Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 18.21
Bible en Swahili de l’est


1 Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe; Hushindana na kila shauri jema.
Proverbes 2.1-2.6 Proverbes 20.3 Jude 1.19 Ephésiens 5.15-5.17 Proverbes 14.10
2 Mpumbavu hapendezwi na ufahamu; Ila moyo wake udhihirike tu.
Proverbes 12.23 Psaumes 1.1-1.2 Proverbes 1.7 Proverbes 17.16 Proverbes 13.16
3 Ajapo asiye haki, huja dharau pia; Na pamoja na aibu huja lawama.
1 Samuel 20.30 Néhémie 4.4 Proverbes 22.10 Proverbes 29.16 Proverbes 11.2
4 Maneno ya kinywa cha mtu ni kama maji ya vilindi; Kijito kibubujikacho; chemchemi ya hekima.
Proverbes 20.5 Proverbes 10.11 Proverbes 13.14 Proverbes 16.22 Psaumes 78.2
5 Kukubali uso wake asiye haki si vizuri; Wala kumpotosha mwenye haki hukumuni.
Proverbes 28.21 Lévitique 19.15 Proverbes 24.23 Psaumes 82.2 Proverbes 17.15
6 Midomo ya mpumbavu huingia katika fitina, Na kinywa chake huita mapigo.
Proverbes 16.27-16.28 Proverbes 19.29 Proverbes 19.19 Proverbes 22.24-22.25 Proverbes 29.9
7 Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake, Na midomo yake ni mtego wa nafsi yake.
Proverbes 12.13 Proverbes 13.3 Proverbes 10.14 Psaumes 64.8 Psaumes 140.9
8 Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo; Nayo hushukia pande za ndani za tumbo.
Proverbes 16.28 Lévitique 19.16 Proverbes 12.18 Psaumes 52.2 Proverbes 26.20-26.22
9 Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake, Ni ndugu yake aliye mharabu.
Proverbes 10.4 Proverbes 28.24 Proverbes 23.20-23.21 Matthieu 25.26 Proverbes 24.30-24.34
10 Jina la Bwana ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.
2 Samuel 22.3 Esaïe 26.4 Psaumes 91.2 Psaumes 144.2 Psaumes 61.3-61.4
11 Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu; Ni kama ukuta mrefu katika mawazo yake.
Proverbes 10.15 Luc 12.19-12.21 Proverbes 11.4 Ecclésiaste 7.12 Job 31.24-31.25
12 Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.
Proverbes 15.33 Proverbes 11.2 Proverbes 16.18 Proverbes 29.23 Ezéchiel 28.2
13 Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake.
Jean 7.51 Deutéronome 13.14 Proverbes 20.25 Esther 3.10-3.15 2 Samuel 16.4
14 Roho ya mtu itastahimili udhaifu wake; Bali roho iliyovunjika nani awezaye kuistahimili?
Proverbes 17.22 Proverbes 15.13 Jacques 1.2 2 Corinthiens 12.9-12.10 Psaumes 147.3
15 Moyo wa mwenye busara hupata maarifa; Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa.
Proverbes 15.14 Psaumes 119.97-119.104 Proverbes 23.23 Jacques 1.5 Luc 10.39
16 Zawadi ya mtu humpatia nafasi; Humleta mbele ya watu wakuu.
Genèse 32.20 1 Samuel 25.27 Genèse 43.11 Proverbes 17.8 Genèse 33.10
17 Ajiteteaye kwanza huonekana kuwa ana haki; Lakini jirani yake huja na kumchunguza.
Proverbes 18.13 2 Samuel 19.24-19.27 2 Samuel 16.1-16.3 Actes 24.12-24.13
18 Kura hukomesha mashindano; Hukata maneno ya wakuu.
Proverbes 16.33 1 Chroniques 24.31 Josué 14.2 1 Chroniques 6.63 1 Samuel 10.21-10.27
19 Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuliko mji wa nguvu; Na mashindano ni kama mapingo ya ngome.
Actes 15.39 Genèse 32.6-32.11 2 Samuel 13.22 Proverbes 6.19 Genèse 4.5-4.8
20 Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake.
Proverbes 12.13-12.14 Proverbes 13.2 Proverbes 25.11-25.12
21 Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake.
Ephésiens 4.29 Matthieu 12.35-12.37 Colossiens 4.6 Proverbes 10.19-10.21 Jacques 3.6-3.9
22 Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa Bwana.
Proverbes 19.14 Proverbes 12.4 Proverbes 31.10-31.31 Ecclésiaste 9.9 Proverbes 8.35
23 Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali.
Jacques 2.3 1 Samuel 25.10 Exode 5.2 Esaïe 66.2 1 Samuel 25.17
24 Ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe; Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu.
Proverbes 17.17 Proverbes 27.9 Jean 15.13-15.15 1 Chroniques 12.38-12.40 Matthieu 26.49-26.50

Cette Bible est dans le domaine public.