Salutation et louange
 1 Paulo, na Silwano, na Timotheo, kwa kanisa la Wathesalonike, lililo katika Mungu Baba, na katika Bwana Yesu Kristo. Neema na iwe kwenu na amani.
Romains 1.7  2 Thessaloniciens 1.1  2 Corinthiens 1.19  Actes 18.5  1 Pierre 5.12  
 2 Twamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu nyote, tukiwataja katika maombi yetu.
Romains 1.8-1.9  Ephésiens 1.15-1.16  Colossiens 1.3  1 Corinthiens 1.4  Philémon 1.4  
 3 Wala hatuachi kuikumbuka kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya upendo, na saburi yenu ya tumaini lililo katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele za Mungu Baba yetu.
1 Corinthiens 13.13  2 Thessaloniciens 1.11  Apocalypse 2.19  Galates 5.6  Romains 8.24-8.25  
 4 Kwa maana, ndugu mnaopendwa na Mungu, twajua uteule wenu;
2 Thessaloniciens 2.13  2 Pierre 1.10  Tite 3.4-3.5  1 Thessaloniciens 1.3  Ephésiens 2.4-2.5  
 5 ya kwamba injili yetu haikuwafikia katika maneno tu, bali na katika nguvu, na katika Roho Mtakatifu, na uthibitifu mwingi; kama vile mnavyojua jinsi zilivyokuwa tabia zetu kwenu, kwa ajili yenu.
2 Thessaloniciens 2.14  Colossiens 2.2  1 Pierre 1.12  Marc 16.20  1 Corinthiens 2.2-2.5  
 6 Nanyi mkawa wafuasi wetu na wa Bwana, mkiisha kulipokea neno katika dhiki nyingi, pamoja na furaha ya Roho Mtakatifu.Actes 13.52  Galates 5.22  1 Corinthiens 11.1  Actes 17.5-17.10  1 Corinthiens 4.16  
 7 Hata mkawa kielelezo kwa watu wote waaminio katika Makedonia, na katika Akaya.
Tite 2.7  1 Timothée 4.12  2 Corinthiens 9.2  1 Pierre 5.3  1 Thessaloniciens 1.8  
 8 Maana kutoka kwenu neno la Mungu limevuma, si katika Makedonia na Akaya tu, ila na kila mahali imani yenu mliyo nayo kwa Mungu imeenea; hata hatuna haja sisi kunena lo lote.
Romains 1.8  2 Thessaloniciens 1.4  2 Thessaloniciens 3.1  1 Corinthiens 14.36  Exode 18.9  
 9 Kwa kuwa wao wenyewe wanatangaza habari zetu, jinsi kulivyokuwa kuingia kwetu kwenu; na jinsi mlivyomgeukia Mungu mkaziacha sanamu, ili kumtumikia Mungu aliye hai, wa kweli;
1 Timothée 4.10  Galates 4.8-4.9  1 Corinthiens 12.2  Actes 14.15  Romains 9.26  
 10 na kumngojea Mwanawe kutoka mbinguni, ambaye alimfufua katika wafu, naye ni Yesu, mwenye kutuokoa na ghadhabu itakayokuja.
1 Thessaloniciens 5.9  Matthieu 3.7  Actes 2.24  Romains 4.25  Actes 1.11