Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 8.12
Bible en Swahili de l’est


Idolâtrie d’Israël

1 Ikawa katika mwaka wa sita, mwezi wa sita, siku ya tano ya mwezi, nilipokuwa nikikaa nyumbani mwangu, wazee wa Yuda nao wali wamekaa mbele yangu, mkono wa Bwana MUNGU ukaniangukia huko.
Ezéchiel 20.1 Ezéchiel 14.1 Ezéchiel 1.2-1.3 Ezéchiel 33.31 Ezéchiel 32.17
2 Ndipo nikaangalia, na tazama, kana kwamba ni mfano wa moto; tangu mfano wa viuno vyake na chini, moto; na tangu mfano wa viuno vyake na juu, kana kwamba ni mfano wa mwangaza, kama rangi ya kaharabu.
Ezéchiel 1.4 Ezéchiel 1.26-1.27 Apocalypse 1.14-1.15 Daniel 7.9-7.10
3 Naye akanyosha mfano wa mkono, akanishika kwa kishungi kimoja cha nywele za kichwa changu; nayo roho ikaniinua kati ya dunia na mbingu, ikanileta katika maono ya Mungu mpaka Yerusalemu, mpaka mlango wa kuingilia ua wa ndani uelekeao upande wa kaskazini; mahali palipokuwa pamewekwa sanamu ya wivu, itiayo wivu.
Deutéronome 32.16 Ezéchiel 11.1 Daniel 5.5 Ezéchiel 5.11 Ezéchiel 40.2
4 Na tazama, huo utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwapo hapo, sawasawa na maono yale niliyoyaona katika uwanda.
Ezéchiel 3.22-3.23 Exode 40.34-40.35 Ezéchiel 11.22-11.23 Exode 25.22 Ezéchiel 1.26-1.28
5 Ndipo akaniambia, Mwanadamu, inua macho yako sasa, uangalie upande wa kaskazini. Basi nikainua macho yangu, nikaangalia upande wa kaskazini, na tazama, upande wa kaskazini wa mlango, ilikuwako sanamu ile ya wivu, mahali pale pa kuingilia.
Ezéchiel 8.3 Jérémie 3.2 Psaumes 48.2 Psaumes 78.58 Jérémie 32.34
6 Akaniambia, Mwanadamu, je! Unayaona wanayoyafanya, yaani, haya machukizo makubwa wanayoyafanya nyumba ya Israeli hapa, hata niende zangu mbali na patakatifu pangu? Lakini utaona tena machukizo makubwa mengine.
Ezéchiel 5.11 Ezéchiel 10.19 Ezéchiel 8.9 Jérémie 23.11 Lamentations 2.6-2.7
7 Akanileta hata mlango wa ua; nami nilipoangalia, tazama, pana tundu katika ukuta.
1 Rois 7.12 2 Rois 21.5
8 Ndipo akaniambia, Mwanadamu, toboa sasa katika ukuta huu; nami nilipotoboa, tazama, pana mlango.
Esaïe 29.15 Job 34.22 Jérémie 23.24 Jérémie 2.34 Amos 9.2-9.3
9 Akaniambia, Ingia uyaone machukizo mabaya wanayoyafanya hapa.
Ezéchiel 20.8
10 Basi, nikaingia, nikaona; na tazama, kila namna ya wadudu, na wanyama wachukizao, na taswira za vinyago vyote vya nyumba ya Israeli, zimepigwa ukutani pande zote.
Exode 20.4 Romains 1.23 Lévitique 11.42-11.44 Lévitique 11.10-11.12 Deutéronome 4.18
11 Na watu sabini wa wazee wa Israeli walikuwa wamesimama na kuzielekea, na katikati yao alisimama Yaazania, mwana wa Shafani; kila mmoja ana chetezo mkononi mwake, na harufu ya moshi wa uvumba ilipaa juu.
Nombres 16.35 Nombres 16.17 Nombres 11.16 Jérémie 19.1 Nombres 11.25
12 Kisha akaniambia, Mwanadamu, umeyaona wanayotenda wazee wa nyumba ya Israeli gizani, kila mtu ndani ya vyumba vyake vya sanamu? Maana husema, Bwana hatuoni; Bwana ameiacha nchi hii.
Ezéchiel 9.9 Esaïe 29.15 Psaumes 10.11 Psaumes 94.7-94.10 Ezéchiel 8.11
13 Akaniambia tena, Utaona tena machukizo makubwa mengine wanayoyatenda.
Ezéchiel 8.6 Ezéchiel 8.15 Jérémie 9.3 2 Timothée 3.13
14 Ndipo akanileta mpaka mlango wa kuingilia katika nyumba ya Bwana, ulioelekea upande wa kaskazini, na tazama, wanawake wameketi wakimlilia Tamuzi.
Ezéchiel 44.4 Ezéchiel 46.9
15 Akaniambia, Mwanadamu umeyaona haya? Utaona tena machukizo makubwa kuliko hayo.
Ezéchiel 8.9 2 Timothée 3.13 Ezéchiel 8.6 Ezéchiel 8.12-8.13
16 Akanileta mpaka ua wa ndani wa nyumba ya Bwana, na tazama, mlangoni pa hekalu la Bwana, kati ya ukumbi na madhabahu, walikuwako watu kama ishirini na watano, wamelipa kisogo hekalu la Bwana, na nyuso zao zimeelekea upande wa mashariki, nao wanaliabudu jua, kwa kuuelekea upande wa mashariki.
Jérémie 2.27 Deutéronome 17.3 Deutéronome 4.19 Joël 2.17 Ezéchiel 45.19
17 Basi, akaniambia, Umeyaona haya, Ee mwanadamu? Je! Ni jambo dogo sana kwa nyumba ya Yuda, wayafanye machukizo wanayoyafanya hapa? Kwa maana wameijaza nchi hii udhalimu, tena wamerejea nyuma ili kunikasirisha; na, tazama, wanaliweka tawi puani.
Ezéchiel 9.9 Ezéchiel 7.23 Amos 3.10 Michée 2.2 Ezéchiel 11.6
18 Kwa sababu hiyo mimi nami nitatenda kwa ghadhabu; jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma, na wajapolia masikioni mwangu kwa sauti kuu, sitawasikiliza.
Esaïe 1.15 Michée 3.4 Zacharie 7.13 Jérémie 11.11 Juges 10.13-10.14

Cette Bible est dans le domaine public.