Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Amos 1.2
Bible en Swahili de l’est


Prophéties contre les nations

Introduction

1 Maneno ya Amosii, aliyekuwa mmoja wa wachungaji wa Tekoa; maono aliyoyaona katika habari za Israeli, siku za Uzia, mfalme wa Yuda, na siku za Yeroboamu, mwana wa Yoashi, mfalme wa Israeli, miaka miwili kabla ya tetemeko la nchi.
Amos 7.14 Zacharie 14.5 2 Samuel 14.2 Jérémie 6.1 Osée 1.1
2 Naye alisema, Bwana atanguruma toka Sayuni, Atatoa sauti yake toka Yerusalemu; Na malisho ya wachungaji yataomboleza, Na kilele cha Karmeli kitanyauka.
Joël 3.16 Jérémie 25.30 Amos 9.3 Jérémie 12.4 Esaïe 42.13

Sur Damas

3 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Dameski, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wameipura Gileadi kwa vyombo vya kupuria vya chuma;
Esaïe 8.4 Amos 1.9 Amos 2.6 Amos 2.4 Amos 1.6
4 lakini nitapeleka moto uingie katika nyumba ya Hazaeli, nao utayateketeza majumba ya Ben-hadadi.
Jérémie 49.27 2 Rois 8.7-8.15 Jérémie 17.27 2 Rois 13.3 2 Rois 13.25
5 Nami nitalivunja komeo la Dameski, na kuwakatilia mbali wenyeji wa bondeni mwa Aveni, na yeye aishikaye fimbo ya enzi katika Beth-Adini; na watu wa Shamu watakwenda hali ya kufungwa hata Kiri, asema Bwana.
2 Rois 16.9 Amos 9.7 Jérémie 51.30 Lamentations 2.9 Esaïe 43.14

Sur Gaza

6 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Gaza, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu waliichukua katika hali ya kufungwa kabila nzima, wawatie katika mikono ya Edomu;
2 Chroniques 28.18 Abdias 1.11 Amos 1.9 Amos 1.11 1 Samuel 6.17
7 lakini nitapeleka moto juu ya ukuta wa Gaza, nao utayateketeza majumba yake.
Jérémie 47.1 2 Rois 18.8 2 Chroniques 26.6 Psaumes 75.7-75.8 Jérémie 25.18-25.20
8 Nami nitamkatilia mbali mwenyeji katika Ashdodi; na yeye aishikaye fimbo ya enzi katika Ashkeloni; nami nitaugeuza mkono wangu uwe juu ya Ekroni; na mabaki ya Wafilisti wataangamia, asema Bwana MUNGU.
Ezéchiel 25.16 Esaïe 14.29-14.31 Jérémie 47.4-47.5 Sophonie 2.4-2.7 Esaïe 20.1

Sur Tyr

9 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Tiro, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wameitia kabila nzima katika mikono ya Edomu, wala hawakulikumbuka agano la udugu;
1 Rois 9.11-9.14 Esaïe 23.1-23.18 Joël 3.4-3.8 Zacharie 9.2-9.4 2 Chroniques 2.8-2.16
10 lakini nitapeleka moto juu ya ukuta wa Tiro, nao utayateketeza majumba yake.
Zacharie 9.4 Amos 1.4 Ezéchiel 26.12 Amos 1.7

Sur Édom

11 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Edomu, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu alimfuatia ndugu yake kwa upanga, akatupilia mbali huruma zake zote; hasira yake ikararua-rarua daima, akaishika ghadhabu yake milele;
2 Chroniques 28.17 Nombres 20.14-20.21 Jérémie 49.7-49.22 Ezéchiel 25.12-25.14 Malachie 1.4
12 lakini nitapeleka moto juu ya Temani, nao utayateketeza majumba ya Bosra.
Jérémie 49.20 Abdias 1.9-1.10 Jérémie 49.7 Jérémie 49.13 Jérémie 49.22

Sur Ammon

13 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya wana wa Amoni, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wamewapasua wanawake wa Gileadi wenye mimba, ili wapate kuongeza mipaka yao;
Ezéchiel 25.2-25.7 Osée 13.16 Jérémie 49.1-49.6 Sophonie 2.8-2.9 Esaïe 5.8
14 lakini nitawasha moto katika ukuta wa Raba, nao utayateketeza majumba yake; pamoja na kupiga kelele siku ya vita, pamoja na tufani katika siku ya chamchela;
Amos 2.2 Jérémie 49.2 Deutéronome 3.11 2 Samuel 12.26 Esaïe 30.30
15 na mfalme wao atakwenda utumwani, yeye na wakuu wake wote pamoja, asema Bwana.
Jérémie 49.3

Cette Bible est dans le domaine public.