Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 29.7
Bible en Swahili de l’est


David exclu de l’armée des Philistins

1 Basi hao Wafilisti wakakusanya majeshi yao yote huko Afeki; nao Waisraeli wakafanya kambi karibu na chemchemi iliyoko Yezreeli.
1 Samuel 4.1 1 Rois 21.1 Josué 19.30 Josué 12.18 1 Rois 20.30
2 Nao mashehe wa Wafilisti wakapita mbele, mia kwa mia, na elfu kwa elfu; naye Daudi na watu wake wakapita wa mwisho pamoja na Akishi.
1 Samuel 28.1-28.2 Josué 13.3 1 Samuel 5.8-5.11 1 Samuel 29.6-29.7 1 Samuel 6.4
3 Ndipo wakuu wa Wafilisti wakasema, Waebrania hawa wafanyani hapa? Naye Akishi akawaambia wakuu wa Wafilisti, Je! Siye huyu Daudi, yule mtumishi wa Sauli, mfalme wa Israeli, ambaye amefuatana na mimi siku hizi, naam, miaka hii, wala mimi nisione hatia kwake, tangu hapo aliponiangukia mimi hata leo?
1 Samuel 27.7 Daniel 6.5 1 Pierre 3.16 Romains 12.17 Jean 19.6
4 Lakini wakuu wa Wafilisti wakamkasirikia; nao wakuu wa Wafilisti wakamwambia, Mrudishe huyu, apate kurejea mahali pake ulipomwagiza, wala asiende pamoja nasi vitani, asije akawa adui wetu vitani; kwani mtu huyu angejipatanisha na bwana wake kwa njia gani? Je! Si kwa vichwa vya watu hawa?
1 Samuel 14.21 1 Chroniques 12.19 Luc 16.8 1 Samuel 27.6
5 Je! Siye huyo Daudi, ambaye waliimbiana habari zake katika michezo, wakisema,Sauli amewaua elfu zake,Na Daudi makumi elfu yake?
1 Samuel 21.11 1 Samuel 18.6-18.7 Proverbes 27.14
6 Ndipo Akishi akamwita Daudi, akamwambia, Aishivyo Bwana, wewe umekuwa mwenye adili, tena kutoka kwako na kuingia kwako pamoja nami katika jeshi ni kwema machoni pangu; kwa sababu mimi sikuona uovu ndani yako tangu siku ile uliponijia hata leo; walakini hao wakuu hawakuridhii.
2 Rois 19.27 2 Samuel 3.25 Psaumes 121.8 1 Samuel 20.3 1 Samuel 29.3
7 Basi sasa urudi, uende zako kwa amani, ili usiwachukize hao mashehe wa Wafilisti.
Nombres 22.34
8 Naye Daudi akamwambia Akishi, Lakini mimi nimefanyaje? Nawe umeona nini kwangu mimi mtumwa wako, muda wote niliokaa mbele yako hata leo, nisipate ruhusa niende na kupigana na adui za bwana wangu mfalme?
Matthieu 6.13 2 Samuel 16.18-16.19 1 Samuel 26.18 1 Samuel 12.3 Psaumes 34.13-34.14
9 Akishi akajibu, akamwambia Daudi, Mimi najua ya kuwa u mwema machoni pangu, kama malaika wa Mungu; ila hao wakuu wa Wafilisti wamesema, Huyu hatakwea pamoja nasi kwenda vitani.
2 Samuel 14.17 2 Samuel 19.27 2 Samuel 14.20 1 Samuel 29.4 Galates 4.14
10 Kwa hiyo sasa amka asubuhi na mapema, wewe na watumwa wa bwana wako waliokuja pamoja nawe; nanyi mtakapoamka asubuhi na mapema, na kupata mwanga, nendeni zenu.
1 Chroniques 12.19 1 Corinthiens 10.13 Psaumes 37.23-37.24 Genèse 22.14 1 Samuel 30.1-30.2
11 Basi Daudi akaamka asubuhi na mapema, yeye na watu wake, kwenda zao asubuhi, kuirudia nchi ya Wafilisti. Nao Wafilisti wakakwea kwenda Yezreeli.
Josué 19.18 2 Samuel 4.4 1 Samuel 29.1

Cette Bible est dans le domaine public.