Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Zacharie 11.9
Bible en Swahili de l’est


1 Ifungue milango yako, Ee Lebanoni, Ili moto uiteketeze mierezi yako.
Jérémie 22.6-22.7 Jérémie 22.23 Luc 21.23-21.24 Zacharie 14.1-14.2 Matthieu 24.1-24.2
2 Piga yowe, msunobari, maana mwerezi umeanguka, Kwa sababu miti iliyo mizuri imeharibika; Pigeni yowe, enyi mialoni ya Bashani, Kwa maana msitu wenye nguvu umeangamia.
Ezéchiel 31.17 Luc 23.31 Esaïe 2.12-2.17 Ezéchiel 20.46 Nahum 3.8-3.19
3 Sauti ya wachungaji, ya uchungu mwingi! Kwa maana utukufu wao umeharibika; Sauti ya ngurumo ya wana-simba! Kwa maana kiburi cha Yordani kimeharibika.
Jérémie 50.44 Jérémie 25.34-25.36 Matthieu 3.7-3.10 Matthieu 23.13-23.38 Sophonie 3.3
4 Bwana, Mungu wangu, alisema hivi, Lilishe kundi la machinjo,
Zacharie 11.7 Esaïe 40.9-40.11 Matthieu 15.24 Matthieu 23.37 Zacharie 14.5
5 ambalo wenye kundi hilo huwachinja, kisha hujiona kuwa hawana hatia; na hao wawauzao husema, Na ahimidiwe Bwana, kwa maana mimi ni tajiri; na wachungaji wao wenyewe hawawahurumii.
Jérémie 50.7 Osée 12.8 Matthieu 23.13 Ezéchiel 34.6 Deutéronome 29.19-29.21
6 Maana mimi sitawahurumia tena wenyeji wa nchi hii, asema Bwana; bali, tazama, nitawatia, kila mmoja wao, mikononi mwa mwenzake, na mikononi mwa mfalme; nao wataipiga hiyo nchi, wala mimi sitawaokoa mikononi mwao.
Jérémie 13.14 Michée 5.8 Esaïe 9.19-9.21 Matthieu 22.7 Psaumes 50.22
7 Basi nikalilisha kundi la machinjo, kweli kondoo waliokuwa wanyonge kabisa.
Zacharie 11.4 Zacharie 11.14 Esaïe 61.1 Ezéchiel 37.16-37.23 Esaïe 11.4
8 Nami nikawakatilia mbali wachungaji watatu katika mwezi mmoja; maana nafsi yangu ilikuwa imechoka kwa ajili yao, na nafsi zao pia walinichukia.
Esaïe 49.7 Matthieu 23.34-23.36 Osée 5.7 Jean 7.7 Jérémie 12.8
9 Ndipo nikasema, Sitawalisheni; afaye na afe; atakayekatiliwa mbali na akatiliwe mbali; nao waliosalia, kila mmoja na ale nyama ya mwili wa mwenziwe.
Jérémie 43.11 Matthieu 13.10-13.11 Jérémie 23.39 Jérémie 23.33 Jérémie 15.2-15.3
10 Nikaitwaa hiyo fimbo yangu, iitwayo Neema, nikaikata vipande viwili, ili nipate kulivunja agano langu nililolifanya na watu wa kabila zote.
Zacharie 11.7 Jérémie 14.21 Psaumes 89.39 Actes 6.13-6.14 Ezéchiel 24.21
11 Nayo ikavunjwa siku ile; na hivyo wale kondoo wanyonge walionisikiliza wakajua ya kuwa neno hili ndilo neno la Bwana.
Sophonie 3.12 Romains 11.7-11.12 Luc 24.49-24.53 Psaumes 72.12-72.14 Deutéronome 28.49-28.68
12 Nikawaambia, Mkiona vema, nipeni ujira wangu; kama sivyo, msinipe. Basi wakanipimia vipande thelathini vya fedha, kuwa ndio ujira wangu.
Matthieu 26.15 Exode 21.32 Genèse 37.28 Marc 14.10-14.11 Luc 22.3-22.6
13 Kisha Bwana akaniambia, Mtupie mfinyanzi kima kizuri, hicho nilichotiwa kima na watu hao. Basi nikavitwaa vile vipande thelathini vya fedha, nikamtupia huyo mfinyanzi ndani ya nyumba ya Bwana.
Actes 1.18-1.19 Matthieu 27.3-27.10 Actes 4.11 Esaïe 54.7-54.10 Matthieu 27.12
14 Ndipo nikaikata vipande viwili fimbo yangu ya pili, iitwayo Vifungo, ili nipate kuuvunja udugu uliokuwa kati ya Yuda na Israeli.
Esaïe 9.21 Zacharie 11.7 Jacques 3.14 Galates 5.15 Jacques 3.16
15 Bwana akaniambia, Jitwalie tena vyombo vya mchungaji mpumbavu.
Esaïe 6.10-6.12 Lamentations 2.14 Matthieu 23.17 Ezéchiel 13.3 Jérémie 2.26-2.27
16 Kwa maana, tazama, mimi nitainua katika nchi hii mchungaji, ambaye hatawaangalia waliopotea, wala hatawatafuta waliotawanyika, wala hatamganga aliyevunjika, wala hatamlisha aliye mzima; bali atakula nyama ya wanono, na kuzirarua-rarua kwato zao.
Jérémie 23.2 Ezéchiel 34.2-34.6 Matthieu 23.13-23.29 Luc 12.45-12.46 Matthieu 23.2-23.4
17 Ole wake mchungaji asiyefaa, aliachaye kundi! Upanga utakuwa juu ya mkono wake, na juu ya jicho lake la kuume; mkono wake utakuwa umekauka kabisa, na jicho lake la kuume litakuwa limepofuka.
Jérémie 23.1 Jérémie 50.35-50.37 Esaïe 42.19-42.20 Jérémie 23.32 Ezéchiel 13.3

Cette Bible est dans le domaine public.