Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 66.11
Bible en Swahili de l’est


Gloire de la Jérusalem future

1 Bwana asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?
Matthieu 5.34-5.35 Actes 7.48-7.50 Actes 17.24 1 Rois 8.27 Psaumes 11.4
2 Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema Bwana; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.
Esaïe 57.15 Psaumes 34.18 Matthieu 5.3-5.4 Luc 18.13-18.14 Esaïe 66.5
3 Yeye achinjaye ng’ombe ni kama yeye amwuaye mtu; na yeye atoaye dhabihu ya mwana-kondoo ni kama yeye avunjaye shingo ya mbwa; na yeye atoaye matoleo ni kama yeye atoaye damu ya nguruwe; na yeye afukizaye uvumba ni kama yeye abarikiye sanamu; naam, wamezichagua njia zao wenyewe, na nafsi zao zafurahia machukizo yao.
Lévitique 2.2 Proverbes 15.8 Esaïe 57.17 Juges 10.14 Amos 5.21-5.22
4 Mimi nami nitachagua mapigo yao, nitaleta hofu zao juu yao; kwa sababu nilipoita, hawakuitika; na niliponena, hawakusikia; bali walifanya yaliyo maovu machoni pangu, na kuyachagua nisiyoyafurahia.
Esaïe 65.12 2 Rois 21.6 Proverbes 1.24 2 Rois 21.2 Jérémie 7.13
5 Lisikilizeni neno la Bwana, ninyi mtetemekao kwa sababu ya neno lake; Ndugu zenu wawachukiao ninyi, waliowatupa kwa ajili ya jina langu, wamesema, Na atukuzwe Bwana, tupate kuiona furaha yenu; lakini watatahayarika.
Psaumes 38.20 Esaïe 66.2 Matthieu 5.10-5.12 Matthieu 10.22 Jean 15.18-15.20
6 Sauti ya fujo itokayo mjini! Sauti itokayo hekaluni! Sauti ya Bwana awalipaye adui zake adhabu!
Esaïe 59.18 Amos 1.2 Esaïe 65.5-65.7 Joël 3.7-3.16 Esaïe 34.8
7 Kabla hajaona utungu alizaa; Kabla maumivu yake hayajampata, Alizaa mtoto mwanamume.
Esaïe 54.1 Apocalypse 12.1-12.5 Galates 4.26
8 Ni nani aliyesikia neno kama hili? Ni nani aliyeona mambo kama haya? Je! Nchi yaweza kuzaliwa siku moja? Taifa laweza kuzaliwa mara? Maana Sayuni, mara alipoona utungu, Alizaa watoto wake.
Esaïe 64.4 Actes 21.20 Esaïe 49.20-49.22 Romains 15.18-15.21 Actes 2.41
9 Je! Mimi nilete wana karibu na kuzaliwa, nisizalishe? Asema Bwana; mimi nizalishaye, je! Nilifunge tumbo? Asema Mungu wako.
Esaïe 37.3 Genèse 18.14
10 Furahini pamoja na Yerusalemu, shangilieni kwa ajili yake, ninyi nyote mmpendao; furahini pamoja naye kwa furaha, ninyi nyote mliao kwa ajili yake;
Deutéronome 32.43 Psaumes 26.8 Esaïe 65.18 Psaumes 137.6 Psaumes 122.6
11 mpate kunyonya, na kushibishwa kwa maziwa ya faraja zake, mpate kukama, na kufurahiwa kwa wingi wa utukufu wake.
Esaïe 60.16 Joël 3.18 Esaïe 60.5 Psaumes 36.8 1 Pierre 2.2
12 Maana Bwana asema hivi, Tazama, nitamwelekezea amani kama mto, na utukufu wa mataifa kama kijito kifurikacho, nanyi mtapata kunyonya; mtabebwa; na juu ya magoti mtabembelezwa.
Esaïe 48.18 Esaïe 60.16 Esaïe 54.3 Esaïe 60.4-60.14 Esaïe 66.19-66.20
13 Mfano wa mtu ambaye mama yake amfariji, ndivyo nitakavyowafariji ninyi; nanyi mtafarijiwa katika Yerusalemu.
Esaïe 51.3 1 Thessaloniciens 2.7 Psaumes 137.6 Esaïe 66.10 2 Corinthiens 1.4
14 Nanyi mtaona, na mioyo yenu itafurahi, na mifupa yenu itasitawi kama majani mabichi; na mkono wa Bwana utajulikana, uwaelekeao watumishi wake, naye atawaonea adui zake ghadhabu.
Esdras 8.31 Zacharie 10.7 Proverbes 17.22 Esdras 8.22 Proverbes 3.8
15 Maana Bwana atakuja na moto, na magari yake ya vita kama upepo wa kisulisuli; ili atoe malipo ya ghadhabu yake kwa moto uwakao, na maonyo yake kwa miali ya moto.
Psaumes 68.17 Esaïe 30.33 2 Thessaloniciens 1.6-1.9 Esaïe 30.27-30.28 Daniel 11.40
16 Kwa maana Bwana atateta na wote wenye mwili, kwa moto na kwa upanga wake; nao watakaouawa na Bwana watakuwa wengi.
Esaïe 27.1 Ezéchiel 38.21-38.22 Apocalypse 19.11-19.21 Ezéchiel 39.2-39.10 Esaïe 34.5-34.10
17 Watu wale wajitakasao, na kujisafisha katika bustani, nyuma yake aliye katikati; wakila nyama ya nguruwe, na machukizo, na panya; watakoma pamoja, asema Bwana.
Esaïe 65.3-65.4 Lévitique 11.2-11.8 Deutéronome 14.3-14.8 Esaïe 1.28-1.29
18 Nami nayajua matendo yao na mawazo yao; wakati unakuja nitakapokusanya mataifa yote na lugha zote; nao watakuja, nao watauona utukufu wangu.
Deutéronome 31.21 Esaïe 2.2 Psaumes 72.11 Amos 5.12 Psaumes 86.9
19 Nami nitaweka ishara kati yao, nami nitawatuma hao waliookoka kwa mataifa, Tarshishi, na Puli, na Ludi, wavutao upinde, kwa Tubali na Yavani, visiwa vilivyo mbali; watu wasioisikia habari yangu, wala kuuona utukufu wangu; nao watahubiri utukufu wangu katika mataifa.
Esaïe 52.15 Ezéchiel 27.10 Romains 15.21 Esaïe 55.5 Esaïe 62.10
20 Nao watawaleta ndugu zenu wote kutoka mataifa yote, kuwa sadaka kwa Bwana, juu ya farasi, na katika magari, na katika machela, na juu ya nyumbu, na juu ya wanyama wepesi, mpaka mlima wangu mtakatifu Yerusalemu, asema Bwana; kama vile wana wa Israeli waletavyo sadaka yao nyumbani kwa Bwana katika chombo safi.
Esaïe 43.6 Esaïe 60.3-60.14 Esaïe 56.7 Esaïe 65.11 Romains 15.16
21 Na baadhi ya hao nitawatwaa kuwa makuhani na Walawi, asema Bwana.
1 Pierre 2.9 Esaïe 61.6 Exode 19.6 1 Pierre 2.5 Apocalypse 1.6
22 Kama vile mbingu mpya na nchi mpya, nitakazofanya, zitakavyokaa mbele zangu, asema Bwana, ndivyo uzao wenu na jina lenu litakavyokaa.
Esaïe 65.17 Apocalypse 21.1 2 Pierre 3.13 1 Pierre 1.4-1.5 Jean 10.27-10.29
23 Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana.
Ezéchiel 46.1 Psaumes 86.9 Esaïe 1.13-1.14 Zacharie 14.16 Ezéchiel 46.6
24 Nao watatoka nje na kuitazama mizoga ya watu walioniasi; maana funza wao hatakufa, wala moto wao hautazimika nao watakuwa chukizo machoni pa wote wenye mwili.
Esaïe 14.11 Marc 9.43-9.49 Daniel 12.2 Apocalypse 14.10-14.11 Matthieu 3.12

Cette Bible est dans le domaine public.