Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Michée 4.4
Bible en Swahili de l’est


Promesse pour Jérusalem

1 Lakini itakuwa katika siku za mwisho, ya kwamba mlima wa nyumba ya Bwana utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na watu wa mataifa watauendea makundi makundi.
Esaïe 2.1-2.4 Zacharie 8.3 Jérémie 3.17 Psaumes 22.27 Ezéchiel 43.12
2 Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu mlimani kwa Bwana, na nyumbani kwa Mungu wa Yakobo; naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake; kwa maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la Bwana litatoka Yerusalemu.
Esaïe 54.13 Psaumes 25.8-25.9 Jérémie 31.6 Psaumes 25.12 Zacharie 14.8-14.9
3 Naye atafanya hukumu kati ya watu wa kabila nyingi, naye atawakemea mataifa wenye nguvu walio mbali; nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe.
Esaïe 2.4 Psaumes 110.5-110.6 Matthieu 25.31-25.32 Zacharie 9.10 Apocalypse 19.11
4 Bali wataketi kila mtu chini ya mzabibu wake, na chini ya mtini wake; wala hapana mtu atakayewatia hofu; kwa kuwa kinywa cha Bwana wa majeshi kimesema hivi.
Esaïe 1.20 1 Rois 4.25 Zacharie 3.10 Esaïe 40.5 Jérémie 23.5-23.6
5 Kwa maana mataifa yote watakwenda, kila moja kwa jina la mungu wake, na sisi tutakwenda kwa jina la Bwana, Mungu wetu, milele na milele.
Zacharie 10.12 2 Rois 17.29 Esaïe 2.5 Esaïe 26.8 Exode 3.14-3.15
6 Katika siku ile, asema Bwana, nitamkusanya yeye achechemeaye, nami nitamrudisha yeye aliyefukuzwa, na yeye niliyemtesa.
Sophonie 3.19 Psaumes 147.2 Ezéchiel 34.12-34.17 Jérémie 31.8 Esaïe 35.3-35.6
7 Nami nitamfanya yeye aliyechechemea kuwa mabaki, na yeye aliyetupwa mbali kuwa taifa lenye nguvu, na Bwana atawamiliki katika mlima Sayuni tangu sasa na hata milele.
Michée 2.12 Michée 5.7-5.8 Esaïe 24.23 Luc 1.33 Michée 7.18
8 Na wewe, Ee mnara wa kundi, kilima cha binti Sayuni, utajiliwa; naam, mamlaka ya kwanza yatakuja, ufalme wa binti Yerusalemu.
Apocalypse 22.5 Zacharie 9.10 Esaïe 10.32 Nombres 24.19 Daniel 7.18

Déportation et délivrance d’Israël

9 Sasa mbona unapiga kelele? Je! Hakuna mfalme kwako, mshauri wako amepotea, hata umeshikwa na utungu kama mwanamke wakati wa kuzaa?
Jérémie 8.19 Esaïe 13.8 Jérémie 22.23 Jérémie 4.21 Jérémie 30.6-30.7
10 Uwe na utungu, utaabike ili uzae, Ee binti Sayuni, kama mwanamke mwenye utungu; maana sasa utatoka mjini, nawe utakaa katika mashamba; utafika hata Babeli; huko ndiko utakakookolewa; huko ndiko Bwana atakakokukomboa katika mikono ya adui zako.
2 Rois 20.18 Esaïe 48.20 Osée 2.14 Esaïe 45.13 Osée 13.13
11 Na sasa mataifa mengi wamekusanyika juu yako, wasemao, Na atiwe unajisi; macho yetu na yaone shari ya Sayuni.
Abdias 1.12 Esaïe 5.25-5.30 Michée 7.10 Esaïe 8.7-8.8 Jérémie 52.4
12 Lakini wao hawayajui mawazo ya Bwana, wala hawafahamu shauri lake; kwa maana amewakusanya kama miganda sakafuni.
Esaïe 55.8 Luc 3.17 Jérémie 29.11 Romains 11.33-11.34 Joël 3.12-3.13
13 Haya, simama upure, Ee binti Sayuni; kwa maana nitafanya pembe yako kuwa chuma, na kwato zako kuwa shaba; nawe utaponda-ponda mataifa mengi, na faida yao utaiweka wakfu kwa Bwana, na mali zao kwa Bwana wa dunia yote.
Daniel 2.44 Esaïe 23.18 1 Corinthiens 16.2 2 Samuel 8.10-8.11 Zacharie 6.5

Cette Bible est dans le domaine public.