Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 28.7
Bible en Swahili de l’est


1 Basi Isaka akamwita Yakobo, akambariki, akamwagiza akamwambia, Usitwae mke wa binti za Kanaani.
Genèse 24.3 Genèse 27.46 Genèse 6.2 Genèse 26.34-26.35 Genèse 28.3-28.4
2 Ondoka, uende Padan-aramu, mpaka nyumba ya Bethueli baba ya mama yako, ukajitwalie huko mke katika binti za Labani, ndugu wa mama yako.
Genèse 25.20 Osée 12.12 Genèse 24.50 Genèse 31.18 Genèse 28.5
3 Na Mungu Mwenyezi, akubariki, akuzidishe, na kukuongeza, ili uwe mkutano wa makabila.
Genèse 35.11 Genèse 48.3 Genèse 43.14 Genèse 9.1 Genèse 24.60
4 Akupe mbaraka wa Ibrahimu, wewe na uzao wako pamoja nawe, upate kuirithi nchi ya kusafiri kwako, Mungu aliyompa Ibrahimu.
Genèse 12.7 Psaumes 39.12 Genèse 13.14-13.17 Psaumes 105.6-105.12 Genèse 22.17-22.18
5 Basi Isaka akampeleka Yakobo, naye akaenda Padan-aramu, kwa Labani, mwana wa Bethueli, Mshami, ndugu wa Rebeka, mama yao Yakobo na Esau.
6 Esau akaona ya kwamba Isaka amembariki Yakobo na kumpeleka Padan-aramu, ili ajitwalie mke huko, na katika kumbariki akamwagiza, akasema, Usitwae mke wa binti za Kanaani,
Genèse 28.1 Genèse 27.33
7 na ya kuwa Yakobo amewatii babaye na mamaye, akaenda Padan-aramu.
Genèse 27.43 Proverbes 1.8 Proverbes 30.17 Ephésiens 6.1 Lévitique 19.3
8 Esau akaona ya kuwa binti za Kanaani hawakumpendeza Isaka, baba yake.
Genèse 24.3 Genèse 26.34-26.35 1 Samuel 8.6 Genèse 28.1
9 Basi Esau akaenda kwa Ishmaeli akamtwaa Mahalathi, binti Ishmaeli mwana wa Ibrahimu, ndugu wa Nebayothi, kuwa mkewe pamoja na wakeze aliokuwa nao.
Genèse 36.3 Genèse 36.13 Genèse 25.13-25.17 Genèse 36.18 Genèse 26.34

Vision d’une échelle

10 Yakobo akatoka Beer-sheba, kwenda Harani.
Actes 7.2 Genèse 11.31 Osée 12.12 Genèse 32.10 Actes 25.13
11 Akafika mahali fulani akakaa huko usiku kucha, maana jua lilikuwa limekuchwa; akatwaa jiwe moja la mahali pale akaliweka chini ya kichwa chake, akalala usingizi pale pale.
Genèse 28.18 Genèse 31.46 2 Corinthiens 1.5 Matthieu 8.20
12 Akaota ndoto; na tazama, ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake.
Jean 1.51 Nombres 12.6 Job 33.15-33.16 Genèse 20.3 Matthieu 1.20
13 Na tazama, Bwana amesimama juu yake, akasema, Mimi ni Bwana, Mungu wa Ibrahimu baba yako, na Mungu wa Isaka; nchi hii uilalayo nitakupa wewe na uzao wako.
Genèse 13.15 Genèse 35.12 Genèse 48.3 Genèse 35.1 Genèse 12.7
14 Na uzao wako utakuwa kama mavumbi ya nchi, nawe utaenea upande wa magharibi, na mashariki, na kaskazini, na kusini; na katika wewe, na katika uzao wako, jamaa zote za dunia watabarikiwa.
Genèse 12.3 Genèse 22.18 Actes 3.25 Genèse 13.14 Genèse 26.4
15 Na tazama, mimi nipo pamoja nawe, nitakulinda kila uendako, nami nitakuleta tena mpaka nchi hii, kwa maana sitakuacha, hata nitakapokufanyia hayo niliyokuambia.
Josué 1.5 Esaïe 41.10 Deutéronome 31.6 Genèse 26.24 Jérémie 1.19
16 Yakobo akaamka katika usingizi wake, akasema, Kweli Bwana yupo mahali hapa, wala mimi sikujua.
Josué 5.15 Exode 3.5 Job 9.11 Exode 15.11 Esaïe 8.13
17 Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, napo ndipo lango la mbinguni.
Exode 3.6 2 Chroniques 5.14 Ecclésiaste 5.1 Juges 13.22 1 Timothée 3.15
18 Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo, na kumimina mafuta juu yake.
Genèse 35.14 Nombres 7.1 Genèse 31.45 Genèse 31.13 2 Samuel 18.18
19 Akaita jina la mahali pale Betheli; lakini jina la mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.
Genèse 48.3 Osée 12.4-12.5 Genèse 12.8 1 Rois 12.29 Genèse 35.1
20 Yakobo akaweka nadhiri akisema, Mungu akiwa pamoja nami, akinilinda katika njia niiendeayo, na kunipa chakula nile, na nguo nivae;
2 Samuel 15.8 Genèse 31.13 1 Timothée 6.8 1 Samuel 1.28 Genèse 28.15
21 nami nikirudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu, ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu.
Deutéronome 26.17 Juges 11.31 2 Samuel 15.8 2 Samuel 19.30 2 Rois 5.17
22 Na jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu; na katika kila utakalonipa hakika nitakutolea wewe sehemu ya kumi.
Genèse 14.20 Genèse 35.7 Lévitique 27.30-27.33 Genèse 33.20 Genèse 12.8

Cette Bible est dans le domaine public.