Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 85.7

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 85

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 84 Chapitre 86

Prière pour le rétablissement d’Israël

1 Bwana, umeiridhia nchi yako, Umewarejeza mateka wa Yakobo.
2 Umeusamehe uovu wa watu wako, Umezisitiri hatia zao zote.
3 Umeiondoa ghadhabu yako yote, Umerudi na kuuacha ukali wa hasira yako.
4 Mungu wa wokovu wetu, uturudishe, Uikomeshe hasira uliyo nayo juu yetu.
5 Je! Utatufanyia hasira hata milele? Utadumisha ghadhabu kizazi hata kizazi?
6 Je! Hutaki kurudi na kutuhuisha, Watu wako wakufurahie?
7 Ee Bwana, utuonyeshe rehema zako, Utupe wokovu wako.
8 Na nisikie atakavyosema Mungu Bwana, Maana atawaambia watu wake amani, Naam, na watauwa wake pia, Bali wasiurudie upumbavu tena.
9 Hakika wokovu wake u karibu na wamchao, Utukufu ukae katika nchi yetu.
10 Fadhili na kweli zimekutana, Haki na amani zimehusiana.
11 Kweli imechipuka katika nchi, Haki imechungulia kutoka mbinguni.
12 Naam, Bwana atatoa kilicho chema, Na nchi yetu itatoa mazao yake.
13 Haki itakwenda mbele zake, Nayo itazifanya hatua zake kuwa njia.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 85.7 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.