Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 9.10
Bible en Swahili de l’est


1 Usifurahi, Israeli, kwa sababu ya furaha, kama hao mataifa; kwa kuwa umezini juu ya Mungu wako, umependa ujira katika kila sakafu ya nafaka.
Osée 10.5 Osée 4.12 Jérémie 44.17 Osée 5.7 Esaïe 17.11
2 Sakafu na shinikizo hazitawalisha, na divai mpya itampungukia.
Osée 2.9 Amos 4.5-4.11 Aggée 1.9 Michée 6.13-6.16 Joël 1.3-1.7
3 Hawatakaa katika nchi ya Bwana; lakini Efraimu atarudi Misri, nao watakula chakula kinajisi katika Ashuru.
Ezéchiel 4.13 Osée 8.13 Lévitique 25.23 Jérémie 2.7 1 Rois 9.7
4 Hawatammiminia Bwana divai, wala hazitampendeza sadaka zao; mkate wao utakuwa kama chakula cha matanga kwao; wote watakaokila watatiwa unajisi; kwa maana mkate wao utakuwa kwa shauku zao; hautaingia katika nyumba ya Bwana.
Osée 8.13 Jérémie 6.20 Deutéronome 26.14 Ezéchiel 24.17 Osée 3.4
5 Mtafanya nini katika siku ya mkutano wa idi, na katika siku ya karamu ya Bwana?
Esaïe 10.3 Jérémie 5.31 Osée 2.11 Joël 1.13
6 Kwa maana, tazama, wamekwenda zao ili kukimbia uharibifu, lakini Misri itawakusanya, Nofu itawazika; vitu vyao vya fedha viwapendezavyo, magugu yatavimiliki; miiba itakuwa katika hema zao.
Osée 10.8 Esaïe 5.6 Osée 9.3 Osée 8.13 Esaïe 7.23
7 Siku za kupatilizwa zimekuja, siku za kulipa zimefika; Israeli atayajua hayo; huyo nabii ni mpumbavu, huyo mtu mwenye roho ana wazimu; kwa sababu ya wingi wa uovu wako, na kwa sababu uadui umekuwa mkubwa.
Michée 7.4 Jérémie 10.15 Esaïe 10.3 Lamentations 2.14 Ezéchiel 13.3
8 Efraimu alikuwa mlinzi pamoja na Mungu wangu; na huyo nabii, mtego wa mwinda ndege u katika njia zake zote; katika nyumba ya Mungu wake umo uadui.
Ezéchiel 3.17 Osée 5.1 Esaïe 62.6 2 Rois 4.43 2 Rois 4.33-4.37
9 Wamejiharibu mno, kama katika siku za Gibea; ataukumbuka uovu wao, atazilipiza dhambi zao.
Osée 10.9 Osée 8.13 Esaïe 31.6 Juges 19.16-20.21 Esaïe 24.5

Passé et avenir d’Israël

10 Mimi nalimkuta Israeli kama zabibu nyikani; nami naliwaona baba zenu kama matunda ya mtini yaliyoiva kwanza, wakati wake wa kwanza; lakini walikwenda Baal-Peori, wakajiweka wakfu kwa kitu cha aibu, wakawa chukizo kama kitu kile walichokipenda.
Jérémie 11.13 Osée 4.14 Michée 7.1 Psaumes 106.28-106.29 Nombres 25.1-25.18
11 Naye Efraimu, utukufu wake utarukia mbali kama ndege, uzazi hautakuwako, wala aliye na mimba, wala achukuaye mimba.
Osée 9.14 Deutéronome 28.18 Osée 4.7 Osée 10.5 Deutéronome 28.57
12 Wajapolea watoto wao, mimi nitawanyang’anya watoto wao, asisalie hata mtu mmoja; naam, ole wao! Nitakapoondoka na kuwaacha.
Osée 7.13 Deutéronome 31.17 1 Samuel 28.15-28.16 Osée 9.16 Deutéronome 32.25
13 Efraimu amepandwa mahali pazuri, kama nilivyoona Tiro; lakini Efraimu atamtolea mwuaji watoto wake.
Ezéchiel 26.1-26.21 Ezéchiel 27.3 Amos 7.17 Osée 13.16 Osée 10.14
14 Wape, Ee Bwana; utawapa kitu gani? Wape tumbo lenye kuharibu mimba na maziwa makavu.
Luc 23.29 Job 21.10 Osée 9.11 Matthieu 24.19 Luc 21.23
15 Uovu wao wote u katika Gilgali; maana huko naliwachukia; kwa sababu ya uovu wa matendo yao nitawafukuza watoke katika nyumba yangu; sitawapenda tena; wakuu wao wote ni waasi.
Osée 4.15 Osée 12.11 Esaïe 1.23 Michée 6.5 Actes 4.27
16 Efraimu amepigwa; mzizi wao umekauka; hawatazaa matunda; naam, wajapozaa, nitaliua tunda la tumbo lipendwalo sana.
Osée 9.11-9.13 Ezéchiel 24.21 Esaïe 40.24 Job 18.16 Osée 8.7
17 Mungu wangu atawatupilia mbali, kwa sababu hawakumsikiliza; nao watakuwa watu wa kutanga-tanga kati ya mataifa.
Deutéronome 28.64-28.65 Osée 7.13 Esaïe 7.13 Psaumes 81.11-81.13 Jérémie 26.4-26.6

Cette Bible est dans le domaine public.