Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Michée 4.11
Bible en Swahili de l’est


Promesse pour Jérusalem

1 Lakini itakuwa katika siku za mwisho, ya kwamba mlima wa nyumba ya Bwana utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na watu wa mataifa watauendea makundi makundi.
Esaïe 2.1-2.4 Zacharie 8.3 Jérémie 3.17 Psaumes 22.27 Ezéchiel 43.12
2 Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu mlimani kwa Bwana, na nyumbani kwa Mungu wa Yakobo; naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake; kwa maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la Bwana litatoka Yerusalemu.
Psaumes 25.8-25.9 Jérémie 31.6 Esaïe 54.13 Psaumes 25.12 Zacharie 14.8-14.9
3 Naye atafanya hukumu kati ya watu wa kabila nyingi, naye atawakemea mataifa wenye nguvu walio mbali; nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe.
Esaïe 2.4 Psaumes 110.5-110.6 Matthieu 25.31-25.32 Michée 5.15 1 Samuel 2.10
4 Bali wataketi kila mtu chini ya mzabibu wake, na chini ya mtini wake; wala hapana mtu atakayewatia hofu; kwa kuwa kinywa cha Bwana wa majeshi kimesema hivi.
Esaïe 1.20 1 Rois 4.25 Zacharie 3.10 Esaïe 40.5 Ezéchiel 39.26
5 Kwa maana mataifa yote watakwenda, kila moja kwa jina la mungu wake, na sisi tutakwenda kwa jina la Bwana, Mungu wetu, milele na milele.
Zacharie 10.12 2 Rois 17.29 Esaïe 26.8 Esaïe 2.5 Psaumes 145.1-145.2
6 Katika siku ile, asema Bwana, nitamkusanya yeye achechemeaye, nami nitamrudisha yeye aliyefukuzwa, na yeye niliyemtesa.
Sophonie 3.19 Psaumes 147.2 Ezéchiel 34.12-34.17 Ezéchiel 37.21-37.22 Jean 10.16
7 Nami nitamfanya yeye aliyechechemea kuwa mabaki, na yeye aliyetupwa mbali kuwa taifa lenye nguvu, na Bwana atawamiliki katika mlima Sayuni tangu sasa na hata milele.
Michée 5.7-5.8 Esaïe 24.23 Luc 1.33 Michée 2.12 Daniel 7.14
8 Na wewe, Ee mnara wa kundi, kilima cha binti Sayuni, utajiliwa; naam, mamlaka ya kwanza yatakuja, ufalme wa binti Yerusalemu.
Zacharie 9.10 Apocalypse 22.5 Esaïe 1.26 Marc 12.1 Daniel 2.44

Déportation et délivrance d’Israël

9 Sasa mbona unapiga kelele? Je! Hakuna mfalme kwako, mshauri wako amepotea, hata umeshikwa na utungu kama mwanamke wakati wa kuzaa?
Jérémie 8.19 Esaïe 13.8 Esaïe 3.1-3.7 Jérémie 50.43 Osée 3.4
10 Uwe na utungu, utaabike ili uzae, Ee binti Sayuni, kama mwanamke mwenye utungu; maana sasa utatoka mjini, nawe utakaa katika mashamba; utafika hata Babeli; huko ndiko utakakookolewa; huko ndiko Bwana atakakokukomboa katika mikono ya adui zako.
2 Rois 20.18 Esaïe 48.20 Osée 13.13 Esaïe 52.9-52.12 Esaïe 43.14
11 Na sasa mataifa mengi wamekusanyika juu yako, wasemao, Na atiwe unajisi; macho yetu na yaone shari ya Sayuni.
Abdias 1.12 Michée 7.10 Esaïe 5.25-5.30 Lamentations 2.15-2.16 Esaïe 8.7-8.8
12 Lakini wao hawayajui mawazo ya Bwana, wala hawafahamu shauri lake; kwa maana amewakusanya kama miganda sakafuni.
Esaïe 55.8 Romains 11.33-11.34 Luc 3.17 Jérémie 29.11 Esaïe 21.10
13 Haya, simama upure, Ee binti Sayuni; kwa maana nitafanya pembe yako kuwa chuma, na kwato zako kuwa shaba; nawe utaponda-ponda mataifa mengi, na faida yao utaiweka wakfu kwa Bwana, na mali zao kwa Bwana wa dunia yote.
Esaïe 23.18 Daniel 2.44 Jérémie 51.33 Zacharie 4.14 Deutéronome 33.25

Cette Bible est dans le domaine public.