Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 41.1
Bible en Swahili de l’est


1 Basi ikawa katika mwezi wa saba, Ishmaeli, mwana wa Nethania, mwana wa Elishama, mmoja wa wazao wa kifalme, tena ni mmoja wa majemadari wa mfalme, na watu kumi pamoja naye, wakamwendea Gedalia, mwana wa Ahikamu, huko Mizpa; nao walikula chakula pamoja huko Mizpa.
Jérémie 40.8 Jérémie 40.6 Psaumes 41.9 2 Samuel 3.27 Jean 13.18
2 Akaondoka huyo Ishmaeli, mwana wa Nethania, na watu wale kumi waliokuwa pamoja naye, wakampiga Gedalia, mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, kwa upanga, wakamwua; yeye ambaye mfalme wa Babeli amemweka kuwa liwali wa nchi.
2 Rois 25.25 Jérémie 40.5 Psaumes 41.9 2 Samuel 20.9-20.10 2 Samuel 3.27
3 Tena Ishmaeli akawaua Wayahudi wote waliokuwa pamoja naye, yaani, pamoja na Gedalia, huko Mizpa, na hao Wakaldayo walioonekana huko, yaani, watu wa vita.
Jérémie 41.11-41.12 Lamentations 1.2 Ecclésiaste 9.18 2 Rois 25.25
4 Ikawa siku ya pili baada ya kumwua Gedalia, wala hapakuwa na mtu aliyejua habari hii,
1 Samuel 27.11 Psaumes 52.1-52.2
5 wakafika watu kadha wa kadha toka Shekemu, na toka Shilo, na toka Samaria, watu themanini, nao wamenyoa ndevu zao, na kurarua nguo zao, nao wamejikata-kata, wakichukua sadaka na ubani mikononi mwao, ili wazilete nyumbani kwa Bwana.
Deutéronome 14.1 2 Rois 25.9 Josué 18.1 1 Rois 16.24 Genèse 33.18
6 Na Ishmaeli, mwana wa Nethania, akatoka Mizpa kwenda kuwalaki, akilia alipokuwa akiendelea; ikawa alipokutana nao akawaambia, Njoni kwa Gedalia, mwana wa Ahikamu.
2 Samuel 3.16 Jérémie 50.4 Proverbes 26.23-26.26 2 Samuel 1.2-1.16
7 Basi ikawa walipokuwa katikati ya mji, Ishmaeli, mwana wa Nethania, akawaua, akawatupa katika shimo, yeye na watu wale waliokuwa pamoja naye.
Esaïe 59.7 Psaumes 55.23 Ezéchiel 22.27 2 Rois 11.1-11.2 1 Rois 16.10-16.12
8 Lakini watu kumi walionekana miongoni mwao, waliomwambia Ishmaeli, Usituue; kwa maana tuna akiba zetu zilizofichwa kondeni, za ngano, na shayiri, na mafuta, na asali. Basi, akawaacha, asiwaue watu hao pamoja na ndugu zao.
Job 2.4 Proverbes 13.8 Marc 8.36-8.37 Philippiens 3.7-3.9 Psaumes 49.6-49.8
9 Basi, shimo lile, ambalo Ishmaeli ameitupa mizoga ya watu aliowaua, karibu na Gedalia, (ni lile lile alilolichimba Asa, mfalme, kwa kuwa alimwogopa Baasha, mfalme wa Israeli), Ishmaeli, mwana wa Nethania, akalijaza kwa watu wale aliowaua.
Juges 6.2 Hébreux 11.38 1 Rois 15.17-15.22 1 Samuel 13.6 2 Samuel 17.9
10 Kisha Ishmaeli akawachukua mateka watu wote waliosalia, waliokuwa huko Mizpa, yaani, binti za mfalme, na watu wote waliobaki Mizpa, ambao Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, alikuwa amemkabidhi Gedalia, mwana wa Ahikamu; Ishmaeli, mwana wa Nethania, akawachukua mateka. akaondoka, ili awaendee wana wa Amoni.
Jérémie 40.14 Jérémie 40.7 Néhémie 2.10 Jérémie 40.11-40.12 Néhémie 2.19
11 Lakini Yohana, mwana wa Karea, na maakida wote wa majeshi waliokuwa pamoja naye, waliposikia habari za hayo mabaya yote aliyoyatenda Ishmaeli, mwana wa Nethania,
Jérémie 40.7-40.8 Jérémie 40.13-40.16 Jérémie 43.2-43.5 Jérémie 42.1 Jérémie 41.7
12 wakawatwaa watu wote, wakaenda ili kupigana na Ishmaeli, mwana wa Nethania, nao wakampata karibu na maji makuu ya Gibeoni.
2 Samuel 2.13 Genèse 14.14-14.16 1 Samuel 30.1-30.8 1 Samuel 30.18-30.20
13 Basi, ikawa, watu wote waliokuwa pamoja na Ishmaeli, walipomwona Yohana, mwana wa Karea, na hao maakida wote wa majeshi waliokuwa pamoja naye, ndipo wakafurahi.
14 Basi, watu wote, ambao Ishmaeli amewachukua mateka kutoka Mizpa, wakazunguka, wakarudi, wakamwendea Yohana, mwana wa Karea.
15 Lakini Ishmaeli, mwana wa Nethania, akaokoka pamoja na watu wanane, Yohana asimpate, akawaendea wana wa Amoni.
Proverbes 28.17 Job 21.30 1 Rois 20.20 1 Samuel 30.17 2 Rois 25.25
16 Ndipo Yohana, mwana wa Karea, na maakida wote wa majeshi waliokuwa pamoja naye, wakawatwaa hao watu wote waliosalia, aliowapata tena katika mikono ya Ishmaeli, mwana wa Nethania, huko Mizpa, baada ya kumwua Gedalia, mwana wa Ahikamu, yaani, watu wa vita, na wanawake na watoto, na matowashi, aliowarudisha toka Gibeoni;
Jérémie 43.4-43.7 Jérémie 42.8 Jérémie 41.10
17 wakaenda zao, wakakaa katika Geruthi Kimhamu, ulio karibu na Bethlehemu, ili wapate kuingia Misri,
Jérémie 42.14 2 Samuel 19.37-19.38 Jérémie 42.19 Esaïe 30.2-30.3 Jérémie 43.7
18 kwa sababu ya Wakaldayo; maana waliwaogopa, kwa sababu Ishmaeli, mwana wa Nethania, amemwua Gedalia, mwana wa Ahikamu, ambaye mfalme wa Babeli amemweka kuwa liwali juu ya nchi.
Jérémie 40.5 Luc 12.4-12.5 Jérémie 42.16 Jérémie 42.11 Esaïe 57.11

Cette Bible est dans le domaine public.