Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 21.20
Bible en Swahili de l’est


La pêche miraculeuse

1 Baada ya hayo Yesu alijidhihirisha tena kwa wanafunzi wake, penye bahari ya Tiberia, naye alijidhihirisha hivi.
Jean 6.1 Matthieu 26.32 Marc 16.12 Jean 6.23 Matthieu 28.7
2 Simoni Petro, na Tomaso aitwaye Pacha, na Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, na wana wa Zebedayo, na wengine wawili wa wanafunzi wake, walikuwapo pamoja.
Jean 4.46 Jean 11.16 Jean 1.45-2.1 Luc 5.10 Josué 19.28
3 Simoni Petro aliwaambia, Naenda kuvua samaki. Nao wakamwambia, Sisi nasi tutakwenda nawe. Basi wakaondoka, wakapanda chomboni; ila usiku ule hawakupata kitu.
Luc 5.5 2 Thessaloniciens 3.7-3.9 Matthieu 4.18-4.20 Luc 5.10-5.11 Actes 20.34
4 Hata asubuhi kulipokucha, Yesu alisimama ufuoni; walakini wanafunzi hawakujua ya kuwa ni Yesu.
Jean 20.14 Luc 24.15-24.16 Luc 24.31 Marc 16.12
5 Basi Yesu akawaambia, Wanangu, mna kitoweo? Wakamjibu, La.
Philippiens 4.19 Psaumes 37.3 Philippiens 4.11-4.13 1 Jean 2.13 Luc 24.41-24.43
6 Akawaambia, Litupeni jarife upande wa kuume wa chombo, nanyi mtapata. Basi wakatupa; wala sasa hawakuweza kulivuta tena kwa sababu ya wingi wa samaki.
Luc 5.4-5.7 Actes 2.41 Jean 2.5 Actes 4.4 Hébreux 2.6-2.9
7 Basi yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akamwambia Petro, Ndiye Bwana. Naye Simoni Petro, aliposikia ya kwamba ni Bwana, akajifunga vazi lake, (maana alikuwa uchi), akajitupa baharini.
Jean 13.23 Jean 19.26 Jean 21.20 Psaumes 118.23 Jean 20.2
8 Na hao wanafunzi wengine wakaja katika mashua; maana hawakuwa mbali na nchi kavu; ila yapata dhiraa mia mbili; huku wakilikokota lile jarife lenye samaki.
Deutéronome 3.11
9 Basi waliposhuka pwani, wakaona huko moto wa makaa, na juu yake pametiwa samaki, na mkate.
Marc 8.3 Jean 18.18 1 Rois 19.5-19.6 Jean 21.10 Jean 21.13
10 Yesu akawaambia, Leteni hapa baadhi ya samaki mliowavua sasa hivi.
11 Basi Simoni Petro akapanda chomboni, akalivuta jarife pwani, limejaa samaki wakubwa, mia hamsini na watatu; na ijapokuwa ni wengi namna hiyo, jarife halikupasuka.
Actes 2.41 Luc 5.6-5.8
12 Yesu akawaambia, Njoni mfungue kinywa. Wala hakuna mtu katika wale wanafunzi aliyethubutu kumwuliza, U nani wewe? Wakijua ya kuwa ni Bwana.
Actes 10.41 Jean 4.27 Luc 9.45 Marc 9.32 Jean 16.19
13 Yesu akaenda akautwaa mkate, akawapa, na samaki vivyo hivyo.
Jean 21.9 Actes 10.41 Luc 24.42-24.43
14 Hiyo ndiyo mara ya tatu ya Yesu kuonekana na wanafunzi wake baada ya kufufuka katika wafu.
Jean 20.19 Jean 20.26
15 Basi walipokwisha kula, Yesu akamwambia Simoni Petro, Je! Simoni wa Yohana, wewe wanipenda kuliko hawa? Akamwambia , Naam ,Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Lisha wana-kondoo wangu.
Esaïe 40.11 1 Jean 4.19 Galates 5.6 1 Timothée 4.15-4.16 2 Corinthiens 5.14-5.15
16 Akamwambia tena mara ya pili, Simoni wa Yohana, wanipenda? Akamwambia, Ndiyo, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Chunga kondoo zangu.
Actes 20.28 1 Pierre 5.2 Jean 18.17 Hébreux 13.20 Matthieu 2.6
17 Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo zangu.
Jean 16.30 Jean 13.38 Marc 14.72 Jean 21.15-21.16 Apocalypse 2.23
18 Akasema, Amin, amin, nakuambia, Wakati ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini utakapokuwa mzee, utainyosha mikono yako, na mwingine atakufunga na kukuchukua usikotaka.
Jean 13.36 Actes 12.3-12.4 Actes 21.11 Jean 12.27-12.28 2 Corinthiens 5.4
19 Akasema neno hilo kwa kuonyesha ni kwa mauti gani atakayomtukuza Mungu. Naye akiisha kusema hayo akamwambia, Nifuate.
2 Pierre 1.14 Jean 21.22 Philippiens 1.20 Matthieu 19.28 Jean 12.26
20 Petro akageuka akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu anafuata; (ndiye huyo aliyeegama kifuani pake wakati wa kula chakula cha jioni, akasema, Bwana, ni nani akusalitiye?)
Jean 21.7 Jean 20.2 Jean 21.24 Jean 13.23-13.26
21 Basi Petro akamwona huyo, akamwambia Yesu, Bwana, na huyu je?
Actes 1.6-1.7 Matthieu 24.3-24.4 Luc 13.23-13.24
22 Yesu akamwambia, Ikiwa nataka huyu akae hata nijapo, imekupasaje wewe? Wewe unifuate mimi.
1 Corinthiens 4.5 Apocalypse 2.25 Marc 9.1 Jean 21.19 1 Corinthiens 11.26
23 Basi neno hilo lilienea katikati ya ndugu ya kwamba mwanafunzi yule hafi. Walakini Yesu hakumwambia ya kwamba hafi; bali, Ikiwa nataka huyu akae hata nijapo, imekupasaje wewe?
Job 28.28 Actes 1.15 Daniel 4.35 Deutéronome 29.29 Job 33.13
24 Huyu ndiye yule mwanafunzi ayashuhudiaye haya, na aliyeyaandika haya: nasi twajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
Jean 19.35 3 Jean 1.12 Jean 15.27 1 Jean 5.6 1 Jean 1.1-1.2
25 Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa.
Psaumes 40.5 Psaumes 71.15 Jean 20.30-20.31 Actes 10.38 Hébreux 11.32

Cette Bible est dans le domaine public.