Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Josué 22.10
Bible en Swahili de l’est


Retour de Ruben, Gad et Manassé chez eux

1 Wakati huo Yoshua akawaita Wareubeni, na Wagadi, na hiyo nusu ya kabila ya Manase,
Deutéronome 29.7-29.8 Nombres 32.18-32.33
2 naye akawaambia, Ninyi mmeyaandama hayo yote mliyoamriwa na Musa, mtumishi wa Bwana, nanyi mmeisikia sauti yangu katika yote niliyowaamuru mimi;
Josué 1.12-1.18 Deutéronome 3.16-3.20 Nombres 32.20-32.29
3 hamkuwaacha hao ndugu zenu siku hizi nyingi hata hivi leo, lakini mmeyashika mausia ya amri ya Bwana, Mungu wenu.
Philippiens 1.23-1.27
4 Na sasa yeye Bwana, Mungu wenu, amewapa ndugu zenu kustarehe, kama alivyowaambia; basi sasa rudini ninyi mwende mahemani kwenu, hata nchi ya milki yenu, ambayo huyo Musa, mtumishi wa Bwana, aliwapa ng’ambo ya pili ya Yordani.
Josué 13.8 Deutéronome 3.1-3.17 Deutéronome 12.9 Nombres 32.18 Josué 21.43-21.44
5 Lakini mjibidiishe sana kuzifanya amri na sheria, ambazo Musa, mtumishi wa Bwana, aliwaamuru, kumpenda Bwana, Mungu wenu, na kwenenda katika njia zake zote, na kuzishika amri zake, na kushikamana na yeye, na kumtumikia kwa moyo wenu wote na nafsi yenu yote.
Deutéronome 6.17 Matthieu 4.10 Deutéronome 11.22 Deutéronome 11.1 Deutéronome 11.13
6 Basi Yoshua akawabarikia, na kuwapa ruhusa waende zao; nao wakaenda mahemani kwao.
Josué 14.13 Luc 24.50 Exode 39.43 2 Samuel 6.18 Genèse 47.7
7 Basi Musa alikuwa amewapa hiyo nusu moja ya kabila ya Manase urithi katika Bashani; lakini hiyo nusu ya pili Yoshua aliwapa urithi kati ya ndugu zao, ng’ambo ya Yordani upande wa kuelekea magharibi. Zaidi ya hayo Yoshua, hapo alipowapeleka waende zao mahemani kwao, akawabarikia,
Josué 17.1-17.12 Josué 13.29-13.31 Nombres 32.33
8 kisha akanena nao, na kuwaambia, Rudini na mali mengi mahemani kwenu, na ng’ombe wengi sana, na fedha, na dhahabu, na shaba, na chuma, na mavao mengi sana; mzigawanye na ndugu zenu hizo nyara za adui zenu.
Nombres 31.27 1 Samuel 30.24 Deutéronome 8.9-8.14 1 Samuel 30.16 Hébreux 11.26
9 Basi wana wa Reubeni, na wana wa Gadi, na hiyo nusu ya kabila ya Manase wakarudi, wakatoka kwa wana wa Israeli katika Shilo, ulioko nchi ya Kanaani, ili waende nchi ya Gileadi, hiyo nchi ya milki yao, waliyokuwa wanaimiliki, sawasawa na amri ya Bwana kwa mkono wa Musa.
Nombres 32.29 Nombres 32.26 Nombres 32.1 Josué 13.25 Deutéronome 3.15-3.16
10 Nao walipofika pande za Yordani, zilizo katika nchi ya Kanaani, hao wana wa Reubeni, na wana wa Gadi, na nusu ya kabila ya Manase, wakajenga madhabahu huko karibu na Yordani, iliyoonekana kuwa ni madhabahu kubwa.
Josué 22.25-22.28 Josué 4.5-4.9 Josué 24.26-24.27 Genèse 31.46-31.52 Genèse 28.18
11 Wana wa Israeli walisikia ikinenwa, Tazama, wana wa Reubeni, na wana wa Gadi, na hiyo nusu ya kabila ya Manase, wamejenga madhabahu huko upande wa mbele wa nchi ya Kanaani, katika nchi iliyo karibu na Yordani, kwa upande huo ulio milki ya wana wa Israeli.
Deutéronome 13.12-13.14 Juges 12.5 Deutéronome 12.5-12.7 Josué 3.14-3.16 Jean 20.12
12 Basi, wana wa Israeli waliposikia habari hiyo, mkutano wote wa wana wa Israeli wakakutanika pamoja huko Shilo, ili waende kupigana nao.
Actes 11.2-11.3 Josué 18.1 Juges 20.1-20.11 Romains 10.2 Deutéronome 13.15
13 Kisha wana wa Israeli wakatuma wajumbe waende kwa wana wa Reubeni, na wana wa Gadi, na hiyo nusu ya kabila ya Manase, hata nchi ya Gileadi; nao ni hawa, Finehasi mwana wa Eleazari kuhani;
Nombres 25.7 Exode 6.25 Juges 20.28 Juges 20.12 Proverbes 20.18
14 na pamoja naye wakuu kumi, mkuu mmoja wa nyumba ya mababa kwa ajili ya kila kabila ya Israeli; nao kila mmoja alikuwa ni kichwa cha nyumba ya mababa katika maelfu ya Israeli.
Nombres 1.4 Exode 18.25
15 Nao wakawafikilia hao wana wa Reubeni, na wana wa Gadi, na hiyo nusu ya kabila ya Manase, katika nchi ya Gileadi, na wakasema nao, wakinena,
1 Chroniques 21.3 1 Samuel 15.23 Nombres 32.15 Matthieu 6.14-6.15 Esaïe 63.10
16 Mkutano wote wa Bwana wanena, Ni kosa gani hili mlilolikosa juu ya Mungu wa Israeli, hata mkakengeuka hivi leo na kuacha kumwandama Bwana, katika kujijengea madhabahu, na kuasi hivi leo juu ya Bwana?
Deutéronome 12.13-12.14
17 Je! Ule uovu wa Peori haututoshi, ambao hamjajitakasa nafsi zenu katika huo hata hivi leo, ijapokuwa ilikuja tauni juu ya mkutano wa Bwana,
Deutéronome 4.3-4.4 Nombres 25.1-25.18 Psaumes 106.28-106.29 1 Corinthiens 10.8 1 Corinthiens 10.11
18 hata ikawa hamna budi hivi leo kugeuka na kuacha kumwandama Bwana? Kisha itakuwa, kwa kuwa ninyi mwamwasi Bwana hivi leo, kwamba kesho yeye atakasirika na mkutano wote wa Israeli.
Nombres 16.22 Josué 22.16 Deutéronome 7.4 Josué 22.20 Esdras 9.13-9.14
19 Basi kwamba hiyo nchi ya milki yenu si tohara, ndipo ninyi vukeni na kuingia nchi ya milki yake Bwana, ambayo maskani ya Bwana inakaa ndani yake, nanyi twaeni milki kati yetu; lakini msimwasi Bwana, wala msituasi sisi, kwa kujijengea madhabahu zaidi ya hiyo madhabahu ya Bwana, Mungu wetu.
Josué 18.1 Actes 10.14-10.15 Lévitique 18.25-18.28 Exode 15.17 Actes 11.8-11.9
20 Je! Huyo Akani mwana wa Zera hakukosa katika vile vitu vilivyowekwa wakfu, na hasira ikauangukia mkutano wote wa Israeli? Kisha mtu huyo hakuangamia peke yake katika uovu wake?
Josué 7.1 Josué 7.5 Josué 7.18 Josué 7.24 1 Corinthiens 10.6
21 Ndipo hapo wana wa Reubeni, na wana wa Gadi, na hiyo nusu ya kabila ya Manase, wakajibu, na kuwaambia hao waliokuwa ni vichwa vya maelfu ya Israeli, wakasema,
1 Pierre 3.15 Michée 5.2 Proverbes 24.26 Proverbes 18.13 Exode 18.21-18.25
22 Mungu, Mungu Bwana, naam, Mungu, Mungu Bwana, yeye yuajua, na Israeli naye atajua; kama ni katika uasi, au kama ni katika kosa juu ya Bwana, (usituokoe hivi leo);
1 Rois 8.39 Deutéronome 10.17 Psaumes 44.21 Job 10.7 Jérémie 17.10
23 sisi kujijengea madhabahu ili kukengeuka na kuacha kumwandama Bwana; au kama ni kusongeza juu yake sadaka ya kuteketezwa, au sadaka ya unga, au kama ni kusongeza sadaka za amani juu yake, yeye Bwana mwenyewe na alitake jambo hili;
1 Samuel 20.16 Deutéronome 18.19 Ezéchiel 33.8 Ezéchiel 3.18 Genèse 9.4
24 au kama sisi tumefanya jambo hili kwa hadhari sana, tena makusudi, huku tukisema, Katika siku zijazo wana wenu yamkini wakanena na wana wetu, na kusema, Ninyi mna nini na Bwana, yeye Mungu wa Israeli?
Josué 4.6 Exode 13.14 Deutéronome 6.20 Genèse 18.19 Genèse 30.33
25 Kwa kuwa yeye Bwana ameufanya huu mto wa Yordani uwe mpaka katikati ya sisi na ninyi, enyi wana wa Reubeni, na wana wa Gadi, hamna fungu katika Bwana; basi hivyo wana wenu wangewakomesha wana wetu wasimche Bwana.
1 Rois 15.30 1 Rois 14.16 Josué 22.27 Esdras 4.2-4.3 Néhémie 2.20
26 Kwa ajili ya hayo tulisema, Na tufanye tayari ili kujijengea madhabahu, si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kwa sadaka yo yote;
27 bali itakuwa ni ushahidi kati ya sisi na ninyi, tena kati ya vizazi vyetu baada yetu, ili kwamba tufanye huo utumishi wa Bwana mbele yake kwa njia ya sadaka zetu za kuteketezwa, na kwa dhabihu zetu, na kwa sadaka zetu za amani; ili kwamba wana wenu wasiwaambie wana wetu katika zamani zijazo, Ninyi hamna fungu katika Bwana.
Josué 24.27 Genèse 31.48 Deutéronome 12.5-12.6 Josué 22.34 Deutéronome 12.17-12.18
28 Kwa hiyo tulisema, Itakuwa, hapo watakapotuambia neno kama hilo, au kuwaambia watu wa vizazi vyetu katika zamani zijazo neno kama hilo, ndipo sisi tutawaambia, Angalieni huu mfano wa madhabahu ya Bwana, walioufanya baba zetu, si kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, wala kwa ajili ya dhabihu; lakini ni ushahidi kati ya sisi na ninyi.
Hébreux 8.5 Exode 25.40 2 Rois 16.10 Ezéchiel 43.10-43.11
29 Mungu na atuzuie msimwasi Bwana, na kukengeuka hivi leo na kuacha kumwandama Bwana, hata mkajenga madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, au sadaka za unga, au dhabihu, mbali na ile madhabahu ya Bwana, Mungu wetu, iliyo huko mbele ya maskani yake.
Deutéronome 12.13-12.14 Josué 24.16 1 Samuel 12.23 Genèse 44.17 2 Rois 18.22
30 Basi Finehasi kuhani, na wakuu wa mkutano, maana, ni hao waliokuwa vichwa vya maelfu ya Israeli waliokuwa pamoja naye, hapo walipoyasikia hayo maneno waliyoyasema hao wana wa Reubeni, na wana wa Gadi, na wana wa Manase, maneno hayo yaliwaridhia sana.
Josué 22.33 Actes 11.18 1 Samuel 29.6 1 Samuel 25.32-25.33 Genèse 28.8
31 Naye Finehasi, mwana wa Eleazari, kuhani, akawaambia wana wa Reubeni, na wana wa Gadi, na wana wa Manase, akasema, Siku hii ya leo twajua ya kwamba Bwana yu kati yetu, kwa sababu hamkukosa katika jambo hili mbele ya Bwana; sasa ninyi mmewaokoa wana wa Israeli na mkono wa Bwana.
Lévitique 26.11-26.12 2 Chroniques 15.2 Zacharie 8.23 Psaumes 68.17 Matthieu 1.23
32 Kisha Finehasi, mwana wa Eleazari, kuhani, na hao wakuu, wakarudi na kuwaacha wana wa Reubeni, na wana wa Gadi, wakatoka katika nchi ya Gileadi, na kuingia nchi ya Kanaani; wakawarudia wana wa Israeli, wakawapa habari.
Proverbes 25.13 Josué 22.12-22.14
33 Wana wa Israeli nao wakaliridhia jambo hilo; nao wana wa Israeli wakamhimidi Mungu, wala hawakusema tena habari ya kuwaendea juu yao kupigana nao, wala kuiharibu nchi waliyoikaa wana wa Reubeni, na wana wa Gadi.
1 Chroniques 29.20 Luc 2.28 Daniel 2.19 Josué 22.30 2 Corinthiens 7.7
34 Basi hao wana wa Reubeni, na wana wa Gadi, wakaiita madhabahu hiyo Edi; wakasema, Kwa kuwa ni ushahidi kati yetu ya kwamba yeye Bwana ndiye Mungu.
Josué 22.27 1 Rois 18.39 Matthieu 4.10 Josué 24.27 Esaïe 43.10

Cette Bible est dans le domaine public.