Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 48
Bible en Swahili de l’est


Jacob bénit les deux fils de Joseph

1 Ikawa, baada ya mambo hayo, Yusufu akaambiwa, Tazama, baba yako hawezi; akawatwaa wanawe wawili, Manase na Efraimu, pamoja naye.
Jean 11.3 Psaumes 128.6 Job 42.16 Genèse 41.50-41.52 Genèse 50.23
2 Naye akaarifiwa Yakobo ya kwamba, Angalia, mwanao Yusufu anakuja kwako. Israeli akajitia nguvu, akaketi juu ya kitanda.
Deutéronome 3.28 1 Samuel 23.16 Proverbes 23.15 Ephésiens 6.10 Néhémie 2.18
3 Yakobo akamwambia Yusufu, Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu, katika nchi ya Kanaani, akanibariki,
Exode 6.3 Genèse 17.1 Genèse 35.6-35.7 Genèse 28.3 Juges 1.23
4 akaniambia, Mimi hapa, nitakuongezea uzao wako, na kukuzidisha, nami nitakufanya uwe kundi la mataifa; kisha nitawapa wazao wako nchi hii baada yako, iwe milki ya milele.
Genèse 17.8 Genèse 35.11 Genèse 28.3 Genèse 46.3 Genèse 32.12
5 Basi sasa wanao wawili uliozaliwa katika nchi ya Misri kabla sijaja kwako Misri ni watoto wangu, yaani, Efraimu na Manase watakuwa wangu, kama Reubeni na Simeoni.
Josué 14.4 Genèse 46.20 Genèse 41.50-41.52 1 Chroniques 5.1-5.2 Josué 13.7
6 Na wazao wako utakaozaa baada ya hawa watakuwa wako; kwa jina la ndugu zao wataitwa katika urithi wao.
Josué 14.4
7 Na mimi nilipokuja kutoka Padan, Raheli akanifia katika nchi ya Kanaani, njiani, si mwendo mkubwa kabla ya kufika Efrathi. Nikamzika katika njia ya Efrathi, ndio Bethlehemu.
Genèse 35.16-35.19 Genèse 35.9 Ruth 1.2 1 Samuel 17.12 1 Samuel 1.1
8 Israeli akawaona wana wa Yusufu, akasema, Ni nani hawa?
9 Yusufu akamwambia babaye, Hawa ni wanangu, Mungu alionipa hapa. Akasema, Tafadhali uwalete kwangu nami nitawabariki.
Genèse 27.4 Genèse 33.5 Hébreux 11.21 Ruth 4.11-4.14 Psaumes 127.3
10 Na macho ya Israeli yalikuwa mazito kwa uzee, wala hakuweza kuona. Akawaleta kwake, naye akawabusu, na kuwakumbatia.
Genèse 27.1 Genèse 27.27 Esaïe 59.1 Genèse 31.55 Genèse 45.15
11 Israeli akamwambia Yusufu, Sikudhani ya kwamba nitakuona uso wako, na Mungu amenionyesha na uzao wako pia.
Genèse 45.26 Genèse 37.33 Ephésiens 3.20 Genèse 37.35 Genèse 42.36
12 Yusufu akawatoa katika magoti yake, naye akainama kifudifudi
Genèse 42.6 Genèse 23.7 1 Rois 2.19 Genèse 33.3 Lévitique 19.3
13 Yusufu akawaweka wote wawili, Efraimu katika mkono wake wa kuume, kuelekea mkono wa kushoto wa Israeli; na Manase katika mkono wake wa kushoto, kuelekea mkono wa kuume wa Israeli, akawasogeza karibu naye.
14 Israeli akanyosha mkono wake wa kuume akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, aliyekuwa mdogo, na mkono wake wa kushoto akauweka juu ya kichwa cha Manase, huku akijua atiavyo mikono; maana Manase ndiye aliyezaliwa kwanza.
Genèse 41.51 Exode 15.6 Deutéronome 34.9 Genèse 46.20 Psaumes 118.16
15 Akambariki Yusufu, akasema, Mungu ambaye baba zangu, Ibrahimu na Isaka, walienenda mbele zake, yeye Mungu aliyenilisha, maisha yangu yote, hata siku hii ya leo,
Genèse 17.1 Esaïe 33.16 Psaumes 37.3 Genèse 27.4 Psaumes 23.1
16 naye Malaika aliyeniokoa na maovu yote, na awabariki vijana hawa; jina langu na litajwe juu yao, na jina la baba zangu, Ibrahimu na Isaka; na wawe wingi wa watu kati ya nchi.
Esaïe 63.9 Actes 15.17 2 Timothée 4.18 Psaumes 34.22 Amos 9.12
17 Yusufu alipoona kwamba babaye anaweka mkono wake wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, ikawa vibaya machoni pake. Akauinua mkono wa babaye auondoe katika kichwa cha Efraimu, ili auweke juu ya kichwa cha Manase.
Genèse 48.14 Romains 9.11 Romains 9.7-9.8 1 Chroniques 21.7 Nombres 11.1
18 Yusufu akamwambia babaye, Sivyo, babangu, maana huyu ni mzaliwa wa kwanza; weka mkono wako wa kuume kichwani pake.
Actes 10.14 Matthieu 25.9 Genèse 29.26 Actes 11.8 Genèse 49.3
19 Babaye akakataa, akasema, Najua, mwanangu najua, yeye naye atakuwa taifa, yeye naye atakuwa mkuu; lakini ndugu yake mdogo atakuwa mkubwa kuliko yeye, na uzao wake watakuwa wingi wa mataifa.
Deutéronome 33.17 Ezéchiel 27.10 Ruth 4.11-4.12 Nombres 2.19-2.21 Nombres 1.33-1.35
20 Akawabariki siku ile akasema, Katika ninyi Waisraeli watabariki, wakisema, Mungu na akufanye kama Efraimu na Manase. Akamweka Efraimu mbele ya Manase.
Ruth 4.11-4.12 Genèse 24.60 Nombres 7.54 Nombres 7.48 Nombres 10.22-10.23
21 Israeli akamwambia Yusufu, Angalia, mimi ninakufa, lakini Mungu atakuwa pamoja nanyi, naye atawarudisha mpaka nchi ya baba zenu.
Genèse 50.24 Genèse 46.4 Genèse 26.3 Genèse 28.15 2 Timothée 4.6
22 Nami nimekupa wewe sehemu moja zaidi kuliko ndugu zako, niliyoitwaa katika mikono ya Waamori, kwa upanga wangu na upinde wangu.
Josué 24.32 Jean 4.5 Deutéronome 21.17 Genèse 15.16 Josué 17.14-17.18

Cette Bible est dans le domaine public.