Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 11.16
Bible en Swahili de l’est


Promesses et menaces

1 Kwa ajili hii mpende Bwana, Mungu wako, na kushika sikuzote mausia yake, na amri zake, na hukumu zake, na maagizo yake.
Deutéronome 6.5 Deutéronome 10.12 Zacharie 3.7 Lévitique 8.35 Luc 1.74-1.75
2 Nanyi leo jueni; kwa kuwa sisemi sasa na vijana vyenu, ambao hawakujua, wala hawakuona adhabu ya Bwana, Mungu wenu, ukuu wake, na mkono wake wa nguvu, na mkono wake ulionyoka,
Deutéronome 5.24 Proverbes 22.19 Deutéronome 4.34 Deutéronome 7.19 Deutéronome 9.26
3 na ishara zake, na kazi zake alizomfanya Farao mfalme wa Misri, na nchi yake yote, katikati ya Misri;
Deutéronome 7.19 Jérémie 32.20-32.21 Psaumes 105.27-105.45 Deutéronome 4.34 Psaumes 135.9
4 na alivyolifanya jeshi la Misri, farasi zao, na magari yao; na alivyowafunikiza maji ya Bahari ya Shamu walipokuwa wakiwaandamia, na alivyowaangamiza Bwana hata hivi leo;
Psaumes 106.11 Exode 15.9-15.10 Exode 15.4 Exode 15.19 Hébreux 11.29
5 na mambo aliyowafanyia ninyi barani, hata mkaja mahali hapa;
Psaumes 78.14-78.72 Psaumes 105.39-105.41 Psaumes 106.12-106.48 Psaumes 77.20
6 na alivyowafanya Dathani, na Abiramu, wana wa Eliabu mwana wa Reubeni; nchi ilivyofunua kinywa chake, ikawameza, na walio nyumbani mwao, na mahema yao, na kila kitu kilichokuwa hai kikiwafuata, katikati ya Israeli yote;
Psaumes 106.17 Nombres 26.9-26.10 Nombres 27.3 Nombres 16.1-16.35
7 lakini macho yenu yameiona kazi kubwa ya Bwana aliyoifanya, yote.
Deutéronome 5.3 Deutéronome 7.19 Psaumes 145.12 Psaumes 150.2 Psaumes 106.2
8 Kwa hiyo yaangalieni maagizo yote niwaagizayo leo, mpate kuwa na nguvu, na kuingia mkaimiliki nchi mwivukiayo kuimiliki;
Josué 1.6-1.7 Deutéronome 31.23 Deutéronome 26.16-26.19 Colossiens 1.11 Daniel 10.19
9 nanyi mpate kuzifanya siku zenu kuwa nyingi juu ya nchi Bwana aliyowaapia baba zenu, ya kuwa atawapa wao na kizazi chao, nchi imiminikayo maziwa na asali
Deutéronome 4.40 Exode 3.8 Proverbes 10.27 Deutéronome 9.5 Deutéronome 6.2
10 Kwa kuwa nchi mwingiayo kuimiliki, si mfano wa nchi ya Misri mlikotoka, uliyokuwa ukipanda mbegu zako humo na kuinywesheleza kwa mguu wako, kama shamba la mboga;
Zacharie 14.18
11 lakini nchi mwivukiayo kuimiliki ni nchi ya vilima na mabonde, nayo hunyweshwa maji ya mvua ya mbinguni;
Psaumes 65.12-65.13 Esaïe 28.1 Hébreux 6.7 Deutéronome 8.7-8.9 Jérémie 2.7
12 nayo ni nchi itunzwayo na Bwana, Mungu wako; macho ya Bwana Mungu wako, ya juu yake, tangu mwanzo wa mwaka hata mwisho wa mwaka.
1 Rois 9.3 Jérémie 24.6 Psaumes 34.15 Psaumes 33.18 Esdras 5.5
13 Tena itakuwa, mtakaposikiza kwa bidii maagizo yangu niwaagizayo leo, kwa kumpenda Bwana, Mungu wenu, na kumtumikia kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote,
Deutéronome 6.17 Deutéronome 10.12 Deutéronome 4.29 Deutéronome 11.22 Psaumes 119.4
14 ndipo nitakapowapa mvua ya nchi yenu kwa wakati wake, mvua ya masika, na mvua ya vuli, upate kuvuna nafaka yako, na divai yako, na mafuta yako.
Jacques 5.7 Lévitique 26.4 Deutéronome 28.12 Joël 2.22-2.23 Job 5.10-5.11
15 Nami nitakupa nyasi katika mavue yako kulisha wanyama wako wa mifugo, nawe utakula na kushiba.
Deutéronome 6.11 Psaumes 104.14 Joël 2.19 Malachie 3.10-3.11 Joël 1.18
16 Jitunzeni nafsi zenu, mioyo yenu isije ikadanganywa, mkageuka na kutumikia miungu mingine na kuiabudu;
Job 31.27 Deutéronome 29.18 Deutéronome 8.19 Hébreux 2.1 Hébreux 3.12
17 hasira za Bwana zikawaka juu yenu, naye akafunga mbingu kusiwe na mvua, wala nchi isitoe matunda yake; mkaangamia kwa upesi mtoke katika nchi nzuri awapayo Bwana.
1 Rois 8.35 Deutéronome 6.15 2 Chroniques 6.26 Deutéronome 4.26 2 Chroniques 7.13
18 Kwa hiyo yawekeni maneno yangu mioyoni mwenu na rohoni mwenu; yafungeni yawe dalili juu ya mikono yenu, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yenu.
2 Pierre 1.12 2 Pierre 3.1-3.2 Proverbes 6.20-6.23 Psaumes 119.11 Exode 13.9
19 Nayo wafunzeni vijana vyenu kwa kuyazungumza uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo.
Deutéronome 6.7 Esaïe 38.19 Proverbes 2.1 Deutéronome 4.9-4.10 Psaumes 34.11
20 Tena yaandike juu ya miimo ya nyumba yako, na juu ya malango yako;
Deutéronome 6.9
21 ili siku zenu zifanywe nyingi, na za vijana vyenu nao, juu ya nchi Bwana aliyowaapia baba zenu kuwa atawapa, kama zilivyo siku za mbingu juu ya nchi.
Psaumes 72.5 Proverbes 4.10 Proverbes 3.2 Deutéronome 4.40 Proverbes 9.11
22 Kwa kuwa kwamba mtayashika kwa bidii maagizo haya yote niwaagizayo, kuyafanya; kumpenda Bwana, Mungu wenu, na kutembea katika njia zake zote, na kushikamana naye;
Deutéronome 10.20 Deutéronome 6.17 Deutéronome 11.13 Genèse 2.24 Actes 11.23
23 ndipo Bwana atakapowafukuza mataifa haya yote mbele yenu, nanyi mtamiliki mataifa makubwa yenye nguvu kuwapita ninyi.
Deutéronome 4.38 Deutéronome 9.1 Exode 34.11 Exode 23.27-23.30 Deutéronome 7.22-7.23
24 Kila mahali mtakapokanyaga kwa nyayo za miguu yenu patakuwa penu; tokea hilo jangwa, na Lebanoni, na tokea mto wa Frati, mpaka bahari ya magharibi, itakuwa ndiyo mipaka yenu.
Josué 14.9 Exode 23.31 Josué 1.3-1.4 Genèse 15.18-15.21 1 Rois 4.21
25 Hapatakuwa na mtu atakayeweza kusimama mbele yenu; Bwana, Mungu wenu, ataweka utisho wenu na kuhofiwa kwenu juu ya nchi yote mtakayoikanyaga, kama alivyowaambia.
Exode 23.27 Deutéronome 7.24 Deutéronome 2.25 Josué 5.1 Josué 1.5
26 Angalieni, nawawekea mbele yenu hivi leo baraka na laana;
Deutéronome 30.1 Galates 3.10 Deutéronome 30.15-30.20 Galates 3.13-3.14
27 baraka ni hapo mtakapoyasikiza maagizo ya Bwana, Mungu wenu, niwaagizayo leo;
Deutéronome 28.1-28.14 Esaïe 1.19 Romains 2.7 Jean 14.21-14.23 Lévitique 26.3-26.13
28 na laana ni hapo msiposikiza maagizo ya Bwana, Mungu wenu, mkikengeuka katika njia niwaagizayo leo, kwa kuandama miungu mingine msiyoijua.
Deutéronome 28.15-28.68 Esaïe 1.20 Lévitique 26.14-26.32 Matthieu 25.41 Romains 2.8-2.9
29 Tena itakuwa, atakapokuleta Bwana, Mungu wako, na kukutia katika nchi uendeayo kuimiliki, ndipo uiweke baraka juu ya mlima wa Gerizimu, na laana uiweke juu ya mlima wa Ebali.
Josué 8.30-8.35 Deutéronome 27.12-27.26
30 Je! Haiwi ng’ambo ya Yordani? Nyuma ya njia ya machweo ya jua, katika nchi ya Wakanaani waketio katika Araba kuelekea Gilgali, kando ya hiyo mialoni ya More?
Genèse 12.6 Juges 7.1 Josué 5.9 Josué 4.19
31 Kwani ninyi mtavuka Yordani mwingie kuimiliki nchi awapayo Bwana, Mungu wenu, nanyi muimiliki na kuketi humo.
Josué 1.11 Deutéronome 9.1 Josué 3.13-3.17
32 Nanyi angalieni mzifanye amri na hukumu zote niwawekeazo leo mbele yenu.
Deutéronome 12.32 1 Thessaloniciens 4.1-4.2 Deutéronome 5.32-5.33 Psaumes 119.6 Luc 1.6

Cette Bible est dans le domaine public.