Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 17.1
Bible en Swahili de l’est


La prière sacerdotale

1 Maneno hayo aliyasema Yesu; akainua macho yake kuelekea mbinguni, akasema, Baba, saa imekwisha kufika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe;
Jean 13.31-13.32 Philippiens 2.9-2.11 Jean 12.23 Jean 11.41 Actes 3.13
2 kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele.
Jean 6.39 Jean 6.37 Jean 17.24 Daniel 7.14 Psaumes 2.6-2.12
3 Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.
1 Jean 5.20 1 Jean 5.11-5.12 Jean 17.25 Jean 3.17 Jean 3.34
4 Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.
Jean 4.34 Jean 19.30 Jean 13.31-13.32 2 Timothée 4.7 Jean 14.13
5 Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.
Jean 1.1-1.3 Jean 17.24 Philippiens 2.6 Jean 10.30 Hébreux 1.3
6 Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika.
Jean 17.26 Jean 17.2 Jean 6.37 Exode 34.5-34.7 Psaumes 22.22
7 Sasa wamejua ya kuwa yote uliyonipa yatoka kwako.
Jean 16.15 Jean 12.49-12.50 Jean 7.16-7.17 Jean 14.7-14.10 Jean 16.27-16.30
8 Kwa kuwa maneno uliyonipa nimewapa wao; nao wakayapokea, wakajua hakika ya kuwa nalitoka kwako, wakasadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
Jean 17.14 Jean 16.27 Jean 16.30 Jean 17.21 Jean 6.68
9 Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako;
Luc 22.32 Jean 17.6 Jean 14.16 Jean 17.20 1 Jean 5.19
10 na wote walio wangu ni wako, na walio wako ni wangu; nami nimetukuzwa ndani yao.
2 Thessaloniciens 1.10 1 Pierre 2.9 2 Thessaloniciens 1.12 Jean 10.30 Colossiens 2.9
11 Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo.
Jean 17.21-17.22 Jean 13.1 Ephésiens 4.4 Jean 17.25 Jude 1.1
12 Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.
Jean 18.9 Jean 6.37 Jean 13.18 Psaumes 109.6-109.19 Jean 6.39-6.40
13 Na sasa naja kwako; na maneno haya nayasema ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu imetimizwa ndani yao.
Jean 15.11 Jean 3.29 Jean 16.22-16.24 Psaumes 43.4 Néhémie 8.10
14 Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umewachukia; kwa kuwa wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.
Jean 15.18-15.21 1 Jean 5.19-5.20 Jean 8.23 Jean 17.16 1 Jean 4.5-4.6
15 Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu.
Psaumes 121.7 Luc 11.4 1 Chroniques 4.10 Galates 1.4 Philippiens 1.20-1.26
16 Wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.
Jean 17.14
17 Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli.
Jean 15.3 Psaumes 119.160 1 Pierre 1.22-1.23 Ephésiens 5.26 2 Thessaloniciens 2.13
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami vivyo hivyo naliwatuma hao ulimwenguni.
Jean 20.21 Jean 17.21 Jean 17.25 Jean 17.8 Esaïe 61.1-61.3
19 Na kwa ajili yao najiweka wakfu mwenyewe, ili na hao watakaswe katika kweli.
Hébreux 2.11 Hébreux 10.5-10.10 1 Corinthiens 1.2 Jean 10.36 Tite 2.14
20 Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao.
Actes 2.41 Jean 17.6-17.11 Romains 16.26 Actes 4.4 Romains 15.18-15.19
21 Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
Philippiens 1.27 Jean 17.11 Jean 17.22-17.23 1 Corinthiens 12.12 Colossiens 3.11-3.14
22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.
Jean 14.20 1 Jean 1.3 2 Corinthiens 3.18 Jean 1.14 1 Jean 3.24
23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi.
1 Jean 3.1 Jean 17.21 Jean 16.27 Jean 17.26 Colossiens 3.14
24 Baba, hao ulionipa nataka wawe pamoja nami po pote nilipo, wapate na kuutazama utukufu wangu ulionipa; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu.
Jean 12.26 Jean 17.5 2 Corinthiens 3.18 Jean 1.14 1 Jean 3.2
25 Baba mwenye haki, ulimwengu haukukujua; lakini mimi nalikujua, na hao wamejua ya kuwa ndiwe uliyenituma.
Jean 17.11 Jean 17.8 Jean 7.29 Jean 15.21 Jean 16.27
26 Nami naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo; ili pendo lile ulilonipenda mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao.
Jean 15.9 Jean 17.6 Jean 17.23 Jean 8.50 Jean 14.20

Cette Bible est dans le domaine public.