Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 34.5
Bible en Swahili de l’est


Prophétie sur le sort de Sédécias

1 Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, hapo Nebukadreza, mfalme wa Babeli, na jeshi lake lote, na falme zote za dunia zilizokuwa chini ya mamlaka yake, na kabila zote za watu, walipopigana na Yerusalemu, na miji yake yote, kusema,
Jérémie 1.15 Daniel 2.37-2.38 Jérémie 32.2 Jérémie 52.4-52.11 Jérémie 27.5-27.7
2 Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Enenda ukaseme na Sedekia, mfalme wa Yuda, ukamwambie, Bwana asema hivi, Tazama, nitatia mji huu katika mikono ya mfalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto;
Jérémie 21.10 Jérémie 34.22 2 Chroniques 36.11-36.12 Jérémie 32.3 Jérémie 22.1-22.2
3 tena wewe hutaokoka mkononi mwake, lakini utakamatwa kweli kweli, na kutiwa katika mikono yake; na macho yako yatayatazama macho ya mfalme wa Babeli, naye atasema nawe mdomo kwa mdomo, nawe utakwenda Babeli.
Jérémie 32.4 Jérémie 21.7 Jérémie 34.21 2 Rois 25.4-25.7 Ezéchiel 12.13
4 Hata hivyo lisikie neno la Bwana, Ee Sedekia, mfalme wa Yuda; Bwana asema hivi katika habari zako; hutakufa kwa upanga;
5 utakufa katika amani; na kwa mafukizo ya baba zako, wafalme wa zamani waliokutangulia, ndivyo watakavyokufukizia; nao watakulilia, Aa, Bwana! Kwa maana mimi nimelinena neno hili, asema Bwana.
Jérémie 22.18 2 Chroniques 16.14 Ezéchiel 17.16 2 Chroniques 21.19-21.20 Daniel 2.46
6 Basi Yeremia, nabii, akamwambia Sedekia, mfalme wa Yuda, maneno hayo yote katika Yerusalemu,
1 Samuel 15.16-15.24 1 Samuel 3.18 2 Samuel 12.7-12.12 Matthieu 14.4 1 Rois 21.19
7 wakati ule jeshi la Babeli walipopigana na Yerusalemu na miji yote ya Yuda iliyosalia, na Lakishi, na Azeka; kwa maana miji hiyo tu ndiyo iliyosalia katika miji ya Yuda yenye maboma.
Josué 10.3 2 Chroniques 11.5-11.10 Jérémie 4.5 2 Rois 18.13-18.14 Josué 15.35

Le refus d’affranchir les esclaves

8 Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, baada ya wakati ule mfalme Sedekia alipofanya agano na watu wote waliokuwa katika Yerusalemu, kuwatangazia habari ya uhuru;
Lévitique 25.10 2 Rois 11.17 Jérémie 34.17 Néhémie 5.1-5.13 2 Rois 23.2-23.3
9 ya kwamba kila mtu amweke huru mtumwa wake, na kila mtu amweke huru mjakazi wake, ikiwa yule mwanamume au yule mwanamke ni Mwebrania; mtu ye yote asiwatumikishe, yaani, asimtumikishe Myahudi, nduguye;
Exode 2.6 Genèse 14.13 Lévitique 25.39-25.46 Jérémie 30.8 Philippiens 3.5
10 na wakuu wote, na watu wote, wakati, waliofanya agano hilo, ya kwamba kila mtu amweke huru mtumwa wake na mjakazi wake, mtu ye yote asiwatumikishe tena; wakatii, wakawaacha.
Jérémie 26.16 Jérémie 26.10 Marc 6.20 Jérémie 36.12 Jérémie 3.10-3.11
11 Lakini baadaye wakaghairi, wakawarudisha watumwa wale, na wajakazi wale, ambao wamewaacha huru, nao wakawatia utumwani wawe watumwa na wajakazi wao.
1 Samuel 19.6-19.11 Ecclésiaste 8.11 Osée 6.4 Romains 2.4-2.5 Sophonie 1.6
12 Basi, neno la Bwana likamjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, kusema,
13 Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nalifanya agano na baba zenu, siku ile nilipowatoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa, nikisema,
Josué 24.17 Juges 6.8 Deutéronome 5.2-5.3 Exode 24.7-24.8 Exode 24.3
14 Mwisho wa kila mwaka wa saba kila mtu na amweke huru ndugu yake aliye Mwebrania, aliyeuzwa kwako na kukutumikia miaka sita utamwacha atoke kwako huru, lakini baba zenu hawakunisikiliza, wala hawakutega masikio yao.
Deutéronome 15.12 1 Samuel 8.7-8.8 1 Rois 9.22 2 Rois 17.13-17.14 Amos 2.6
15 Na ninyi mlikuwa mmegeuka, mkafanya yaliyo haki machoni pangu, kwa kumtangazia uhuru kila mtu ndugu yake; nanyi mlikuwa mmefanya agano mbele zangu, katika nyumba ile iitwayo kwa jina langu;
Jérémie 34.8 2 Rois 23.3 Néhémie 10.29 Jérémie 7.10-7.11 Jérémie 32.34
16 lakini mlighairi, na kulitukana jina langu; kila mtu akamrudisha mtumwa wake na mjakazi wake, ambao mmewaweka huru kama walivyopenda wenyewe, mkawatia utumwani tena, wawe watumwa wenu na wajakazi wenu.
Lévitique 19.12 Exode 20.7 Ezéchiel 3.20 Jérémie 34.11 Ezéchiel 18.24
17 Basi Bwana asema hivi, Hamkunisikiliza kumtangazia uhuru kila mtu ndugu yake, na kila mtu jirani yake; tazama, mimi nawatangazieni uhuru, asema Bwana, yaani, wa upanga, na njaa, na tauni; nami nitawatoa ninyi mtupwe huko na huko katika falme zote za dunia.
Matthieu 7.2 Deutéronome 28.25 Jérémie 29.18 Galates 6.7 Jérémie 15.4
18 Na watu hao waliolivunja agano langu, wasioyatimiza maneno ya agano lile, walilolifanya mbele zangu, wakati ule walipomkata ndama vipande viwili, wakapita katikati ya vipande vile;
Genèse 15.10 Osée 6.7 Deutéronome 17.2 Osée 8.1 Genèse 15.17-15.18
19 wakuu wa Yuda, na wakuu wa Yerusalemu, matowashi, na makuhani, na watu wote wa nchi, waliopita katikati ya vipande vile vya huyo ndama;
Sophonie 3.3-3.4 Jérémie 29.2 Jérémie 34.10 Daniel 9.6 Ezéchiel 22.27-22.31
20 mimi nitawatia katika mikono ya adui zao, na katika mikono ya watu wale wanaowatafuta roho zao, na mizoga yao itakuwa ni chakula cha ndege za mbinguni, na cha wanyama wakali wa nchi.
Jérémie 7.33 Jérémie 11.21 Jérémie 22.25 Jérémie 21.7 Jérémie 16.4
21 Na Sedekia, mfalme wa Yuda, na wakuu wake nitawatia katika mikono ya adui zao, na katika mikono ya watu wale wanaowatafuta roho zao, na katika mikono ya jeshi la mfalme wa Babeli, waliokwenda zao na kuwaacheni.
Jérémie 52.24-52.27 Jérémie 39.6 Ezéchiel 17.16 2 Rois 25.18-25.21 Jérémie 52.10
22 Tazama, nitawapa amri yangu, asema Bwana, na kuwarejeza kwenye mji huu; nao watapigana nao, na kuutwaa, na kuuteketeza kwa moto; nami nitaifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa, isikaliwe na mtu.
Jérémie 9.11 Jérémie 39.8 Jérémie 39.1-39.2 Jérémie 33.10 Jérémie 44.22

Cette Bible est dans le domaine public.