Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 16.6
Bible en Swahili de l’est


La Pâque

1 Utunze mwezi wa Abibu, ukamfanyie pasaka Bwana, Mungu wako, kwa kuwa ilikuwa ni mwezi wa Abibu alipokutoa Misri usiku Bwana; Mungu wako.
Exode 34.18 Exode 13.4 Exode 12.2-12.20 Nombres 28.16 Lévitique 23.5
2 Nawe umchinjie pasaka Bwana, Mungu wako, katika kundi la kondoo na la ng’ombe, mahali atakapochagua Bwana apakalishe jina lake.
Deutéronome 12.5 Deutéronome 12.26 Deutéronome 12.11 Marc 14.12 1 Corinthiens 5.7
3 Usimle pamoja na mikate iliyotiwa chachu; siku saba utakula naye mikate isiyotiwa chachu, nayo ni mikate ya mateso; kwa maana ulitoka nchi ya Misri kwa haraka; ili upate kukumbuka siku uliyotoka nchi ya Misri, siku zote za maisha yako.
Exode 12.39 Exode 34.18 Nombres 9.11 Exode 12.8 Exode 12.19-12.20
4 Wala isionekane kwako chachu muda wa siku saba katika mipaka yako yote; wala katika hiyo nyama uchinjayo siku ya kwanza jioni, kisilale cho chote usiku kucha hata asubuhi.
Exode 12.10 Exode 34.25 Exode 13.7 Exode 12.15 Exode 12.8
5 Usimchinje pasaka ndani ya malango yako yote akupayo Bwana, Mungu wako;
Deutéronome 12.5-12.6 Deutéronome 16.2
6 ila mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako, apakalishe jina lake, ndipo mtakapomchinja pasaka jioni, katika machweo ya jua, kwa wakati kama uliotoka Misri.
Nombres 9.3 Hébreux 9.26 Matthieu 26.20 Exode 12.6-12.9 1 Pierre 1.19-1.20
7 Nawe umwoke na kumla mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako; kisha asubuhi yake ugeuke uende hemani mwako.
2 Chroniques 35.13 Deutéronome 16.2 Jean 2.23 Jean 2.13 Psaumes 22.14-22.15
8 Siku sita utakula mikate isiyotiwa chachu; na siku ya saba na uwe mkutano mtukufu kwa Bwana, Mungu wako, usifanye kazi yo yote.
Lévitique 23.36 Exode 13.6-13.8 Nombres 28.17-28.19 Lévitique 23.6-23.8 Exode 12.15-12.16

La fête des semaines

9 Jihesabie majuma saba; tangu wakati uanzao kutia mundu katika mmea utaanza kuhesabu majuma saba.
Exode 23.16 Exode 34.22 Actes 2.1 Lévitique 23.15-23.16 Deutéronome 16.10
10 Nawe sikukuu ya majuma umfanyie Bwana, Mungu wako, kwa kutoa sadaka ya hiari ya mkono wako, utakayotoa kwa kadiri akubarikiavyo Bwana, Mungu wako;
1 Corinthiens 16.2 Nombres 31.37 2 Corinthiens 8.12 Lévitique 12.8 Proverbes 3.9-3.10
11 nawe utafurahi mbele ya Bwana, Mungu wako, wewe na mwana wako na binti yako, na mtumwa wako na mjakazi wako, na Mlawi aliye ndani ya malango yako, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio katikati yako, katika mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako, apakalishe jina lake.
Deutéronome 12.12 Deutéronome 12.7 Deutéronome 12.18 Romains 5.11 2 Corinthiens 1.24
12 Nawe kumbuka kwamba ulikuwa mtumwa huko Misri; tena zishike amri hizi kwa kuzifanya.
Deutéronome 15.15 Romains 6.17-6.18 Ephésiens 2.11 Lamentations 3.19-3.20 Ephésiens 2.1-2.3

La fête des tentes

13 Fanya sikukuu ya vibanda siku saba, utakapokwisha kuyakusanya yatokayo katika sakafu yako ya nafaka, na katika kinu chako cha divai;
Exode 23.16 Lévitique 23.34-23.36 Jean 7.2 2 Chroniques 8.13 Exode 34.22
14 nawe utafurahi katika sikukuu yako, wewe, na mwanao, na binti yako, na mtumwa wako, na mjakazi wako, na Mlawi, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio ndani ya malango yako.
Néhémie 8.9-8.12 Deutéronome 16.11 Ecclésiaste 9.7 Deutéronome 12.12 1 Thessaloniciens 5.16
15 Siku saba mfanyie sikukuu Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua Bwana; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, atakubarikia katika maongeo yako yote, na katika kazi zote za mikono yako, nawe uwe katika kufurahi kabisa.
Deutéronome 7.13 Deutéronome 30.16 Lévitique 23.36-23.42 Deutéronome 16.10 Nombres 29.12-29.38
16 Mara tatu kwa mwaka na watokee wanawaume wako wote mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua; katika sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu, na katika sikukuu ya majuma, na katika sikukuu ya vibanda; wala wasitokee mbele za Bwana mikono mitupu.
Proverbes 3.9-3.10 Aggée 1.9 Matthieu 2.11 Exode 23.14-23.17 1 Chroniques 29.3-29.9
17 Kila mtu na atoe kama awezavyo, kwa kadiri ya baraka ya Bwana, Mungu wako, alivyokupa.
Deutéronome 16.10 2 Corinthiens 8.12 Lévitique 27.8 Esdras 2.63 2 Corinthiens 9.6-9.7

Institution des juges

18 Weka waamuzi na maakida katika malango yako yote akupayo Bwana, Mungu wako, kwa hesabu ya kabila zako; nao wawaamue watu kwa maamuzi ya haki.
1 Chroniques 23.4 1 Chroniques 26.29 Deutéronome 17.12 Deutéronome 1.15-1.17 Deutéronome 17.9
19 Usipotoe maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; wala usitwae rushwa; kwa kuwa rushwa hupofusha macho ya wenye akili, na kugeuza daawa ya wenye haki.
Lévitique 19.15 Exode 23.2 Ecclésiaste 7.7 Proverbes 24.23 Deutéronome 27.19
20 Yaliyo haki kabisa ndiyo utakayoyafuata, ili upate kuishi na kuirithi nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.
Deutéronome 4.1 Michée 6.8 Ezéchiel 18.5 Philippiens 4.8 Deutéronome 25.13-25.16

Avertissements contre l’idolâtrie

21 Usipande mti uwao wote kuwa Ashera kwako kando ya madhabahu utakayofanya ya Bwana, Mungu wako.
2 Rois 17.16 2 Chroniques 33.3 Exode 34.13 2 Rois 21.3 1 Rois 16.33
22 Wala usisimamishe nguzo; ambayo Bwana, Mungu wako, aichukia.
Lévitique 26.1 Exode 20.4 Apocalypse 2.15 Deutéronome 12.31 Zacharie 8.17

Cette Bible est dans le domaine public.