Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 18.3
Bible en Swahili de l’est


Prophétie sur l’Éthiopie

1 Ole wa nchi ya uvumi wa mabawa, Iliyoko mbali kupita mito ya Kushi;
Sophonie 3.10 Ezéchiel 30.4-30.5 2 Rois 19.9 Sophonie 2.12 Psaumes 36.7
2 Ipelekayo wajumbe wake kwa njia ya bahari, Na katika vyombo vya manyasi juu ya maji. Nendeni, wajumbe wepesi,kwa watu warefu,laini; Watu watishao tangu mwanzo wao hata sasa; Taifa la wenye nguvu,wakanyagao watu, Ambao mito inakata nchi yao.
Genèse 10.8-10.9 Esaïe 18.7 2 Chroniques 16.8 2 Chroniques 12.2-12.4 2 Chroniques 14.9
3 Enyi watu mkaao katika ulimwengu wote, na wenyeji wa dunia, bendera ikiinuliwa milimani, angalieni; na wakipiga tarumbeta, sikieni.
Esaïe 5.26 Esaïe 26.11 Matthieu 13.16 Matthieu 13.9 Michée 6.2
4 Maana Bwana ameniambia hivi, Mimi nitatulia, na kuangalia katika makazi yangu, kama wakati wa mwangaza mweupe wa jua kali, mfano wa wingu la umande katika hari ya mavuno.
Esaïe 26.21 Osée 5.15 Esaïe 18.7 2 Samuel 23.4 Joël 3.17
5 Maana kabla ya mavuno, maua yaangukapo, na maua yakawa zabibu zianzazo kuiva, ndipo atakapoyakata matawi kwa miundu, na kuviondoa vitawi vilivyopanuka na kuvikata.
Cantique 2.13 Ezéchiel 17.6-17.10 Cantique 2.15 Esaïe 17.10-17.11
6 Wote pamoja wataachiwa ndege wakali wa milimani, na hayawani wa nchi; ndege wakali watakaa juu yao wakati wa jua, na hayawani wote wa nchi watakaa juu yao wakati wa baridi.
Jérémie 7.33 Ezéchiel 39.17-39.20 Ezéchiel 32.4-32.6 Esaïe 56.9 Esaïe 14.19
7 Wakati huo Bwana wa majeshi ataletewa hedaya na watu warefu, laini; Watu watishao tangu mwanzo wao hata sasa; Taifa la wenye nguvu, wakanyagao watu, Ambao mito inakata nchi yao; mpaka mahali pa jina la Bwana wa majeshi,mlima Sayuni.
Esaïe 18.4 Sophonie 3.10 2 Chroniques 32.23 Zacharie 14.16-14.17 Esaïe 45.14

Cette Bible est dans le domaine public.