Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Corinthiens 5.12
Bible en Swahili de l’est


Désordres sexuels et moraux dans l’Église

1 Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye.
Lévitique 18.8 Apocalypse 21.8 Deutéronome 22.30 Galates 5.19 Actes 15.20
2 Nanyi mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo aliyetenda jambo hilo.
1 Corinthiens 5.13 2 Corinthiens 7.7-7.11 Jérémie 13.17 1 Corinthiens 5.5-5.7 Nombres 25.6
3 Kwa maana kweli, nisipokuwapo kwa mwili, lakini nikiwapo kwa roho, mimi mwenyewe nimekwisha kumhukumu yeye aliyetenda jambo hilo, kana kwamba nikiwapo.
Colossiens 2.5 1 Thessaloniciens 2.17 2 Corinthiens 10.11 2 Corinthiens 10.1 2 Corinthiens 13.2
4 Katika jina la Bwana wetu Yesu, ninyi mkiwa mmekusanyika pamoja na roho yangu, pamoja na uweza wa Bwana wetu Yesu;
Jean 20.23 2 Corinthiens 13.10 2 Corinthiens 13.3 Matthieu 16.19 2 Thessaloniciens 3.6
5 kumtolea Shetani mtu huyo, ili mwili uadhibiwe, ili na roho iokolewe katika siku ya Bwana Yesu.
1 Timothée 1.20 1 Corinthiens 11.32 Job 2.6 1 Corinthiens 1.8 Galates 6.1-6.2
6 Kujisifu kwenu si kuzuri. Hamjui kwamba chachu kidogo hulichachusha donge zima?
Galates 5.9 Jacques 4.16 1 Corinthiens 5.2 1 Corinthiens 15.33 1 Corinthiens 3.21
7 Basi, jisafisheni, mkatoe ile chachu ya kale, mpate kuwa donge jipya, kama vile mlivyo hamkutiwa chachu. Kwa maana Pasaka wetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani, Kristo;
1 Corinthiens 10.17 Jean 19.14 Actes 8.32-8.35 Exode 12.5-12.6 Exode 12.15
8 basi na tuifanye karamu, si kwa chachu ya kale, wala kwa chachu ya uovu na ubaya, bali kwa yasiyochachika, ndio weupe wa moyo na kweli.
Deutéronome 16.3 Exode 12.15 Matthieu 16.6 Marc 8.15 Luc 12.1
9 Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane na wazinzi.
Ephésiens 5.11 2 Thessaloniciens 3.14 2 Thessaloniciens 3.6 2 Corinthiens 6.14 2 Corinthiens 6.17
10 Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang’anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia.
1 Corinthiens 10.27 Jean 17.15-17.16 Matthieu 5.14-5.16 2 Corinthiens 4.4 Jean 8.23
11 Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.
2 Thessaloniciens 3.6 2 Thessaloniciens 3.14 Romains 16.17 Matthieu 18.17 2 Jean 1.10
12 Maana yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani?
Marc 4.11 Colossiens 4.5 1 Corinthiens 6.1-6.5 1 Corinthiens 5.3-5.5 1 Thessaloniciens 4.12
13 Lakini hao walio nje Mungu atawahukumu. Ninyi mwondoeni yule mbaya miongoni mwenu.
Deutéronome 13.5 Deutéronome 17.7 Deutéronome 21.21 Deutéronome 22.24 Deutéronome 17.12

Cette Bible est dans le domaine public.