Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 9.4
Bible en Swahili de l’est


1 Usifurahi, Israeli, kwa sababu ya furaha, kama hao mataifa; kwa kuwa umezini juu ya Mungu wako, umependa ujira katika kila sakafu ya nafaka.
Osée 10.5 Jérémie 44.17 Osée 4.12 Amos 6.6-6.7 Ezéchiel 20.32
2 Sakafu na shinikizo hazitawalisha, na divai mpya itampungukia.
Osée 2.9 Esaïe 24.7-24.12 Osée 2.12 Aggée 2.16 Amos 4.5-4.11
3 Hawatakaa katika nchi ya Bwana; lakini Efraimu atarudi Misri, nao watakula chakula kinajisi katika Ashuru.
Ezéchiel 4.13 Osée 8.13 Lévitique 25.23 Jérémie 2.7 Jérémie 16.18
4 Hawatammiminia Bwana divai, wala hazitampendeza sadaka zao; mkate wao utakuwa kama chakula cha matanga kwao; wote watakaokila watatiwa unajisi; kwa maana mkate wao utakuwa kwa shauku zao; hautaingia katika nyumba ya Bwana.
Osée 8.13 Jérémie 6.20 Deutéronome 26.14 Osée 3.4 Ezéchiel 24.17
5 Mtafanya nini katika siku ya mkutano wa idi, na katika siku ya karamu ya Bwana?
Esaïe 10.3 Jérémie 5.31 Osée 2.11 Joël 1.13
6 Kwa maana, tazama, wamekwenda zao ili kukimbia uharibifu, lakini Misri itawakusanya, Nofu itawazika; vitu vyao vya fedha viwapendezavyo, magugu yatavimiliki; miiba itakuwa katika hema zao.
Osée 10.8 Esaïe 5.6 Osée 9.3 Osée 8.13 Esaïe 7.23
7 Siku za kupatilizwa zimekuja, siku za kulipa zimefika; Israeli atayajua hayo; huyo nabii ni mpumbavu, huyo mtu mwenye roho ana wazimu; kwa sababu ya wingi wa uovu wako, na kwa sababu uadui umekuwa mkubwa.
Michée 7.4 Ezéchiel 14.9-14.10 Jérémie 10.15 Esaïe 10.3 Lamentations 2.14
8 Efraimu alikuwa mlinzi pamoja na Mungu wangu; na huyo nabii, mtego wa mwinda ndege u katika njia zake zote; katika nyumba ya Mungu wake umo uadui.
Osée 5.1 Ezéchiel 3.17 Esaïe 62.6 Jérémie 31.6 2 Rois 6.17-6.18
9 Wamejiharibu mno, kama katika siku za Gibea; ataukumbuka uovu wao, atazilipiza dhambi zao.
Osée 10.9 Osée 8.13 Juges 19.16-20.21 Esaïe 31.6 Esaïe 24.5

Passé et avenir d’Israël

10 Mimi nalimkuta Israeli kama zabibu nyikani; nami naliwaona baba zenu kama matunda ya mtini yaliyoiva kwanza, wakati wake wa kwanza; lakini walikwenda Baal-Peori, wakajiweka wakfu kwa kitu cha aibu, wakawa chukizo kama kitu kile walichokipenda.
Osée 4.14 Jérémie 11.13 Nombres 25.1-25.18 Jérémie 2.2-2.3 Osée 2.15
11 Naye Efraimu, utukufu wake utarukia mbali kama ndege, uzazi hautakuwako, wala aliye na mimba, wala achukuaye mimba.
Osée 4.7 Osée 10.5 Osée 9.14 Deutéronome 28.18 Psaumes 58.8
12 Wajapolea watoto wao, mimi nitawanyang’anya watoto wao, asisalie hata mtu mmoja; naam, ole wao! Nitakapoondoka na kuwaacha.
Osée 7.13 Deutéronome 31.17 Osée 9.16 Deutéronome 32.25 1 Samuel 28.15-28.16
13 Efraimu amepandwa mahali pazuri, kama nilivyoona Tiro; lakini Efraimu atamtolea mwuaji watoto wake.
Ezéchiel 26.1-26.21 Ezéchiel 27.3 2 Rois 15.16 Osée 9.16 Jérémie 9.21
14 Wape, Ee Bwana; utawapa kitu gani? Wape tumbo lenye kuharibu mimba na maziwa makavu.
Luc 23.29 Osée 9.13 Marc 13.17 1 Corinthiens 7.26 Job 21.10
15 Uovu wao wote u katika Gilgali; maana huko naliwachukia; kwa sababu ya uovu wa matendo yao nitawafukuza watoke katika nyumba yangu; sitawapenda tena; wakuu wao wote ni waasi.
Osée 4.15 Esaïe 1.23 Osée 12.11 Amos 4.4 1 Samuel 7.16
16 Efraimu amepigwa; mzizi wao umekauka; hawatazaa matunda; naam, wajapozaa, nitaliua tunda la tumbo lipendwalo sana.
Osée 9.11-9.13 Ezéchiel 24.21 Esaïe 5.24 Osée 5.11 Esaïe 40.24
17 Mungu wangu atawatupilia mbali, kwa sababu hawakumsikiliza; nao watakuwa watu wa kutanga-tanga kati ya mataifa.
Deutéronome 28.64-28.65 Osée 7.13 Amos 9.9 Jérémie 25.3-25.4 2 Chroniques 36.16

Cette Bible est dans le domaine public.