Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 33.18
Bible en Swahili de l’est


Promesses de restauration

1 Tena, neno la Bwana likamjia Yeremia mara ya pili, hapo alipokuwa akali amefungwa katika uwanda wa walinzi, kusema,
Jérémie 37.21 Jérémie 38.28 Jérémie 32.8 Jérémie 32.2-32.3 2 Timothée 2.9
2 Bwana alitendaye jambo hili, Bwana aliumbaye ili alithibitishe; Bwana ndilo jina lake; asema hivi,
Exode 15.3 Exode 6.3 Esaïe 37.26 Psaumes 102.16 Apocalypse 21.2
3 Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.
Jérémie 29.12 Esaïe 48.6 Deutéronome 4.29 Esaïe 65.24 Ephésiens 3.20
4 Maana Bwana, Mungu wa Israeli asema hivi, katika habari za nyumba za mji huu, na katika habari za nyumba za wafalme wa Yuda, zilizobomolewa ili kuyapinga maboma na upanga;
Jérémie 32.24 Habakuk 1.10 Ezéchiel 4.2 Ezéchiel 21.22 Ezéchiel 26.8
5 Wanakuja kupigana na Wakaldayo, lakini ni kuzijaza kwa mizoga ya watu, niliowaua katika hasira yangu na ghadhabu yangu, ambao kwa ajili ya uovu wao wote nimeuficha mji huu uso wangu.
Esaïe 8.17 Jérémie 21.4-21.7 Jérémie 32.5 Jérémie 21.10 Michée 3.4
6 Tazama, nitauletea afya na kupona, nami nitawaponya; nami nitawafunulia wingi wa amani na kweli.
Esaïe 30.26 Tite 3.5-3.6 Jean 10.10 Esaïe 26.2-26.4 Galates 5.22-5.23
7 Nami nitawarudisha wafungwa wa Yuda, na wafungwa wa Israeli, na kuwajenga kama kwanza.
Jérémie 30.3 Esaïe 1.26 Amos 9.14-9.15 Jérémie 31.4 Jérémie 32.44
8 Nami nitawasafisha na uovu wao wote, ambao kwa huo wamenitenda dhambi; nami nitawasamehe maovu yao yote, ambayo kwayo wamenitenda dhambi, na kukosa juu yangu.
Zacharie 13.1 Jérémie 31.34 Psaumes 51.2 Ezéchiel 36.25 Esaïe 44.22
9 Na mji huu utakuwa kwangu jina la furaha, na sifa na utukufu, mbele ya mataifa yote ya dunia, watakaosikia habari ya mema yote niwatendeayo, nao wataogopa na kutetemeka, kwa sababu ya mema yote na amani nitakaoupatia mji huo.
Esaïe 60.5 Esaïe 62.7 Jérémie 13.11 Sophonie 3.17-3.20 Néhémie 6.16
10 Bwana asema hivi, katika mahali hapo ambapo mnasema kwamba ni ukiwa, hapana mwanadamu wala mnyama, naam, katika miji ya Yuda na katika njia za Yerusalemu, zilizo ukiwa, hazina mwanadamu wala mwenyeji wala mnyama,
Jérémie 32.43 Ezéchiel 37.11 Jérémie 32.36
11 itasikilikana tena sauti ya furaha na sauti ya shangwe, sauti ya bwana arusi na sauti ya bibi arusi, sauti yao wasemao Mshukuruni Bwana wa majeshi, maana Bwana ni mwema, rehema zake ni za milele; na sauti zao waletao sadaka za shukrani nyumbani kwa Bwana. Kwa kuwa nitawarudisha wafungwa wa nchi hii kama kwanza, asema Bwana.
1 Chroniques 16.34 Psaumes 106.1 Psaumes 107.1 Psaumes 107.22 1 Chroniques 16.8
12 Bwana wa majeshi asema hivi, Katika mahali hapa, palipo ukiwa, hapana mwanadamu wala mnyama, na katika miji yake yote, yatakuwapo makao ya wachungaji wakizilaza kondoo zao.
Esaïe 65.10 Jérémie 51.62 Jérémie 31.24 Jérémie 36.29 Sophonie 2.6-2.7
13 Katika miji ya nchi ya vilima, katika miji ya nchi tambarare, katika miji ya Negebu, na katika nchi ya Benyamini, na katika mahali palipo karibu na Yerusalemu, na katika miji ya Yuda, makundi ya kondoo yatapita tena chini ya mikono yake awahesabuye, asema Bwana.
Lévitique 27.32 Jérémie 17.26 Luc 15.4 Jean 10.3-10.4

Des alliances irrévocables

14 Tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapolitimiza neno lile jema nililolinena, katika habari za nyumba ya Israeli, na katika habari za nyumba ya Yuda.
Jérémie 29.10 Aggée 2.6-2.9 Jérémie 23.5 Esaïe 32.1-32.2 Ezéchiel 34.23-34.25
15 Katika siku zile, na wakati ule, nitamchipushia Daudi Chipukizi la haki; naye atafanya hukumu na haki katika nchi hii.
Esaïe 4.2 Esaïe 11.1-11.5 Jérémie 23.5-23.6 Zacharie 6.12-6.13 Zacharie 3.8
16 Katika siku zile Yuda ataokolewa, na Yerusalemu utakaa salama, na jina lake atakaloitwa ni hili, Bwana ni haki yetu.
Jérémie 23.6 Esaïe 45.17 1 Corinthiens 1.30 Esaïe 45.24-45.25 2 Corinthiens 5.21
17 Maana Bwana asema hivi, Daudi hatakosa kuwa na mtu wa kuketi katika kiti cha enzi cha nyumba ya Israeli;
1 Rois 2.4 Psaumes 89.29-89.37 1 Rois 8.25 1 Chroniques 17.11-17.14 2 Samuel 3.29
18 wala makuhani Walawi hawatakosa kuwa na mtu wa kusimama mbele zangu, na kutoa sadaka za kuteketezwa, na kufukiza matoleo, na kufanya dhabihu daima.
Romains 1.21 1 Pierre 2.9 1 Pierre 2.5 Ezéchiel 45.5 Ezéchiel 44.9-44.11
19 Neno la Bwana likamjia Yeremia, kusema,
20 Bwana asema hivi, Kama mkiweza kulivunja agano langu la mchana, na agano langu la usiku, hata usiwepo tena mchana na usiku kwa wakati wake,
Psaumes 104.19-104.23 Jérémie 33.25-33.26 Esaïe 54.9-54.10 Psaumes 89.37 Genèse 8.22
21 ndipo agano langu nililolifanya na Daudi, mtumishi wangu, laweza kuvunjika, hata asiwe na mwana wa kumiliki katika kiti chake cha enzi; tena agano langu nililofanya na Walawi makuhani, wahudumu wangu, laweza kuvunjika.
Psaumes 89.34 2 Chroniques 7.18 2 Samuel 23.5 2 Chroniques 21.7 Luc 1.69-1.70
22 Kama vile jeshi la mbinguni haliwezi kuhesabiwa, wala mchanga wa bahari kupimwa; ndivyo nitakavyoongeza wazao wa Daudi, mtumishi wangu, na Walawi wanaonihudumia.
Genèse 22.17 Genèse 15.5 Ezéchiel 37.24-37.27 Hébreux 11.12 Esaïe 66.21
23 Kisha neno la Bwana likamjia Yeremia, kusema,
24 Je! Hufikiri neno hili walilolisema watu hawa, wakinena, Jamaa zile mbili alizozichagua Bwana amezitupilia mbali? Hivyo ndivyo wanavyowadharau watu wangu, ili wasiwe taifa tena mbele yao.
Néhémie 4.2-4.4 Psaumes 44.13-44.14 Psaumes 83.4 Ezéchiel 26.2 Jérémie 33.21-33.22
25 Bwana asema hivi, Ikiwa agano langu la mchana na usiku halikai imara, ikiwa mimi sikuziamuru kawaida za mbingu na dunia;
Psaumes 74.16-74.17 Jérémie 31.35-31.36 Jérémie 33.20 Genèse 8.22 Psaumes 104.19
26 ndipo nitawatupilia mbali wazao wa Yakobo, na Daudi, mtumishi wangu, hata nisitwae wazao wake watawale juu ya wazao wa Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo; kwa maana nitawarudisha wafungwa wao, nami nitawarehemu.
Jérémie 31.37 Esaïe 14.1 Osée 2.23 Ezéchiel 39.25 Esaïe 54.8

Cette Bible est dans le domaine public.