Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 26.7
Bible en Swahili de l’est


Jérémie menacé de mort

1 Mwanzo wa kumiliki kwake Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, neno hili lilitoka kwa Bwana, kusema,
Jérémie 27.1 2 Chroniques 36.4-36.5 Jérémie 36.1 Jérémie 1.3 Jérémie 35.1
2 Bwana asema hivi, Simama katika uwanja wa nyumba ya Bwana, useme na miji yote ya Yuda, wajao ili kuabudu katika nyumba ya Bwana; sema nao maneno yote ninayokuamuru kuwaambia, usizuie hata neno moja.
Actes 20.27 Deutéronome 4.2 Jérémie 19.14 Jérémie 1.17 Matthieu 28.20
3 Labda watasikia, na kughairi na kuacha kila mtu njia yake mbaya; ili niyaghairi mabaya niliyokusudia kuwatenda, kwa sababu ya uovu wa matendo yao.
Jérémie 36.3 Jérémie 18.7-18.10 Esaïe 1.16-1.19 1 Rois 21.27 Ezéchiel 18.27-18.30
4 Nawe utawaambia, Bwana asema hivi, Kama hamtaki kunisikia, kwenda katika sheria yangu, niliyoiweka mbele yenu,
1 Rois 9.6 Jérémie 44.10 Esaïe 1.20 Deutéronome 28.15-28.68 Esaïe 42.23-42.25
5 kuyasikiliza maneno ya watumishi wangu, manabii, ninaowatuma kwenu, naam, nikiondoka mapema na kuwatuma; lakini ninyi hamkuwasikiliza;
Jérémie 25.3-25.4 Jérémie 7.13 2 Rois 9.7 Esdras 9.11 Apocalypse 11.18
6 basi, nitafanya nyumba hii kuwa kama Shilo, na mji huu nitaufanya kuwa laana kwa taifa zote za dunia.
2 Rois 22.19 Jérémie 24.9 Jérémie 25.18 Esaïe 65.15 Jérémie 7.12-7.14
7 Na makuhani, na manabii, na watu wote, wakamsikia Yeremia, hapo aliposema maneno haya katika nyumba ya Bwana.
Michée 3.11 Jérémie 5.31 Sophonie 3.4 Actes 4.1-4.6 Matthieu 21.15
8 Ikawa, Yeremia alipokuwa amekwisha kusema maneno yote Bwana aliyomwamuru kuwaambia watu wote, ndipo hao makuhani, na manabii, na watu wote, wakamkamata, wakisema, Bila shaka utakufa.
Lamentations 4.13-4.14 Jérémie 2.30 Actes 5.33 Actes 7.52 Matthieu 22.6
9 Kwa nini umetabiri kwa jina la Bwana, ukisema, Nyumba hii itakuwa kama Shilo, na mji huu utakuwa ukiwa, hautakaliwa na mtu? Watu wote wakamkusanyikia Yeremia katika nyumba ya Bwana.
Actes 17.5-17.8 Actes 13.50 Matthieu 21.23 Actes 6.14 2 Chroniques 25.16
10 Na wakuu wa Yuda waliposikia habari za mambo haya, wakatoka katika nyumba ya mfalme, wakapanda juu mpaka nyumbani kwa Bwana; wakaketi, hapo watu waingiapo katika lango jipya la nyumba ya Bwana.
Jérémie 36.10 Jérémie 36.25 Jérémie 38.4-38.6 Jérémie 26.16-26.17 Jérémie 36.12-36.19
11 Ndipo hapo makuhani, na manabii, wakawaambia wakuu na watu wote, wakisema, Mtu huyu amestahili kufa, kwa sababu ametabiri juu ya mji huu, kama mlivyosikia kwa masikio yenu.
Jérémie 38.4 Deutéronome 18.20 Matthieu 26.66 Actes 6.11-6.14 Actes 22.22
12 Ndipo Yeremia akawaambia wakuu wote na watu wote, akisema, Bwana ndiye aliyenituma kutabiri juu ya nyumba hii, na juu ya mji huu, maneno hayo yote mliyoyasikia.
Actes 5.29 Jérémie 26.15 Actes 4.19 Jérémie 26.2 Jérémie 1.17-1.18
13 Basi sasa, tengenezeni njia zenu, na matendo yenu, mkaisikilize sauti ya Bwana, Mungu wenu; naye Bwana atayaghairi mabaya aliyoyanena juu yenu.
Jonas 4.2 Jérémie 35.15 Jonas 3.9 Joël 2.14 Jérémie 18.8
14 Lakini kwangu mimi, tazama, mimi nipo hapa mikononi mwenu; nitendeni myaonayo kuwa mema na haki mbele ya macho yenu.
Jérémie 38.5 Josué 9.25 Daniel 3.16 2 Samuel 15.26
15 Lakini jueni yakini ya kuwa, mkiniua, mtajiletea juu yenu damu isiyo na hatia itakuwa juu yenu, na juu ya mji huu, na juu ya wenyeji wake; kwa maana ni kweli Bwana amenituma kwenu, kuwaambieni yote mliyoyasikia.
Jérémie 7.6 Proverbes 6.17 Nombres 35.33 2 Rois 24.4 Matthieu 23.30-23.36
16 Ndipo wakuu na watu wote wakawaambia makuhani, na manabii, wakisema, Mtu huyu hastahili kuuawa; kwa maana amesema nasi katika jina la Bwana Mungu wetu.
Actes 5.34-5.39 Actes 23.9 Actes 23.29 Jérémie 36.25 Actes 25.25
17 Ndipo watu kadha wa kadha miongoni mwa wazee wa nchi wakaondoka, wakanena na mkutano wa watu, wakisema,
Actes 5.34 Michée 1.1
18 Mikaya Mmorashti, alitabiri katika siku za Hezekia, mfalme wa Yuda; akasema na watu wote wa Yuda, ya kwamba, Bwana wa majeshi asema hivi, Sayuni utalimwa kama shamba lilimwavyo, na Yerusalemu utakuwa magofu, na mlima wa nyumba utakuwa kama mahali palipoinuka msituni.
Néhémie 4.2 Jérémie 9.11 Zacharie 8.3 Michée 1.1 Jérémie 17.3
19 Je! Hezekia, mfalme wa Yuda, na watu wote wa Yuda, walimwua Mikaya? Je! Hakumcha Bwana, na kumwomba Bwana awafadhili; naye Bwana akaghairi, asiyatende mabaya yale aliyoyatamka juu yao? Na sisi tungetenda mabaya makuu juu ya roho zetu.
Exode 32.14 2 Samuel 24.16 Esaïe 37.15-37.20 2 Chroniques 29.6-29.11 2 Chroniques 32.25-32.26
20 Tena, kulikuwa na mtu aliyetabiri katika jina la Bwana, Uria, mwana wa Shemaya, wa Kiriath-Yearimu; yeye naye alitabiri juu ya mji huu, na juu ya nchi hii, sawasawa na maneno yote ya Yeremia;
1 Samuel 7.2 Josué 9.17 1 Samuel 6.21 Josué 15.60 Josué 18.14
21 na Yehoyakimu, mfalme, na mashujaa wake wote, na wakuu wake wote, waliposikia maneno yake, mfalme akataka kumwua; lakini Uria alipopata habari, aliogopa, akakimbia akaenda Misri.
Matthieu 10.23 Matthieu 14.5 2 Chroniques 16.10 Jérémie 36.26 1 Rois 19.1-19.3
22 Basi, mfalme Yehoyakimu akatuma watu waende Misri, Elnathani, mwana wa Akbori, na watu wengine pamoja naye, kwenda Misri;
Jérémie 36.12 2 Rois 22.14 2 Rois 22.12 Jérémie 36.25 Psaumes 12.8
23 wakamtoa Uria katika Misri, wakamleta kwa Yehoyakimu, mfalme; naye akamwua kwa upanga, akamtupa yule maiti katika makaburi ya watu wasio na cheo.
Jérémie 2.30 1 Thessaloniciens 2.15 Jérémie 26.15 Jérémie 36.30 Matthieu 23.34-23.35
24 Lakini mkono wa Ahikamu, mwana wa Shafani, alikuwa pamoja na Yeremia, wasimtie katika mikono ya watu auawe.
2 Rois 22.12-22.14 1 Rois 18.4 Jérémie 39.14 Jérémie 40.5-40.7 Jérémie 1.18-1.19

Cette Bible est dans le domaine public.