Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Corinthiens 13.10
Bible en Swahili de l’est


1 Hii ndiyo mara ya tatu ya mimi kuja kwenu. Kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno litathibitishwa.
Deutéronome 19.15 2 Corinthiens 12.14 Matthieu 18.16 Nombres 35.30 Deutéronome 17.6
2 Nimetangulia kuwaambia; na, kama vile nilipokuwapo mara ya pili, vivyo hivyo sasa nisipokuwapo, nawaambia wazi wao waliotenda dhambi tangu hapo, na wengine wote, ya kwamba, nikija, sitahurumia;
2 Corinthiens 1.23 2 Corinthiens 10.8-10.11 1 Corinthiens 4.19-4.21 2 Corinthiens 10.1-10.2 2 Corinthiens 13.10
3 kwa kuwa mnatafuta dalili ya Kristo, asemaye ndani yangu, ambaye si dhaifu kwenu, bali ana uweza ndani yenu.
Matthieu 10.20 2 Corinthiens 12.12 1 Corinthiens 5.4-5.5 2 Corinthiens 2.6 Matthieu 18.18-18.20
4 Maana, alisulibiwa katika udhaifu, lakini anaishi kwa nguvu za Mungu. Maana sisi nasi tu dhaifu katika yeye; lakini tutaishi pamoja naye kwa uweza wa Mungu ulio kwenu.
1 Pierre 3.18 Romains 6.4 1 Corinthiens 2.3 Romains 1.4 Philippiens 3.10
5 Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa.
1 Corinthiens 11.28 Lamentations 3.40 1 Corinthiens 9.27 Hébreux 12.15 Galates 6.4
6 Lakini natumaini kama mtajua ya kuwa sisi hatukukataliwa.
2 Corinthiens 12.20 2 Corinthiens 13.3-13.4 2 Corinthiens 13.10
7 Nasi twamwomba Mungu, msifanye lo lote lililo baya; si kwamba sisi tuonekane tumekubaliwa, lakini ninyi mfanye lile lililo jema, tujapokuwa sisi tu kama waliokataliwa.
2 Timothée 2.15 2 Timothée 4.18 Philippiens 1.9-1.11 1 Thessaloniciens 5.23 Philippiens 4.8
8 Maana hatuwezi kutenda neno lo lote kinyume cha kweli, bali kwa ajili ya kweli.
Actes 13.3-13.12 Actes 5.1-5.11 2 Rois 1.9-1.13 Proverbes 21.30 2 Corinthiens 10.8
9 Maana twafurahi, iwapo sisi tu dhaifu, nanyi mmekuwa hodari. Tena twaomba hili nalo, kutimilika kwenu.
2 Corinthiens 13.11 1 Thessaloniciens 3.10 1 Corinthiens 4.10 2 Corinthiens 13.7-13.8 2 Corinthiens 7.1
10 Kwa sababu hiyo, naandika haya nisipokuwapo, ili, nikiwapo, nisiutumie ukali kwa kadiri ya uwezo ule niliopewa na Bwana, kwa kujenga wala si kwa kubomoa.
2 Corinthiens 10.8 Tite 1.13 2 Corinthiens 2.3 2 Corinthiens 13.8 2 Corinthiens 13.2
11 Hatimaye, ndugu, kwaherini; mtimilike, mfarijike, nieni mamoja, mkae katika amani; na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.
Romains 15.33 Marc 9.50 Romains 12.16 Romains 12.18 1 Corinthiens 1.10
12 Salimianeni kwa busu takatifu.
Romains 16.16 1 Pierre 5.14 1 Corinthiens 16.20 1 Thessaloniciens 5.26
13 Watakatifu wote wawasalimu.
Philémon 1.23-1.24 Hébreux 13.24 3 Jean 1.14 Romains 16.16 Philippiens 4.21-4.22
14 Neema ya Bwana Yesu Kristo, na pendo la Mungu, na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote.
Romains 16.20 Romains 5.5 Jude 1.21 Philippiens 2.1 Romains 1.7

Cette Bible est dans le domaine public.