Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 6
Bible en Swahili de l’est


Elimination de l’idolâtrie

1 Neno la Bwana likanijia, kusema,
2 Mwanadamu, uelekeze uso wako uitazame milima ya Israeli, ukaitabirie,
Ezéchiel 35.12 Ezéchiel 36.1 Ezéchiel 20.46 Ezéchiel 19.9 Ezéchiel 25.2
3 ukisema, Enyi milima ya Israeli, lisikieni neno la Bwana MUNGU; Bwana MUNGU aiambia hivi milima na vilima, na vijito na mabonde; Tazama, mimi, naam, mimi, nitaleta upanga juu yenu, nami nitapaharibu mahali penu palipoinuka,
Lévitique 26.30 Ezéchiel 36.1-36.4 Ezéchiel 36.8 Jérémie 3.6 Jérémie 22.29
4 Na madhabahu zenu zitakuwa ukiwa, na sanamu zenu za jua zitavunjika; nami nitawatupa wana wenu waliouawa mbele ya vinyago vyenu.
2 Chroniques 14.5 Lévitique 26.30 Ezéchiel 6.13 2 Rois 23.16-23.20 Jérémie 8.1-8.2
5 Nami nitaiweka mizoga ya wana wa Israeli mbele ya vinyago vyao; nami nitaitawanya mifupa yenu pande zote za madhabahu zenu.
Jérémie 8.1-8.2 2 Rois 23.16 2 Rois 23.14
6 Kila mahali mkaapo miji itaharibika, na mahali palipoinuka patakuwa ukiwa; ili madhabahu zenu ziharibiwe, na kufanywa ukiwa, na vinyago vyenu vivunjwe, na kukoma, na sanamu zenu za jua zikatwe, na kuangushwa, na kazi zenu zifutwe kabisa.
Esaïe 6.11 Ezéchiel 5.14 Zacharie 13.2 Michée 1.7 Lévitique 26.30
7 Na hao waliouawa wataanguka katikati yenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Ezéchiel 24.24 Jérémie 18.21 Ezéchiel 25.17 Ezéchiel 13.23 Ezéchiel 28.23
8 Lakini nitasaza mabaki; maana mtakuwa na baadhi ya watu watakaoukimbia upanga kati ya mataifa, mtakapokuwa mmetawanyika katika nchi za watu.
Ezéchiel 14.22 Ezéchiel 12.16 Jérémie 44.14 Esaïe 6.13 Jérémie 44.28
9 Na hao wa kwenu watakaookoka watanikumbuka kati ya mataifa, watakakochukuliwa mateka, jinsi nilivyoiponda mioyo yao ya kikahaba, iliyoniacha, na macho yao, yaendayo kufanya uasherati na vinyago vyao; nao watajichukia nafsi zao machoni pao wenyewe, kwa sababu ya mabaya yao yote, waliyoyatenda kwa machukizo yao yote.
Ezéchiel 20.43 Esaïe 7.13 Psaumes 78.40 Jérémie 51.50 Ezéchiel 20.7
10 Nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana; sikusema bure kama nitawatenda mabaya hayo.
Jérémie 5.12-5.14 Ezéchiel 14.22-14.23 Daniel 9.12 Jérémie 44.28 Ezéchiel 6.7
11 Bwana MUNGU asema hivi; Piga kwa mkono wako, ipige nchi kwa mguu wako, ukaseme, Ole! Kwa sababu ya machukizo maovu yote ya nyumba ya Israeli; maana wataanguka kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni.
Ezéchiel 5.12 Ezéchiel 25.6 Ezéchiel 9.4 Esaïe 58.1 Jérémie 15.2-15.3
12 Yeye aliye mbali sana atakufa kwa tauni; na yeye aliye karibu atakufa kwa upanga; na yeye atakayesalia, na kuhusuriwa katika mji, atakufa kwa njaa, hivyo ndivyo nitakavyoitimiza ghadhabu yangu juu yao.
Ezéchiel 5.13 Daniel 9.7 Lamentations 4.11 Lamentations 4.22 Esaïe 40.2
13 Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, watu wa kwao waliouawa watakapokuwa kati ya vinyago vyao, pande zote za madhabahu zao, juu ya kila kilima kirefu, juu ya vilele vya milima, na chini ya kila mti wenye majani mabichi, na chini ya kila mwaloni mnene, pale pale walipovifukizia uvumba mzuri vinyago vyao vyote.
Ezéchiel 20.28 Osée 4.13 1 Rois 14.23 Jérémie 2.20 2 Rois 16.4
14 Nami nitanyosha mkono wangu juu yao, na kuifanya nchi kuwa maganjo, tena ukiwa mbaya kuliko jangwa upande wa Dibla, katika makao yao yote; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Esaïe 5.25 Esaïe 9.12 Ezéchiel 20.33-20.34 Ezéchiel 14.13 Nombres 33.46

Cette Bible est dans le domaine public.