Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Amos 8.13
Bible en Swahili de l’est


Vision d’une corbeille de fruits

1 Haya ndiyo aliyonionyesha Bwana MUNGU; tazama, kikapu cha matunda ya wakati wa hari.
Amos 7.1 Amos 7.4 Amos 7.7
2 Akaniambia, Amosii, unaona nini? Nikasema, Naona kikapu cha matunda ya wakati wa hari. Ndipo Bwana akaniambia, Mwisho wao umewajilia watu wangu Israeli; sitawapita tena kamwe.
Amos 7.8 Lamentations 4.18 Michée 7.1 Jérémie 1.11-1.14 Jérémie 24.1-24.3
3 Tena nyimbo za hekaluni zitakuwa vilio siku ile, asema Bwana MUNGU; mizoga itakuwa mingi; kila mahali wataitupa, wakinyamaza kimya.
Amos 6.9-6.10 Amos 5.23 Amos 8.10 Jérémie 9.21-9.22 Jérémie 22.18
4 Lisikieni hili, ninyi mnaopenda kuwameza wahitaji, na kuwakomesha maskini wa nchi,
Psaumes 14.4 Proverbes 30.14 Amos 5.11 Jérémie 28.15 Amos 7.16
5 mkisema, Mwezi mpya utaondoka lini, tupate kuuza nafaka? Na sabato nayo, tupate kuandika ngano? Mkiipunguza efa na kuiongeza shekeli, mkidanganya watu kwa mizani ya udanganyifu;
Osée 12.7 Michée 6.10-6.11 2 Rois 4.23 Néhémie 13.15-13.21 Nombres 28.11-28.15
6 tupate kuwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji kwa jozi ya viatu; na kuziuza takataka za ngano.
Amos 2.6 Amos 8.4 Joël 3.3 Néhémie 5.1-5.5 Néhémie 5.8
7 Bwana ameapa kwa fahari ya Yakobo, Hakika sitazisahau kamwe kazi zao hata mojawapo.
Amos 6.8 Osée 8.13 Osée 9.9 Psaumes 68.34 Psaumes 10.11
8 Kwa ajili ya hayo, je! Haitatetemeka nchi, na kuomboleza kila mtu akaaye ndani yake? Naam, itainuka yote pia kama huo Mto; nayo itataabika na kupwa tena kama Mto wa Misri.
Amos 9.5 Osée 4.3 Jérémie 46.8 Psaumes 18.7 Esaïe 5.25
9 Tena itakuwa siku hiyo, asema Bwana MUNGU, nitalifanya jua litue wakati wa adhuhuri, nami nitaitia nchi giza wakati wa nuru ya mchana.
Jérémie 15.9 Michée 3.6 Matthieu 24.29 Esaïe 59.9-59.10 Amos 5.8
10 Nami nitazigeuza sikukuu zenu kuwa maombolezo, na nyimbo zenu zote kuwa vilio; nami nitatia nguo za magunia katika viuno vyote, na upaa katika kila kichwa; nami nitayafanya haya kuwa kama maombolezo kwa ajili ya mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.
Jérémie 6.26 Zacharie 12.10 Jérémie 48.37 Ezéchiel 7.18 Job 20.23
11 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana MUNGU, ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Bwana.
Psaumes 74.9 1 Samuel 3.1 1 Samuel 28.6 Michée 3.6 Ezéchiel 7.26
12 Nao watatanga-tanga toka bahari hata bahari; na toka upande wa kaskazi hata upande wa mashariki; watapiga mbio, wakienda huko na huko, kulitafuta neno la Bwana, wasilione.
2 Timothée 3.6-3.7 Proverbes 14.6 Matthieu 24.23-24.26 Matthieu 11.25-11.27 Romains 9.31-9.33
13 Siku hiyo wanawali wazuri na wavulana watazimia kwa kiu.
Osée 2.3 Lamentations 1.18 Lamentations 2.21 Esaïe 40.30 Psaumes 63.1
14 Na hao waapao kwa dhambi ya Samaria, na kusema, Kama aishivyo Mungu wako, Ee Dani, na, Kama iishivyo njia ya Beer-sheba, hao nao wataanguka, wasiinuke tena.
Amos 5.5 1 Rois 12.28-12.29 Deutéronome 9.21 Actes 9.2 Psaumes 36.12

Cette Bible est dans le domaine public.