Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 17.14
Bible en Swahili de l’est


La prière sacerdotale

1 Maneno hayo aliyasema Yesu; akainua macho yake kuelekea mbinguni, akasema, Baba, saa imekwisha kufika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe;
Jean 13.31-13.32 Philippiens 2.9-2.11 Actes 3.13 Jean 7.39 Jean 12.23
2 kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele.
Jean 6.37 Jean 6.39 Jean 17.24 Daniel 7.14 Jean 10.28-10.29
3 Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.
1 Jean 5.20 1 Jean 5.11-5.12 Jean 3.17 Jean 17.25 Jean 3.34
4 Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.
Jean 4.34 Jean 13.31-13.32 Jean 19.30 Jean 14.13 Actes 20.24
5 Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.
Jean 1.1-1.3 Philippiens 2.6 Jean 17.24 Hébreux 1.3 Jean 1.18
6 Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika.
Jean 17.26 Jean 17.2 Jean 6.37 Psaumes 22.22 1 Jean 5.20
7 Sasa wamejua ya kuwa yote uliyonipa yatoka kwako.
Jean 17.10 Jean 8.28 Jean 10.29-10.30 Jean 14.20 Jean 16.15
8 Kwa kuwa maneno uliyonipa nimewapa wao; nao wakayapokea, wakajua hakika ya kuwa nalitoka kwako, wakasadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
Jean 16.30 Jean 17.14 Jean 16.27 Jean 6.68 1 Thessaloniciens 2.13
9 Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako;
Luc 22.32 Jean 14.16 Jean 17.6 Hébreux 9.24 1 Jean 2.1-2.2
10 na wote walio wangu ni wako, na walio wako ni wangu; nami nimetukuzwa ndani yao.
2 Thessaloniciens 1.10 1 Pierre 2.9 2 Thessaloniciens 1.12 Jean 11.4 Jean 16.14-16.15
11 Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo.
Jean 17.21-17.22 Jean 13.1 Ephésiens 4.4 Jean 17.25 Jean 17.12-17.18
12 Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.
Jean 18.9 Jean 13.18 Jean 6.37 Jean 6.39-6.40 Jean 10.27-10.28
13 Na sasa naja kwako; na maneno haya nayasema ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu imetimizwa ndani yao.
Jean 15.11 Jean 3.29 Jean 16.22-16.24 Jean 13.3 Actes 13.52
14 Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umewachukia; kwa kuwa wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.
Jean 15.18-15.21 1 Jean 5.19-5.20 Jean 8.23 Jean 17.16 1 Jean 4.5-4.6
15 Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu.
Psaumes 121.7 Luc 11.4 1 Chroniques 4.10 Galates 1.4 Philippiens 1.20-1.26
16 Wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.
Jean 17.14
17 Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli.
Jean 15.3 Psaumes 119.160 Ephésiens 5.26 1 Pierre 1.22-1.23 Jean 17.19
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami vivyo hivyo naliwatuma hao ulimwenguni.
Jean 20.21 2 Corinthiens 5.20 Jean 17.23 Jean 17.3 Jean 17.21
19 Na kwa ajili yao najiweka wakfu mwenyewe, ili na hao watakaswe katika kweli.
Hébreux 2.11 Tite 2.14 Hébreux 10.5-10.10 1 Corinthiens 1.2 Jean 10.36
20 Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao.
Actes 2.41 Ephésiens 4.11 2 Timothée 1.2 Jean 17.6-17.11 Romains 16.26
21 Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
Philippiens 1.27 Jean 17.11 Colossiens 3.11-3.14 Jean 10.38 Jean 17.22-17.23
22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.
1 Jean 1.3 2 Corinthiens 3.18 Jean 1.14 Jean 14.20 Marc 6.7
23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi.
1 Jean 3.1 Jean 17.21 Jean 16.27 Jean 17.26 Colossiens 3.14
24 Baba, hao ulionipa nataka wawe pamoja nami po pote nilipo, wapate na kuutazama utukufu wangu ulionipa; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu.
Jean 12.26 Jean 17.5 2 Corinthiens 3.18 Jean 1.14 1 Jean 3.2
25 Baba mwenye haki, ulimwengu haukukujua; lakini mimi nalikujua, na hao wamejua ya kuwa ndiwe uliyenituma.
Jean 7.29 Jean 15.21 Jean 17.11 Jean 17.8 Jean 10.15
26 Nami naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo; ili pendo lile ulilonipenda mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao.
Jean 17.6 Jean 17.23 Jean 15.9 Jean 14.23 Jean 15.15

Cette Bible est dans le domaine public.