Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jonas 4.9
Bible en Swahili de l’est


Irritation de Jonas et reproches de Dieu

1 Lakini jambo hili lilimchukiza Yona sana, naye akakasirika.
Luc 15.28 Jonas 4.9 Jonas 4.4 Matthieu 20.15 Luc 7.39
2 Akamwomba Bwana, akasema, Nakuomba, Ee Bwana; sivyo hivyo nilivyosema, hapo nilipokuwa katika nchi yangu? Hii ndiyo sababu nalifanya haraka kukimbilia Tarshishi; kwa maana nalijua ya kuwa wewe u Mungu mwenye neema, umejaa huruma, si mwepesi wa hasira, u mwingi wa rehema, nawe waghairi mabaya.
Psaumes 86.15 Jonas 1.3 Psaumes 86.5 Exode 34.6-34.7 Nombres 14.18-14.19
3 Basi, sasa, Ee Bwana, nakuomba, uniondolee uhai wangu; maana ni afadhali nife mimi kuliko kuishi.
1 Rois 19.4 Ecclésiaste 7.1 Job 7.15-7.16 Job 6.8-6.9 Nombres 11.15
4 Naye Bwana akasema, Je! Unatenda vema kukasirika?
Matthieu 20.15 Jonas 4.9 Jacques 1.19-1.20 Psaumes 106.32-106.33 Michée 6.3
5 Ndipo Yona akatoka mjini, akaketi upande wa mashariki wa mji, akajifanyia kibanda huko, akakaa chini yake uvulini, hata aone mji ule utakuwaje.
1 Rois 19.9 1 Rois 19.13 Luc 19.41-19.44 Jérémie 20.9 Esaïe 57.17
6 Na Bwana Mungu aliweka tayari mtango, akaufanya ukue juu ya Yona, ili uwe kivuli juu ya kichwa chake, na kumponya katika hali yake mbaya. Basi Yona akafurahi sana kwa sababu ya ule mtango.
Luc 10.20 1 Corinthiens 7.30 Esther 5.9 Jonas 1.17 Esaïe 39.2
7 Lakini siku ya pili kulipopambazuka, Mungu akaweka tayari buu, nalo likautafuna ule mtango, ukakatika.
Joël 1.12 Psaumes 102.10 Psaumes 30.6-30.7 Psaumes 90.5-90.6 Job 1.21
8 Basi ikawa, jua lilipopanda juu, Mungu akaweka tayari upepo wa mashariki, wenye hari nyingi; jua likampiga Yona kichwani, hata akazimia, naye akajitakia kufa, akasema, Ni afadhali nife mimi kuliko kuishi.
Psaumes 121.6 Jonas 4.3 Esaïe 49.10 Ezéchiel 19.12 Psaumes 39.9
9 Mungu akamwambia Yona, Je! Unatenda vema kukasirika kwa ajili ya mtango? Naye akasema, Ndiyo, natenda vema kukasirika hata kufa.
2 Corinthiens 7.10 Job 5.2 Juges 16.16 Apocalypse 9.6 Matthieu 26.38
10 Bwana akamwambia, Wewe umeuhurumia mtango, ambao hukuufanyia kazi, wala kuuotesha; uliomea katika usiku mmoja, na kuangamia katika usiku mmoja;
11 na mimi, je! Haikunipasa kuuhurumia Ninawi, mji ule mkubwa; ambao ndani yake wamo watu zaidi ya mia na ishirini elfu, wasioweza kupambanua katika mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto; tena wamo wanyama wa kufugwa wengi sana?
Jonas 1.2 Luc 15.28-15.32 Psaumes 36.6 Matthieu 18.33 Deutéronome 1.39

Cette Bible est dans le domaine public.