ahiya nabii.
1 Rois 14.13
19 Na mambo yake Yeroboamu yaliyosalia, ya kupigana na ya kutawala, tazama, yameandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli.
2 Chroniques 13.2-13.20 1 Chroniques 27.24 1 Rois 16.14 1 Rois 16.27 Esther 6.1
20 Na siku alizotawala Yeroboamu zilikuwa miaka ishirini na miwili; akalala na babaze, naye Nadabu mwanawe akatawala mahali pake.
1 Rois 2.10 Psaumes 4.8 1 Rois 11.43 1 Rois 15.25-15.31 Psaumes 3.5

Règne de Roboam sur Juda

21 Naye Rehoboamu mwana wa Sulemani akatawala katika Yuda. Rehoboamu akaanza kutawala alipokuwa mwenye miaka arobaini na mmoja, akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji aliouchagua Bwana miongoni mwa kabila zote za Israeli, ili aliweke jina lake huko. Na jina la mamaye aliitwa Naama, Mwamoni.
2 Chroniques 12.13 1 Rois 11.36 1 Rois 14.31 Deutéronome 12.21 Psaumes 132.13-132.14
22 Basi Yuda wakafanya maovu machoni pa Bwana; wakamtia wivu, kwa makosa yao waliyoyakosa, kuliko yote waliyoyafanya baba zao.
2 Chroniques 12.1 Psaumes 78.58 1 Corinthiens 10.22 Ezéchiel 16.47-16.48 Jérémie 3.7-3.11
23 Maana hao pia wakajijengea mahali pa juu, na nguzo, na maashera, juu ya kila kilima kirefu, na chini ya kila mti wenye majani mabichi.
Deutéronome 12.2 Esaïe 57.5 2 Rois 17.9-17.10 Ezéchiel 16.24-16.25 1 Rois 3.2
24 Na mahanithi walikuwako katika nchi, wakafanya sawasawa na machukizo yote ya mataifa Bwana aliowafukuza mbele ya wana wa Israeli.
Deutéronome 23.17 2 Rois 23.7 1 Rois 15.12 1 Rois 22.46 Genèse 19.5
25 Ikawa, mwaka wa tano wa mfalme Rehoboamu, akapanda Shishaki, mfalme wa Misri, juu ya Yerusalemu;
1 Rois 11.40 2 Chroniques 12.9 2 Chroniques 12.2-12.4
26 akazichukua hazina za nyumba ya Bwana, na hazina za nyumba ya mfalme; akazichukua zote. Akazichukua pia ngao zote za dhahabu alizozifanya Sulemani.
1 Rois 15.18 2 Chroniques 9.15-9.16 2 Chroniques 12.9-12.11 Psaumes 89.35-89.45 2 Rois 24.13
27 Mfalme Rehoboamu akafanya ngao za shaba mahali pake, akawakabidhi wakuu wa walinzi, waliongoja mlangoni pa nyumba ya mfalme.
1 Samuel 8.11 1 Samuel 22.17 1 Rois 14.1 2 Samuel 15.1 1 Rois 18.46
28 Ikawa kila wakati mfalme alipoingia nyumbani mwa Bwana, hao walinzi walizichukua; wakazirudisha tena katika chumba cha walinzi.
2 Chroniques 12.11
29 Na mambo yake Rehoboamu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda?
1 Rois 15.23 1 Rois 14.19 2 Chroniques 12.15-12.16 1 Rois 22.45 1 Rois 11.41
30 Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu siku zote.
1 Rois 12.24 1 Rois 12.21 1 Rois 15.6-15.7 2 Chroniques 12.15
31 Rehoboamu akalala na babaze, akazikwa pamoja na babaze mjini mwa Daudi. Na jina la mamaye aliitwa Naama, Mwamoni. Na mwanawe, Abiya, alitawala mahali pake.
2 Chroniques 12.16 Matthieu 1.7 1 Chroniques 3.10 1 Rois 15.24 1 Rois 14.20-14.21

Cette Bible est dans le domaine public.