Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 8.2
Bible en Swahili de l’est


Terre promise et reconnaissance

1 Amri hii ninayokuamuru leo mtaishika kuitenda, mpate kuishi na kuongezeka, na kuingia katika nchi ile ambayo Bwana aliwaapia baba zenu; nanyi mtaimiliki.
Deutéronome 4.1 Deutéronome 5.32-6.3 1 Thessaloniciens 4.1-4.2 Psaumes 119.4-119.6
2 Nawe utaikumbuka njia ile yote Bwana, Mungu wako aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, kukujaribu kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo.
Jacques 1.3 Amos 2.10 2 Chroniques 32.31 Exode 15.25 1 Pierre 5.5-5.6
3 Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha Bwana.
Matthieu 4.4 Luc 4.4 Exode 16.2-16.3 Psaumes 78.23-78.25 Hébreux 13.5-13.6
4 Mavazi yako hayakuchakaa, wala mguu wako haukuvimba, miaka hiyo arobaini.
Deutéronome 29.5 Néhémie 9.21 Matthieu 26.25-26.30
5 Nawe fikiri moyoni mwako, ya kuwa kama vile baba amrudivyo mwanawe, ndivyo Bwana, Mungu wako, akurudivyo.
Apocalypse 3.19 Proverbes 3.12 2 Samuel 7.14 1 Corinthiens 11.32 Hébreux 12.5-12.11
6 Nawe uzishike amri za Bwana, Mungu wako, upate kwenda katika njia zake, na kumcha.
Deutéronome 5.33 Exode 18.20 Luc 1.6 Psaumes 128.1 2 Chroniques 6.31
7 Kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yuakuingiza katika nchi nzuri, nchi yenye vijito vya maji, na chemchemi, na visima, vibubujikavyo katika mabonde na milima;
Deutéronome 11.9-11.12 Psaumes 65.9-65.13 Ezéchiel 20.6 Néhémie 9.24-9.25 Exode 3.8
8 nchi ya ngano na shayiri, na mizabibu, na mitini, na mikomamanga; nchi ya mizeituni yenye mafuta, na asali;
1 Rois 5.11 Esaïe 7.23 Michée 4.4 Psaumes 81.16 Jean 6.13
9 nchi utakayokula mikate humo, pasina shida, hutapungukiwa na kitu ndani yake; nchi ambayo mawe yake ni chuma, na milima yake yafukuka shaba.
1 Chroniques 22.14 Deutéronome 33.25 Josué 22.8 Job 28.2
10 Nawe utakula ushibe, utamshukuru Bwana, Mungu wako, kwa nchi nzuri aliyokupa.
Psaumes 103.2 Matthieu 14.19 Romains 14.6 Deutéronome 6.11-6.12 Proverbes 3.9
11 Jihadhari, usije ukamsahau Bwana, Mungu wako, kwa kutozishika amri zake, na hukumu zake, na sheria zake, ninazokuamuru leo.
Proverbes 1.32 Osée 2.8-2.9 Psaumes 106.21 Proverbes 30.9 Ezéchiel 16.10-16.15
12 Angalia, utakapokuwa umekula na kushiba, na kujenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake;
Proverbes 30.9 Deutéronome 28.47 Deutéronome 32.15 Ecclésiaste 2.4 Aggée 1.4
13 na makundi yako ya ng’ombe na kondoo yatakapoongezeka, na fedha yako na dhahabu yako itakapoongezeka, na kila kitu ulicho nacho kitakapoongezeka;
Genèse 13.1-13.5 Psaumes 39.6 Job 1.3 Luc 12.13-12.21
14 basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau Bwana, Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa;
Psaumes 106.21 Deutéronome 8.11 2 Chroniques 32.25 2 Chroniques 26.16 1 Corinthiens 4.7-4.8
15 aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa lenye kitisho, lenye nyoka za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji; aliyekutolea maji katika mwamba mgumu,
Psaumes 114.8 Nombres 20.11 Nombres 21.6 Jérémie 2.6 Deutéronome 1.19
16 aliyekulisha jangwani kwa mana, wasiyoijua baba zako; apate kukutweza, apate kukujaribu, ili kukutendea mema mwisho wako.
Exode 16.15 Jérémie 24.5-24.6 Deutéronome 8.3 Hébreux 12.10-12.11 Romains 8.28
17 Hapo usiseme moyoni mwako, Nguvu zangu na uwezo wa mkono wangu ndio ulionipatia utajiri huo.
Deutéronome 9.4 Habakuk 1.16 1 Corinthiens 4.7 Osée 12.8 Deutéronome 7.17
18 Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.
Proverbes 10.22 Osée 2.8 Psaumes 127.1-127.2 Deutéronome 7.8 Deutéronome 7.12
19 Lakini itakuwa, kama ukimsahau Bwana, Mungu wako, na kuiandama miungu mingine, na kuitumikia na kuiabudu, nawashuhudia leo ya kuwa mtaangamia bila shaka.
Deutéronome 4.26 Luc 13.5 1 Samuel 12.25 Josué 23.13 Amos 3.2
20 Kama vile mataifa yale ambayo Bwana anawaangamiza mbele yenu, ndivyo mtakavyoangamia; kwa sababu hamkutaka kuisikiliza sauti ya Bwana, Mungu wenu.
Daniel 9.11-9.12 2 Chroniques 36.16-36.17

Cette Bible est dans le domaine public.