Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Daniel 10.6
Bible en Swahili de l’est


Une apparition terrifiante

1 Katika mwaka wa tatu wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, Danielii, ambaye jina lake aliitwa Belteshaza, alifunuliwa neno; na neno lile lilikuwa kweli; maana ni vita vikubwa; naye akalifahamu neno lile, akaelewa na maono hayo.
Daniel 6.28 Daniel 1.21 Daniel 8.26 Daniel 1.7 Daniel 1.17
2 Katika siku zile mimi, Danielii, nalikuwa nikiomboleza muda wa majuma matatu kamili.
Néhémie 1.4 Esdras 9.4-9.5 Psaumes 42.9 Psaumes 43.2 Jérémie 9.1
3 Sikula chakula kitamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwangu, wala sikujipaka mafuta kabisa, hata majuma matatu kamili yalipotimia.
Matthieu 6.17 Daniel 6.18 2 Samuel 19.24 Daniel 11.8 Esaïe 24.6-24.11
4 Na siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa kando ya ule mto mkubwa, Hidekeli;
Genèse 2.14 Ezéchiel 1.3 Daniel 8.2
5 naliinua macho yangu, nikatazama, na kumbe, mtu aliyevikwa nguo za kitani, viuno vyake vimefungwa dhahabu safi ya Ufazi;
Ezéchiel 9.2 Daniel 12.6-12.7 Jérémie 10.9 Apocalypse 1.13-1.15 Josué 5.13
6 mwili wake pia ulikuwa kama zabarajadi safi, na uso wake mfano wa umeme, na macho yake kama taa za moto, na mikono yake na miguu yake rangi yake kama shaba iliyosuguliwa sana, na sauti ya maneno yake kama sauti ya umati wa watu.
Apocalypse 19.12 Matthieu 17.2 Ezéchiel 1.14 Ezéchiel 10.9 Ezéchiel 1.16
7 Nami, Danielii, nikaona maono haya peke yangu; maana wale watu waliokuwa pamoja nami hawakuyaona maono haya; lakini tetemeko kuu liliwashika, hata wakakimbia ili kujificha.
Actes 9.7 Ezéchiel 12.18 Actes 22.9 Genèse 3.10 Esaïe 2.10
8 Basi nikaachwa peke yangu, nikaona maono haya makubwa, wala hazikubaki nguvu ndani yangu; maana uzuri wangu uligeuzwa ndani yangu kuwa uharibifu, wala sikusaziwa nguvu.
Daniel 8.27 Daniel 7.28 Habakuk 3.16 Apocalypse 1.17 Matthieu 17.6
9 Walakini naliisikia sauti ya maneno yake; nami niliposikia sauti ya maneno yake, ndipo nikashikwa na usingizi mzito, na uso wangu umeielekea nchi.
Daniel 8.18 Genèse 15.12 Job 4.13 Luc 22.45 Job 33.15
10 Na tazama, mkono ukanigusa, ukaniweka juu ya magoti yangu, na vitanga vya mikono yangu.
Apocalypse 1.17 Jérémie 1.9 Daniel 8.18 Daniel 10.18 Daniel 10.16
11 Akaniambia, Ee Danielii, mtu upendwaye sana, yafahamu maneno nikuambiayo, ukasimame kiwima-wima; maana kwako nimetumwa sasa. Na aliponiambia neno hili, nalisimama nikitetemeka.
Daniel 8.16-8.17 Ezéchiel 2.1 Jean 13.23 Actes 26.16 Cantique 7.10
12 Ndipo akaniambia, Usiogope, Danielii; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako.
Actes 10.30-10.31 Daniel 9.20-9.23 Daniel 10.19 Daniel 10.2-10.3 Esaïe 41.14
13 Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi.
Daniel 12.1 Jude 1.9 Apocalypse 12.7 Daniel 10.20-10.21 1 Pierre 3.22
14 Sasa nimekuja kukufahamisha mambo yatakayowapata watu wako katika siku za mwisho; maana maono hayo ni ya siku nyingi bado.
Daniel 8.26 Daniel 2.28 Habakuk 2.3 Daniel 12.9 Daniel 12.4
15 Na alipokwisha kusema nami maneno hayo, nikauelekeza uso wangu chini, nikawa bubu.
Ezéchiel 24.27 Luc 1.20 Daniel 8.18 Daniel 10.9 Ezéchiel 33.22
16 Na kumbe, mmoja mfano wa wanadamu akanigusa midomo yangu; ndipo nikafumbua kinywa changu, nikanena, nikamwambia yeye aliyesimama karibu nami, Ee Bwana wangu, kwa sababu ya maono haya huzuni zangu zimenipata tena; hata sikusaziwa nguvu.
Daniel 8.15 Esaïe 6.7 Jérémie 1.9 Daniel 8.17 Daniel 7.28
17 Maana, mtumishi wa Bwana wangu huyu atawezaje kusema na Bwana wangu huyu? Kwa maana kwangu mimi, mara hazikusalia nguvu ndani yangu, wala pumzi haikusalia ndani yangu.
Esaïe 6.1-6.5 Exode 24.10-24.11 Exode 33.20 Jean 1.18 Genèse 32.20
18 Kisha mmoja mfano wa mwanadamu akanigusa tena, akanitia nguvu.
Daniel 10.16 Esaïe 35.3-35.4 Job 23.6 Colossiens 1.11 2 Corinthiens 12.9-12.10
19 Akasema, Ee mtu upendwaye sana, usiogope; amani na iwe kwako, uwe na nguvu, naam, uwe na nguvu. Aliposema nami nikapata nguvu, nikasema, Ee Bwana wangu, na aseme Bwana wangu; kwa maana umenitia nguvu.
Josué 1.9 Esaïe 35.4 Juges 6.23 Daniel 10.11-10.12 Josué 1.6-1.7
20 Ndipo akasema, Je! Unajua sababu hata nikakujia? Na sasa nitarudi ili nipigane na mkuu wa Uajemi; nami nitakapotoka huku, tazama, mkuu wa Uyunani atakuja.
Daniel 8.21 Daniel 10.13 Daniel 8.5-8.8 Actes 12.23 Daniel 11.2-11.4
21 Lakini nitakuambia yaliyoandikwa katika maandiko ya kweli; wala hapana anisaidiaye juu ya hao ila huyo Mikaeli, mkuu wenu.
Daniel 10.13 Apocalypse 12.7 Jude 1.9 Daniel 12.1 Daniel 12.4

Cette Bible est dans le domaine public.