Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 13.16
Bible en Swahili de l’est


1 Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu,
Jérémie 23.25-23.28 Zacharie 10.2 Jérémie 27.9 Jérémie 29.8 2 Thessaloniciens 2.9

Punition des prétendus prophètes et des idolâtres

2 ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo;
Deutéronome 18.22 Jérémie 28.9 Deutéronome 13.6 Deutéronome 13.13 Apocalypse 13.13-13.14
3 wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda Bwana, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote.
Deutéronome 8.2 1 Corinthiens 11.19 Deutéronome 6.5 2 Corinthiens 8.8 Esaïe 8.20
4 Tembeeni kwa kumfuata Bwana, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye.
Deutéronome 10.20 2 Chroniques 34.31 2 Rois 23.3 1 Corinthiens 6.17 1 Thessaloniciens 4.1-4.2
5 Na yule nabii, au yule mwotaji wa ndoto, na auawe, kwa kuwa amesema yaliyopotoka juu ya Bwana, Mungu wenu, aliyewatoa katika nchi ya Misri, akakukomboa katika nyumba ya utumwa, apate yule mtu kukupotoa katika njia aliyokuamuru Bwana, Mungu wako, uiendee. Ndivyo utakavyouondoa uovu utoke katikati yako.
1 Corinthiens 5.13 Deutéronome 17.7 Deutéronome 19.19 Deutéronome 18.20 1 Rois 18.40
6 Atakapokushawishi kwa siri ndugu yako, mwana wa mamaako, au mwana wako, au binti yako, au mke wa kifuani mwako, au rafiki yako aliye kama moyo wako, akikuambia, Twende tukaabudu miungu mingine usiyoijua wewe wala baba zako;
Deutéronome 17.2-17.7 1 Samuel 18.1 1 Samuel 20.17 Deutéronome 28.54 1 Samuel 18.3
7 katika miungu ya mataifa yaliyo kando-kando yenu karibu nawe au mbali nawe, tokea ncha moja ya dunia hata ncha ya pili ya dunia;
8 usimkubalie wala usimsikize; wala jicho lako lisimwonee huruma, wala usimwache, wala usimfiche;
Proverbes 1.10 Deutéronome 7.16 Deutéronome 19.13 Galates 1.8-1.9 1 Jean 5.21
9 mwue kweli; mkono wako na uwe wa kwanza juu yake katika kumwua, na baadaye mikono ya watu wote.
Jean 8.7 Deutéronome 17.2-17.7 Actes 7.58 Matthieu 10.37 Luc 14.26
10 Nawe mtupie mawe hata afe; kwa kuwa alitaka kukupotoa na Bwana, Mungu wako aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.
Josué 7.25 Lévitique 20.2 Exode 20.2 Lévitique 24.23 2 Chroniques 24.21
11 Na Israeli wote watasikia na kuogopa, wasifanye tena uovu mfano wa huo katikati yako.
Deutéronome 19.20 Deutéronome 17.13 Proverbes 21.11 Proverbes 19.25 1 Timothée 5.20
12 Ukisikia yasemwa habari ya miji yako mmojawapo, akupayo Bwana, Mungu wako, ukae humo, ukiambiwa,
Josué 22.11-22.34 Juges 20.1-20.17
13 Kumetoka katikati yako mabaradhuli kadha wa kadha, wamewapotoa wenyeji wa mji wao, wakisema, Twendeni tukaabudu miungu mingine msiyoijua;
Deutéronome 13.2 1 Samuel 25.17 Juges 20.13 1 Jean 2.19 1 Rois 21.10
14 ndipo nawe uulize na kutafuta, ukiuliza kwa bidii; nawe angalia, ikiwa kweli, na jambo lile halina shaka, kwamba machukizo mfano wa haya yafanyika katikati yako;
Deutéronome 17.4 Jean 7.24 Nombres 35.30 Esaïe 11.3-11.4 1 Timothée 5.19
15 hakika yako uwapige wenyeji wa mji ule kwa makali ya upanga, kwa kuwaangamiza kabisa, pamoja na vitu vyote vilivyomo, na wanyama walio humo, kwa makali ya upanga.
Exode 22.20 Lévitique 27.28 Deutéronome 7.2 Apocalypse 17.16 Deutéronome 2.34
16 Na nyara zake zote uzikusanyie katikati ya njia yake; na mji uuteketeze kwa moto, na nyara zake zote, kuwe sadaka kamili ya kuteketezwa kwa Bwana, Mungu wako; nao utakuwa magofu milele; usijengwe tena.
Josué 8.28 Jérémie 49.2 Esaïe 17.1 Josué 6.24 Esaïe 25.2
17 Kisishikamane na mkono wako kitu cho chote katika kitu kilichoharimishwa; ili ageuke Bwana na ukali wa hasira zake akurehemu, akuonee huruma, na kukufanya kuwa wengi, kama alivyowaapia baba zako;
Genèse 26.24 Genèse 26.4 Genèse 28.14 Josué 7.26 Josué 6.18
18 utakaposikiza sauti ya Bwana, Mungu wako kwa kushika maagizo yake yote nikuagizayo leo, ufanye yaliyoelekea machoni pa Bwana, Mungu wako.
Deutéronome 12.28 Deutéronome 12.25 Matthieu 7.24 Matthieu 6.33 Psaumes 119.6

Cette Bible est dans le domaine public.