Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 3.11
Bible en Swahili de l’est


1 Akaniambia, Mwanadamu, kula uonacho; kula gombo hili, kisha enenda ukaseme na wana wa Israeli.
Apocalypse 10.9-10.10 Ezéchiel 2.8-2.9 Ezéchiel 3.17-3.21 Ezéchiel 3.10-3.11 Ezéchiel 2.3
2 Basi nikafunua kinywa changu, naye akanilisha lile gombo.
Jérémie 25.17 Actes 26.19
3 Akaniambia, Mwanadamu, lisha tumbo lako, ulijaze tumbo lako kwa hili gombo nikupalo. Ndipo nikalila, nalo kinywani mwangu lilikuwa tamu, kama utamu wa asali.
Jérémie 15.16 Apocalypse 10.9-10.10 Psaumes 119.103 Psaumes 19.10 Jérémie 6.11
4 Akaniambia, Mwanadamu, haya! Waendee wana wa Israeli ukawaambie maneno yangu.
Actes 1.8 Ezéchiel 2.3 Matthieu 10.5-10.6 Matthieu 15.24 Ezéchiel 2.7
5 Maana wewe hukutumwa kwa watu wa maneno mageni, ama wa lugha ngumu, bali kwa nyumba ya Israeli;
Jonas 1.2 Esaïe 33.19 Psaumes 81.5 Esaïe 28.11 Actes 26.17-26.18
6 si kwa watu wa kabila nyingi wenye maneno mageni, na lugha ngumu, ambao huwezi kufahamu maneno yao. Bila shaka, kama ningekutuma kwa watu hao, wangekusikiliza.
Luc 11.30-11.32 Romains 9.30-9.33 Jonas 3.5-3.10 Matthieu 11.20-11.24 Actes 27.28
7 Bali nyumba ya Israeli hawatakusikiliza wewe; kwa kuwa hawanisikilizi mimi; maana nyumba yote ya Israeli wana vipaji vigumu, na mioyo yenye ukaidi.
Ezéchiel 2.4 1 Samuel 8.7 Esaïe 3.9 Ezéchiel 24.7 Luc 19.14
8 Tazama, nimeufanya uso wako kuwa mgumu juu ya nyuso zao, na kipaji cha uso chako kuwa kigumu juu ya vipaji vya nyuso vyao.
Jérémie 1.18 Esaïe 50.7 Exode 4.15-4.16 Exode 11.4-11.8 1 Rois 21.20
9 Kama almasi ilivyo ngumu kuliko gumegume, ndivyo nilivyokifanya kipaji chako; usiwaogope, wala usifadhaike kwa sababu ya nyuso zao, wajapokuwa ni nyumba ya kuasi.
Ezéchiel 2.6 Esaïe 50.7 Esaïe 41.10 Jérémie 17.18 Michée 3.8
10 Tena akaniambia, Mwanadamu, maneno yangu yote nitakayokuambia, yapokee moyoni mwako, na kuyasikia kwa masikio yako.
Job 22.22 Ezéchiel 3.1-3.3 Luc 8.15 1 Thessaloniciens 2.13 Proverbes 8.10
11 Haya! Enenda uwafikilie watu hao waliohamishwa, kwa wana wa watu wako, ukaseme nao, na kuwaambia, Bwana MUNGU asema hivi; kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia.
Ezéchiel 2.7 Ezéchiel 33.17 Ezéchiel 33.30 Ezéchiel 33.2 Ezéchiel 33.12
12 Ndipo roho ikaniinua, nami nikasikia nyuma yangu sauti kama mshindo wa radi kuu, ikisema, Na uhimidiwe utukufu wa Bwana tokea mahali pake.
Ezéchiel 8.3 Actes 8.39 Ezéchiel 11.1 Actes 2.2 Ezéchiel 3.14
13 Nikasikia mshindo wa mabawa ya vile viumbe hai, walipogusana, na mshindo wa yale magurudumu kando yao, mshindo wa radi kuu.
Ezéchiel 10.16-10.17 Ezéchiel 1.24 Ezéchiel 10.5 2 Samuel 5.24 Ezéchiel 1.15
14 Basi roho ikaniinua, ikanichukua mahali pengine; nami nikaenda kwa uchungu, na hasira kali rohoni mwangu, na mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu kwa nguvu.
Ezéchiel 37.1 Ezéchiel 1.3 2 Rois 3.15 Ezéchiel 8.3 Jérémie 20.14-20.18
15 Ndipo nikawafikia watu waliohamishwa, huko Tel-abibu, waliokuwa wakikaa karibu na mto Kebari, nikafika huko walikokuwa wakikaa; nikaketi huko miongoni mwao muda wa siku saba, katika hali ya ushangao mwingi.
Job 2.13 Psaumes 137.1 Ezéchiel 1.1 Genèse 50.10 Ezéchiel 10.15
16 Hata ikawa, mwisho wa siku saba, neno la Bwana likanijia, kusema,
Jérémie 42.7
17 Mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi wa nyumba ya Israeli; basi, sikia neno hili litokalo katika kinywa changu, ukawape maonyo haya yatokayo kwangu.
Esaïe 52.8 Jérémie 6.17 2 Chroniques 19.10 Esaïe 56.10 Esaïe 62.6
18 Nimwambiapo mtu mbaya, Hakika utakufa; wewe usimpe maonyo, wala husemi na huyo mtu mbaya ili kumwonya, kusudi aache njia yake mbaya na kujiokoa roho yake; mtu yule mbaya atakufa katika uovu wake; lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako.
Ezéchiel 33.6 Ezéchiel 33.8-33.10 Ezéchiel 3.20 Genèse 2.17 Ezéchiel 18.20
19 Lakini ukimwonya mtu mbaya, wala yeye hauachi ubaya wake, wala njia yake mbaya, atakufa katika uovu wake; bali wewe umejiokoa roho yako.
Ezéchiel 14.14 Ezéchiel 14.20 Ezéchiel 33.9 Actes 20.26 1 Timothée 4.16
20 Tena mtu mwenye haki aiachapo haki yake, na kutenda uovu, nami nikiweka kikwazo mbele yake, atakufa; kwa sababu hukumwonya, atakufa katika uovu wake, wala matendo yake ya haki aliyoyatenda hayatakumbukwa; lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako.
Ezéchiel 18.24 Ezéchiel 3.18 Ezéchiel 33.12-33.13 Hébreux 10.38 Psaumes 125.5
21 Bali ukimwonya mwenye haki, kwamba yule mwenye haki asitende dhambi, tena ikiwa yeye hatendi dhambi, hakika ataishi, kwa sababu alikubali kuonywa; nawe umejiokoa roho yako.
Actes 20.31 1 Corinthiens 10.12 Apocalypse 3.19 Matthieu 24.24-24.25 1 Jean 3.6-3.9
22 Na mkono wa Bwana ulikuwako juu yangu huko; akaniambia, Ondoka, enenda uwandani; nami nitasema nawe huko.
Actes 9.6 Ezéchiel 1.3 Ezéchiel 8.4 Ezéchiel 37.1 Ezéchiel 3.14
23 Basi, nikaondoka, nikaenda uwandani, na tazama, utukufu wa Bwana ulisimama huko, kama utukufu ule niliouona karibu na mto Kebari; nami nikaanguka kifudifudi.
Ezéchiel 1.28 Actes 7.55 Nombres 16.19 Apocalypse 5.8 Apocalypse 4.10
24 Ndipo roho ile ikaniingia, ikanisimamisha kwa miguu yangu; akasema nami, akaniambia, Enenda ukajifungie nyumbani mwako.
Ezéchiel 2.2 Ezéchiel 4.1-4.4 Ezéchiel 37.10 Daniel 10.19 Daniel 10.8-10.10
25 Lakini wewe, mwanadamu, tazama, watakutia pingu, nao watakufunga kwazo, wala hutakwenda nje kati yao;
Ezéchiel 4.8 Actes 21.11-21.13 Jean 21.18 Marc 3.21 Actes 20.23
26 nami nitaufanya ulimi wako ugandamane na kaakaa lako, hata utakuwa bubu, wala hutakuwa mwonyaji kwao; kwa kuwa wao ni nyumba yenye kuasi.
Ezéchiel 24.27 Michée 3.6-3.7 Esaïe 1.2 Jérémie 1.17 Psaumes 51.15
27 Lakini hapo nitakaposema nawe, nitafumbua kinywa chako, nawe utawaambia, Bwana MUNGU asema hivi. Yeye asikiaye na asikie; naye akataaye na akatae; maana wao ni nyumba yenye kuasi.
Ezéchiel 12.2-12.3 Ezéchiel 24.27 Ezéchiel 3.11 Ezéchiel 29.21 Ezéchiel 2.5

Cette Bible est dans le domaine public.