Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Corinthiens 3.10
Bible en Swahili de l’est


1 Je! Tunaanza tena kujisifu wenyewe? Au tunahitaji, kama wengine, barua zenye sifa kuja kwenu, au kutoka kwenu?
2 Corinthiens 12.11 Actes 18.27 2 Corinthiens 5.12 1 Corinthiens 16.3 2 Corinthiens 10.12
2 Ninyi ndinyi barua yetu, iliyoandikwa mioyoni mwetu, inajulikana na kusomwa na watu wote;
Romains 1.8 1 Corinthiens 9.1-9.2 1 Thessaloniciens 1.8 Philippiens 1.7 2 Corinthiens 11.11
3 mnadhihirishwa kwamba mmekuwa barua ya Kristo tuliyoikatibu, iliyoandikwa si kwa wino, bali kwa Roho wa Mungu aliye hai; si katika vibao vya mawe, ila katika vibao ambavyo ni mioyo ya nyama.
Ezéchiel 11.19 Jérémie 31.33 Hébreux 8.10 Exode 24.12 Proverbes 3.3
4 Na tumaini hilo tunalo mbele za Mungu kwa njia ya Kristo.
Ephésiens 3.12 1 Thessaloniciens 1.8 Exode 18.19 2 Corinthiens 2.14 Philippiens 1.6
5 Si kwamba twatosha sisi wenyewe kufikiri neno lo lote kwamba ni letu wenyewe, bali utoshelevu wetu watoka kwa Mungu.
1 Corinthiens 15.10 Philippiens 4.13 2 Corinthiens 12.9 Jean 15.5 Jacques 1.17
6 Naye ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya; si wa andiko, bali wa roho; kwa maana andiko huua, bali roho huhuisha.
Jérémie 31.31 Jean 6.63 Romains 7.6 Luc 22.20 1 Corinthiens 11.25
7 Basi, ikiwa huduma ya mauti, iliyoandikwa na kuchorwa katika mawe, ilikuja katika utukufu, hata Waisraeli hawakuweza kuukazia macho uso wa Musa, kwa sababu ya utukufu wa uso wake; nao ni utukufu uliokuwa ukibatilika;
Exode 24.12 1 Corinthiens 13.10 Romains 7.10 2 Corinthiens 3.6 2 Corinthiens 3.9-3.11
8 je! Huduma ya roho haitazidi kuwa katika utukufu?
Jude 1.19-1.20 Jean 7.39 Esaïe 59.21 2 Thessaloniciens 2.13 2 Corinthiens 3.17
9 Kwa maana ikiwa huduma ya adhabu ina utukufu, siuze huduma ya haki ina utukufu unaozidi.
Hébreux 12.18-12.21 Romains 3.21-3.22 Galates 3.10 Romains 1.17-1.18 Romains 5.15-5.21
10 Maana hata ile iliyotukuzwa haikuwa na utukufu hivi, kwa sababu ya utukufu uzidio sana.
Job 25.5 Esaïe 24.23 Apocalypse 21.23-21.24 Philippiens 3.7-3.8 Actes 26.13
11 Kwa maana, ikiwa ile inayobatilika ilikuwa na utukufu, zaidi sana ile ikaayo ina utukufu.
Hébreux 8.13 Hébreux 7.21-7.25 2 Corinthiens 3.6-3.7 Romains 5.20-5.21 2 Corinthiens 4.1
12 Basi, kwa kuwa mna taraja la namna hii, twatumia ujasiri mwingi;
2 Corinthiens 7.4 Actes 4.13 1 Thessaloniciens 2.2 Actes 9.27 Actes 4.29-4.31
13 nasi si kama Musa alivyotia utaji juu ya uso wake, ili kwamba Waisraeli wasitazame sana mwisho wa ile iliyokuwa ikibatilika;
Exode 34.33-34.35 2 Corinthiens 3.7 Colossiens 2.17 Ephésiens 2.14-2.15 Hébreux 10.1-10.9
14 ila fikira zao zilitiwa uzito. Kwa maana hata leo hivi, wakati lisomwapo Agano la Kale, utaji uo huo wakaa; yaani, haikufunuliwa kwamba huondolewa katika Kristo;
2 Corinthiens 4.3-4.4 Actes 26.18 Romains 11.25 Actes 16.14 2 Corinthiens 4.6
15 ila hata leo, torati ya Musa isomwapo, utaji huikalia mioyo yao.
Actes 13.27-13.29
16 Lakini wakati wo wote watakapomgeukia Bwana, ule utaji huondolewa.
Exode 34.34 Esaïe 25.7 Esaïe 29.18 Osée 3.4-3.5 Lamentations 3.40
17 Basi (Bwana) ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru.
Romains 8.2 Galates 4.6 Jean 8.32 Galates 5.13 2 Timothée 1.7
18 Lakini sisi sote, kwa uso usiotiwa utaji, tukiurudisha utukufu wa Bwana, kama vile katika kioo, tunabadilishwa tufanane na mfano uo huo, toka utukufu hata utukufu, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho.
2 Corinthiens 4.6 Ephésiens 4.22-4.24 2 Corinthiens 4.4 Romains 12.2 Romains 8.29

Cette Bible est dans le domaine public.