Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 5.7
Bible en Swahili de l’est


1 Musa akawaita Israeli wote, akawaambia, Enyi Israeli, zisikieni amri na hukumu ninenazo masikioni mwenu leo, mpate kujifunza na kuangalia kuzitenda.
Deutéronome 1.1 Deutéronome 29.10 Deutéronome 4.1 Deutéronome 29.2 Matthieu 23.3
2 Bwana, Mungu wetu, alifanya agano nasi katika Horebu.
Deutéronome 4.23 Hébreux 9.19-9.23 Hébreux 8.6-8.13 Exode 19.5-19.8 Exode 24.8
3 Bwana hakufanya agano hili na baba zetu, bali na sisi, yaani, sisi sote tuliopo hapa, tu hai.
Deutéronome 29.10-29.15 Genèse 17.7 Hébreux 8.8-8.9 Psaumes 105.8-105.10 Jérémie 32.38-32.40
4 Bwana alisema nanyi uso kwa uso mlimani, toka kati ya moto;
Deutéronome 34.10 Deutéronome 4.33 Exode 33.11 Deutéronome 4.36 Exode 19.18-19.19
5 (nami wakati ule nalisimama kati ya Bwana na ninyi, ili kuwaonyesha neno la Bwana; maana, mliogopa kwa sababu ya ule moto, wala hamkupanda mlimani); naye akasema,
Galates 3.19 Exode 19.16 Exode 20.18-20.21 Psaumes 106.23 Deutéronome 5.27
6 Mimi ni Bwana, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.
Exode 20.2-20.17 Psaumes 81.5-81.10 Lévitique 26.1-26.2 Deutéronome 4.4
7 Usiwe na miungu mingine ila mimi.
Exode 20.3 Jean 5.23 1 Jean 5.21 Matthieu 4.10
8 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, au kilicho chini duniani, au kilicho majini chini ya nchi.
Exode 20.4 Deutéronome 4.15-4.19
9 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, nawapatiliza wana uovu wa baba zao; hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
Exode 34.7 Exode 34.14 Nombres 14.18 Romains 11.28-11.29 Matthieu 23.35-23.36
10 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.
Jérémie 32.18 Deutéronome 6.5-6.6 Jean 15.14 Jacques 1.25 Deutéronome 10.12-10.13
11 Usilitaje bure Jina la Bwana, Mungu wako; maana Bwana hatamhesabia kuwa hana hatia, mtu alitajaye jina lake bure.
Lévitique 19.12 Deutéronome 6.13 Matthieu 5.33-5.34 Exode 20.7 Jérémie 4.2
12 Ishike siku ya Sabato uitakase, kama Bwana, Mungu wako, alivyokuamuru.
Exode 20.8-20.11 Esaïe 58.13 Esaïe 56.6
13 Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;
Exode 35.2-35.3 Exode 23.12 Ezéchiel 20.12 Luc 23.56 Luc 13.14-13.16
14 lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako; siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwanao, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala ng’ombe wako, wala punda wako, wala mnyama wako ye yote, wala mgeni aliye ndani ya malango yako, ili mtumwa wako na mjakazi wako wapumzike vile vile kama wewe.
Hébreux 4.4 Genèse 2.2 Exode 16.29-16.30 Exode 23.12 Néhémie 13.15
15 Nawe utakumbuka ya kuwa wewe ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri, na ya kuwa Bwana, Mungu wako, alikutoa huko kwa mkono wenye nguvu, na mkono ulionyoshwa; kwa sababu hiyo Bwana, Mungu wako, alikuamuru uishike sabato.
Deutéronome 16.12 Deutéronome 15.15 Psaumes 116.16 Esaïe 63.9 Deutéronome 24.18-24.22
16 Waheshimu baba yako na mama yako; kama Bwana, Mungu wako, alivyokuamuru, siku zako zipate kuzidi, nawe upate kufanikiwa katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.
Deutéronome 4.40 Exode 20.12 Lévitique 19.3 Deutéronome 27.16 Colossiens 3.20
17 Usiue.
Exode 20.13 Matthieu 5.21-5.22 Jacques 2.11 Genèse 9.6 Matthieu 19.18
18 Wala usizini.
Luc 18.20 Exode 20.14 Matthieu 5.27-5.28 Proverbes 6.32-6.33 Lévitique 20.10
19 Wala usiibe.
Exode 20.15 Ephésiens 4.28 Romains 13.9
20 Wala usimshuhudie jirani yako uongo.
Exode 23.1 Exode 20.16 Proverbes 6.19 Proverbes 19.5 Proverbes 19.9
21 Wala usimtamani mke wa jirani yako; wala usiitamani nyumba ya jirani yako, wala shamba lake, wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng’ombe wake, wala punda wake, wala kitu cho chote alicho nacho jirani yako.
Romains 13.9 Exode 20.17 1 Rois 21.1-21.4 Michée 2.2 1 Timothée 6.9-6.10
22 Haya ndiyo maneno ambayo Bwana aliwaambia mkutano wenu wote mlimani kwa sauti kuu toka kati ya moto, na wingu, na giza kuu; wala hakuongeza neno. Akayaandika juu ya mbao mbili za mawe, akanipa.
Exode 24.12 Exode 31.18 Exode 19.18-19.19 Deutéronome 5.4 Deutéronome 4.12-4.15
23 Ikawa, mlipoisikia sauti ile toka kati ya giza, na wakati uo huo mlima ule ulikuwa ukiwaka moto, basi, mlinikaribia, naam, wakuu wote wa kabila zenu, na wazee wenu,
Hébreux 12.18-12.21 Exode 20.18-20.19
24 mkasema, Tazama, Bwana, Mungu wetu, ametuonyesha utukufu wake, na ukuu wake, nasi tunasikia sauti yake toka kati ya moto; mmeona leo ya kuwa Mungu husema na mwanadamu, naye akaishi.
Exode 19.19 Deutéronome 4.33 Exode 33.20 Genèse 32.30 Juges 13.22
25 Sasa basi, mbona tufe? Maana moto huu mkubwa utatuteketeza; tukiisikia tena sauti ya Bwana, Mungu wetu, tutakufa.
Deutéronome 18.16 2 Corinthiens 3.7-3.9 Deutéronome 33.2 Hébreux 12.29 Galates 3.21-3.22
26 Maana katika wote wenye mwili ni nani aliyeisikia sauti ya Mungu aliye hai, akisema toka kati ya moto, kama vile sisi, asife?
Deutéronome 4.33 Romains 3.20 Actes 14.15 Psaumes 84.2 Josué 3.10
27 Enenda karibu wewe, ukasikie yote atakayoyasema Bwana, Mungu wetu; ukatuambie yote atakayokuambia Bwana, Mungu wetu; nasi tutayasikia na kuyatenda.
Hébreux 12.19 Exode 20.19
28 Naye Bwana akasikia sauti ya maneno yenu mliyoniambia; Bwana akaniambia, Nimesikia sauti ya maneno ya watu hawa waliyokuambia; wamesema vema yote waliyosema.
Deutéronome 18.17 Nombres 27.7 Nombres 36.5
29 Laiti wangekuwa na moyo kama huu ndani yao sikuzote, wa kunicha, na kushika amri zangu zote sikuzote, wapate kufanikiwa wao na watoto wao milele!
Esaïe 48.18 Deutéronome 4.40 Ezéchiel 33.31-33.32 Deutéronome 11.1 Luc 19.42
30 Enda uwaambie, Rudini hemani mwenu.
31 Lakini wewe, simama hapa karibu nami, nami nitanena nawe sheria zote, na amri na hukumu, utakazowafunza, wapate kuzifanya katika nchi niwapayo kuimiliki.
Galates 3.19 Exode 24.12 Malachie 4.4 Deutéronome 4.1 Ezéchiel 20.11
32 Tunzeni basi, mtende kama mlivyoamriwa na Bwana, Mungu wenu; msikengeuke kwa mkono wa kuume wala wa kushoto.
Josué 23.6 Proverbes 4.27 Josué 1.7 Deutéronome 17.20 Deutéronome 28.14
33 Endeni njia yote aliyowaagiza Bwana, Mungu wenu, mpate kuwa hai, na kufanikiwa, mkafanye siku zenu kuwa nyingi katika nchi mtakayoimiliki.
Jérémie 7.23 Deutéronome 4.40 Deutéronome 10.12 Luc 1.6 Romains 2.7

Cette Bible est dans le domaine public.