Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 43.26
Bible en Swahili de l’est


Dieu, le seul Sauveur

1 Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu.
Esaïe 43.7 Zacharie 13.9 Esaïe 45.3-45.4 Esaïe 44.2 Actes 27.25
2 Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza.
Psaumes 66.12 Daniel 3.25-3.27 Psaumes 91.15 Josué 1.9 Esaïe 41.10
3 Maana mimi ni Bwana, Mungu wako; Mtakatifu wa Israeli, mwokozi wako, nimetoa Misri kuwa ukombozi wako; nimetoa Kushi na Seba kwa ajili yako.
Exode 20.2 Esaïe 49.26 Esaïe 45.15 Proverbes 21.18 Esaïe 45.21
4 Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako.
Exode 19.5-19.6 Genèse 12.2 Deutéronome 32.9-32.14 Apocalypse 3.9 1 Pierre 2.9
5 Usiogope; maana mimi ni pamoja nawe; nitaleta wazao wako toka mashariki, nitakukusanya toka magharibi;
Esaïe 43.2 Esaïe 49.12 Esaïe 44.2 Jérémie 30.10-30.11 Ezéchiel 36.24-36.27
6 nitaiambia kaskazi, Toa; nayo kusi, Usizuie; waleteni wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia.
Jérémie 3.14 2 Corinthiens 6.17-6.18 Romains 9.7-9.8 Jérémie 3.18-3.19 Esaïe 18.7
7 Kila mmoja aliyeitwa kwa jina langu, niliyemwumba kwa ajili ya utukufu wangu; mimi nimemwumba, naam, mimi nimemfanya.
Ephésiens 2.10 Esaïe 43.1 Psaumes 100.3 Esaïe 43.21 Ephésiens 2.4-2.7
8 Walete vipofu walio na macho, na viziwi walio na masikio.
Ezéchiel 12.2 Esaïe 6.9 Deutéronome 29.2-29.4 Esaïe 42.18-42.20 2 Corinthiens 4.4-4.6
9 Na wakusanyike mataifa yote, kabila zote wakutanike; ni nani miongoni mwao awezaye kuhubiri neno hili, na kutuonyesha mambo ya zamani? Na walete mashahidi wao, wapate kuhesabiwa kuwa na haki; au na wasikie, wakaseme, Ni kweli.
Esaïe 41.1 Esaïe 43.26 Esaïe 45.20-45.21 Esaïe 48.5-48.6 Joël 3.11
10 Ninyi ni mashahidi wangu, asema Bwana, na mtumishi niliyemchagua; mpate kujua, na kuniamini, na kufahamu ya kuwa mimi ndiye; kabla yangu hakuumbwa Mungu awaye yote, wala baada yangu mimi hatakuwapo mwingine.
Esaïe 41.4 Esaïe 45.6 Esaïe 43.12 Esaïe 46.8-46.9 Esaïe 44.6-44.8
11 Mimi, naam, mimi, ni Bwana, zaidi yangu mimi hapana mwokozi.
Osée 13.4 Luc 2.11 Esaïe 12.2 Tite 2.13 Esaïe 43.3
12 Nimetangaza habari, nimeokoa, nimeonyesha, na hapakuwa mungu wa kigeni kati yenu; kwa sababu hiyo ninyi ni mashahidi wangu, asema Bwana, nami ni Mungu.
Deutéronome 32.12 Esaïe 44.8 Esaïe 43.10 Esaïe 37.20 Esaïe 46.9-46.10
13 Naam, tangu siku ya leo, mimi ndiye; wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu; mimi nitatenda kazi, naye ni nani awezaye kuizuia?
Psaumes 90.2 Esaïe 14.27 Job 9.12 Esaïe 41.4 Jean 8.58
14 Bwana, Mkombozi wenu, Mtakatifu wa Israeli, asema hivi; Kwa ajili yenu nimetuma ujumbe Babeli nami nitawashusha wote mfano wa wakimbizi, naam, Wakaldayo, katika merikebu zao walizozifurahia.
Esaïe 23.13 Esaïe 44.24-45.5 Esaïe 43.1 Apocalypse 18.11-18.21 Ezéchiel 27.29-27.36
15 Mimi ni Bwana, Mtakatifu wenu, Muumba wa Israeli, mfalme wenu.
Esaïe 43.1 Habakuk 1.12 Esaïe 48.17 Esaïe 30.11 Matthieu 25.34
16 Bwana asema hivi, yeye afanyaye njia katika bahari; na mahali pa kupita katika maji yenye nguvu;
Esaïe 51.10 Psaumes 77.19 Esaïe 51.15 Exode 14.29 Psaumes 78.13
17 atoaye gari na farasi, jeshi la askari na uwezo; wamelala, hawataondoka; wametoweka, wamezimwa mfano wa utambi.
Esaïe 1.31 Psaumes 76.5-76.6 Exode 14.4-14.9 Ezéchiel 38.8-38.18 Psaumes 118.12
18 Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
Esaïe 65.17 Esaïe 46.9 1 Chroniques 16.12 2 Corinthiens 3.10 Jérémie 23.7-23.8
19 Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani.
Esaïe 48.6 Esaïe 42.9 2 Corinthiens 5.17 Esaïe 41.18 Apocalypse 21.5
20 Wanyama wa kondeni wataniheshimu, mbweha pia na mbuni; kwa sababu nimewapa maji jangwani, na mito nyikani, ili kuwanywesha watu wangu, wateule wangu;
Esaïe 41.17 Esaïe 48.21 Esaïe 13.22 Jean 4.14 Esaïe 49.10
21 watu wale niliojiumbia nafsi yangu, ili wazitangaze sifa zangu.
1 Pierre 2.9 Psaumes 102.18 1 Corinthiens 10.31 Ephésiens 1.5-1.12 Hébreux 13.15
22 Lakini hukuniita, Ee Yakobo, bali umechoka nami, Ee Israeli.
Malachie 1.13 Michée 6.3 Malachie 3.14 Jacques 4.2-4.3 Psaumes 14.4
23 Hukuniletea wana-kondoo kuwa kafara zako, wala hukuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukutumikisha kwa matoleo, wala sikukuchosha kwa ubani.
Amos 5.25 Zacharie 7.5-7.6 Jérémie 7.22 Lévitique 2.1 Esaïe 66.3
24 Hukuninunulia manukato kwa fedha, wala hukunishibisha kwa mafuta ya sadaka zako; bali umenitumikisha kwa dhambi zako, umenichosha kwa maovu yako.
Jérémie 6.20 Esaïe 1.14 Esaïe 7.13 Psaumes 95.10 Ezéchiel 6.9
25 Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako.
Hébreux 8.12 Hébreux 10.17 Jérémie 31.34 Esaïe 1.18 Michée 7.18-7.19
26 Unikumbushe, na tuhojiane; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako.
Esaïe 1.18 Romains 8.33 Esaïe 43.9 Job 40.4-40.5 Job 40.7-40.8
27 Baba yako wa kwanza alifanya dhambi, na wakalimani wako wameniasi.
Jérémie 5.31 Esaïe 28.7 Ezéchiel 16.3 Zacharie 1.4-1.6 Malachie 2.4-2.8
28 Kwa hiyo nitawatia unajisi wakuu wa patakatifu, nami nitamfanya Yakobo kuwalaani, na Israeli kuwa tukano.
Jérémie 24.9 Zacharie 8.13 Deutéronome 28.15-28.20 Psaumes 79.4 Lamentations 2.2

Cette Bible est dans le domaine public.