Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 8.2
Bible en Swahili de l’est


La sortie de l’arche

1 Na Mungu akamkumbuka Nuhu, na kila kilicho hai, na wanyama wote waliokuwamo pamoja naye katika safina; Mungu akavumisha upepo juu ya nchi, maji yakapungua;
1 Samuel 1.19 Exode 14.21 Exode 2.24 Genèse 19.29 Genèse 30.22
2 chemchemi za vilindi zikafungwa, pia na madirisha ya mbinguni, mvua kutoka mbinguni ikazuiliwa;
Genèse 7.11 Job 38.37 Matthieu 8.9 Matthieu 8.26-8.27 Jonas 2.3
3 maji yakadumu kuondoka katika nchi; na mwisho wa siku mia na hamsini maji yakapunguka.
Genèse 7.24 Genèse 7.11
4 Mwezi wa saba, siku ya kumi na saba ya mwezi, safina ikatua juu ya milima ya Ararati.
2 Rois 19.37 Jérémie 51.27 Esaïe 37.38 Genèse 7.17-7.19
5 Maji yakapunguka-punguka hata mwezi wa kumi; mwezi huo wa kumi, siku ya kwanza ya mwezi, vilele vya milima vikaonekana.
Genèse 7.11
6 Ikawa baada ya siku arobaini, Nuhu akalifungua dirisha la safina, alilolifanya;
Genèse 6.16 Daniel 6.10
7 akatoa kunguru, naye akatoka akaenda huko na huko, hata maji yakakauka juu ya nchi.
Lévitique 11.15 Job 38.41 Psaumes 147.9 1 Rois 17.4 1 Rois 17.6
8 Kisha akatoa njiwa, aone kwamba maji yamepunguka usoni pa nchi;
Cantique 2.14 Genèse 8.10-8.12 Cantique 2.11-2.12 Cantique 1.15 Matthieu 10.16
9 bali yule njiwa hakuona mahali pa kutua kwa wayo wa mguu wake, akamrudia Nuhu safinani, maana maji yalikuwa juu ya uso wa nchi yote; naye akanyosha mkono, akamtwaa, akamwingiza mle safinani.
Esaïe 60.8 Ezéchiel 7.16 Matthieu 11.28 Psaumes 116.7 Jean 16.33
10 Akangoja na siku saba tena; kisha akamtoa yule njiwa katika safina mara ya pili,
Esaïe 8.17 Esaïe 26.8 Psaumes 40.1 Romains 8.25 Genèse 7.10
11 njiwa akamjia jioni, na tazama, alikuwa na jani bichi la mzeituni kinywani mwake, ambalo amelitunda, basi Nuhu akajua ya kwamba maji yamepunguka juu ya nchi.
Zacharie 4.12-4.14 Néhémie 8.15 Romains 10.15
12 Akangoja na siku saba tena, akamtoa yule njiwa; naye asimrudie tena kamwe.
Esaïe 30.18 Esaïe 8.17 Psaumes 27.14 Habakuk 2.3 Genèse 2.2-2.3
13 Ikawa mwaka wa mia sita na moja, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, maji yalikauka juu ya nchi. Nuhu akaondoa kifuniko cha safina, naye akaona, na tazama, uso wa nchi umekauka.
Genèse 7.11
14 Na mwezi wa pili, siku ya ishirini na saba ya mwezi, nchi ilikuwa kavu.
Genèse 7.13-7.14 Genèse 7.11
15 Mungu akamwambia Nuhu, akisema,
16 Toka katika safina, wewe, na mkeo, na wanao, na wake za wanao pamoja nawe.
Genèse 7.13 Josué 4.10 Daniel 9.25-9.26 Actes 16.37-16.39 Genèse 7.7
17 Utoe pamoja nawe kila kilicho hai kilichomo pamoja nawe, chenye mwili, ndege, na mnyama, na kila kitambaacho, chenye kutambaa juu ya nchi; wajae katika nchi, wawe na uzazi, wakaongezeke katika nchi.
Genèse 1.22 Genèse 9.1 Jérémie 31.27-31.28 Psaumes 144.13-144.14 Genèse 7.14-7.15
18 Basi Nuhu akatoka, yeye, na wanawe, na mkewe, na wake za wanawe pamoja naye;
Psaumes 121.8
19 kila mnyama, na kila kitambaacho, na kila ndege, kila kinachokwenda juu ya nchi kwa kabila zao, wakatoka katika safina.
20 Nuhu akamjengea Bwana madhabahu; akatwaa katika kila mnyama aliye safi, na katika kila ndege aliye safi, akavitoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu.
Lévitique 11.1-11.47 Genèse 12.7-12.8 Genèse 22.9 Genèse 7.2 Genèse 13.4
21 Bwana akasikia harufu ya kumridhisha; Bwana akasema moyoni, Sitailaani nchi tena baada ya hayo kwa sababu ya wanadamu, maana mawazo ya moyo wa mwanadamu ni mabaya tangu ujana wake; wala sitapiga tena baada ya hayo kila kilicho hai kama nilivyofanya.
Jérémie 17.9 Genèse 3.17 Genèse 6.5 Genèse 6.17 Romains 1.21
22 Muda nchi idumupo, majira ya kupanda, na mavuno, wakati wa baridi na wakati wa hari, wakati wa kaskazi na wakati wa kusi, mchana na usiku, havitakoma.
Jérémie 5.24 Jérémie 33.20-33.26 Psaumes 74.16-74.17 Jérémie 31.35 Cantique 2.11-2.12

Cette Bible est dans le domaine public.