Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 46.12
Bible en Swahili de l’est


Action souveraine de Dieu

1 Beli anaanguka chini, Nebo anainama; sanamu zao ziko juu ya wanyama, na juu ya ng’ombe; vitu vile mlivyokuwa mkivichukua huku na huku vimekuwa mzigo, mzigo wa kumlemea mnyama aliyechoka.
Esaïe 21.9 Jérémie 50.2 Jérémie 51.44 Esaïe 2.20 Exode 12.12
2 Wanajiinamisha, wanainama pamoja; hawakuweza kuutua mzigo, bali wao wenyewe wamekwenda kufungwa.
Jérémie 48.7 Juges 18.17-18.18 2 Samuel 5.21 Juges 18.24 Jérémie 43.12-43.13
3 Nisikilizeni, enyi wa nyumba ya Yakobo, ninyi mlio mabaki ya nyumba ya Israeli, mliochukuliwa nami tangu tumboni, mlioinuliwa tangu mimbani;
Deutéronome 1.31 Esaïe 10.22 Psaumes 71.6 Psaumes 22.9-22.10 Ezéchiel 16.6-16.16
4 na hata uzee wenu mimi ndiye, na hata wakati wenu wa mvi nitawachukueni; nimefanya, nami nitachukua; naam, nitachukua na kuokoa.
Psaumes 71.18 Romains 11.29 Esaïe 43.13 Psaumes 92.14 Psaumes 48.14
5 Mtanifananisha na nani, na kunisawazisha naye, na kunilinganisha naye, ili tuwe sawasawa?
Esaïe 40.18 Esaïe 40.25 Colossiens 1.15 Hébreux 1.3 Exode 15.11
6 Watu wamwagao dhahabu kutoka mfukoni, na kupima fedha katika mizani, huajiri mfua dhahabu, akaifanya mungu; huanguka, naam, huabudu.
Daniel 3.5-3.15 Juges 17.3-17.4 Exode 32.2-32.4 Actes 17.29 Jérémie 10.9
7 Humchukua begani, humchukua, wakamsimamisha mahali pake, akasimama; hataondoka katika mahali pake, naam, mmoja atamwita, lakini hawezi kujibu, wala kumwokoa na taabu yake.
Esaïe 45.20 Jérémie 10.5 Daniel 3.1 Jérémie 2.28 Jonas 1.5
8 Kumbukeni haya, mkajionyeshe kuwa waume; jifahamisheni haya, ninyi mkosao;
Psaumes 115.8 Esaïe 47.7 1 Corinthiens 14.20 Esaïe 44.18-44.21 Aggée 1.5
9 kumbukeni mambo ya zamani za kale; maana mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi;
Deutéronome 32.7 Esaïe 65.17 Psaumes 111.4 Esaïe 42.9 Deutéronome 33.26
10 nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.
Proverbes 19.21 Psaumes 33.11 Proverbes 21.30 Esaïe 43.13 Hébreux 6.17
11 Nikiita ndege mkali kutoka mashariki, mtu wa shauri langu toka nchi iliyo mbali; naam, nimenena, nami nitatekeleza; nimekusudia, nami nitafanya.
Nombres 23.19 Esaïe 41.2 Psaumes 119.24 Esaïe 14.24-14.27 Ephésiens 1.11
12 Nisikilizeni, ninyi mlio na moyo mshupavu, mlio mbali na haki;
Esaïe 46.3 Psaumes 119.150 Jérémie 2.5 Ephésiens 2.13 Esaïe 48.4
13 Mimi ninaleta karibu haki yangu, haitakuwa mbali, na wokovu wangu hautakawia; nami nitaweka wokovu katika Sayuni kwa ajili ya Israeli, utukufu wangu.
Esaïe 61.3 Esaïe 51.5 Esaïe 62.11 Esaïe 44.23 Esaïe 12.2

Cette Bible est dans le domaine public.